Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w16 Mwezi wa 4 uku. 31-32
  • Kazi Yako Ya Kuhubiri Iko Kama Umande?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kazi Yako Ya Kuhubiri Iko Kama Umande?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Vichwa Vidogo
  • NAMNA GANI KAZI YETU YA KUHUBIRI INAWEZA KUWA KAMA UMANDE?
  • UPENDEZWE NA KAZI YAKO YA KUHUBIRI
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
w16 Mwezi wa 4 uku. 31-32
Picha ya Shahidi mumoja mwenye kuhubiri mwanaume fulani, wote wako katika tone la umande

Kazi Yako Ya Kuhubiri Iko Kama Umande?

KAZI yetu ya kuhubiri ni ya maana na yenye kupendeza. Lakini watu wote wenye tunahubiria hawaone hivyo. Watu wanapendezwa na mambo yenye Biblia inasema, lakini wakati fulani hawaone kwamba ni jambo la lazima kujifunza Neno la Mungu pamoja na sisi.

Tuchukuwe mufano wa Gavin. Alikuwa anahuzuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme, lakini hakupenda kujifunza Biblia. Gavin anaeleza kwamba hakujua mambo mengi juu ya Biblia na hakupenda wengine wajue jambo hilo. Alikuwa anaogopa kujiunga na dini fulani, na hakupenda adanganywe. Unawaza nini? Ilikuwa mwepesi kumusaidia Gavin? Fikiria namna mafundisho ya Biblia yanaweza kuwa na matokeo ya muzuri juu ya mutu fulani. Yehova aliwaambia Waisraeli hivi: “Maneno yangu yatadondoka [yataanguka] kama umande, kama mvua ya rasharasha juu ya majani.” (Kumbukumbu la Torati 31:19, 30; 32:2) Tujifunze basi mambo fulani juu ya umande na kuulinganisha na kazi yetu ya kuhubiri ili tuweze kupata matokeo ya muzuri wakati tunasaidia “watu wa namna zote.”—1 Timotheo 2:3, 4.

NAMNA GANI KAZI YETU YA KUHUBIRI INAWEZA KUWA KAMA UMANDE?

Umande unatuliza. Umande unafanyizwa polepole katika hewa kisha unabadilika na kuwa matone madogo-madogo ya maji. Namna gani maneno ya Yehova ‘yalidondoka kama umande’? Alisema na watu wake kwa utulivu, kwa upole, na kwa njia yenye kuonyesha kwamba anawahangaikia. Tunaiga mufano wake wakati tunaheshimia mambo yenye wengine wanaamini. Tunawatia moyo wafikiri na kuchukua maamuzi wao wenyewe. Wakati tunaonyesha kwamba tunawahangaikia hivyo, wanakuwa tayari kabisa kukubali mambo yenye tunasema, na tunapata matokeo mazuri zaidi katika kazi yetu ya kuhubiri.

Umande unatia nguvu. Kazi yetu ya kuhubiri itatia wengine nguvu ikiwa tunafikiria njia mbalimbali zenye tunaweza kutumia ili kuwasaidia wajifunze mengi zaidi juu ya kweli. Ndugu Chris, mutu wa kwanza mwenye alimuomba Gavin ajifunze Biblia pamoja naye, hakumukaza akubali. Lakini, alijikaza kutafuta njia mbalimbali zenye angeweza kutumia ili kumusaidia Gavin akuwe tayari kujifunza Biblia. Ndugu Chris alimuambia Gavin kwamba Biblia iko na ujumbe wa maana, na kwamba kujifunza ujumbe huo kutamusaidia aelewe muzuri maana ya mikutano. Kisha, ndugu Chris alimuelezea kwamba unabii wa Biblia ulimusadikisha kwamba Biblia inasema kweli. Kwa hiyo, walizungumuzia mambo mengi yenye kuonyesha namna unabii mbalimbali wa Biblia ulitimia. Mazungumuzo hayo yalimutia nguvu Gavin, na alikubali kujifunza Biblia.

Umande ni wa lazima ili uzima uendelee. Wakati wa kipwa katika Israeli, mvua inaweza kufanya miezi mingi bila kunyesha. Bila umajimaji wenye umande unaleta, mimea inakauka na inakufa. Yehova alitabiri kwamba wakati wetu kungekuwa hali yenye kufanana na kipwa, ni kusema, watu wangekuwa na kiu ya “kuyasikia maneno ya Yehova.” (Amosi 8:11) Aliahidi kwamba Wakristo watiwa-mafuta wangekuwa “kama umande kutoka kwa Yehova” wakati wangekuwa wanahubiri habari njema ya Ufalme pamoja na “kondoo wengine.” (Mika 5:7; Yohana 10:16) Yehova ana mupango wa kupatia uzima wale wenye kuwa na kiu kwa ajili ya kweli; ujumbe wenye tunahubiri ni sehemu ya mupango huo. Tunaona ujumbe huo kuwa wenye kupendeza?

Umande ni baraka kutoka kwa Yehova. (Kumbukumbu la Torati 33:13) Ujumbe wetu unaweza kuwa baraka, ao zawadi, kwa wale wenye tunahubiria. Funzo la Biblia lilikuwa baraka kwa Gavin, kwa sababu lilimusaidia apate majibu ya maulizo yake yote. Alifanya maendeleo bila kukawia na kubatizwa, na leo anafurahia kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme pamoja na bibi yake Joyce.

Mashahidi wa Yehova wanahubiri mahali kwenye bisi inasimama

Mashahidi wa Yehova wanaeneza habari njema ya Ufalme katika dunia yote

UPENDEZWE NA KAZI YAKO YA KUHUBIRI

Kulinganisha kazi yetu ya kuhubiri na umande kunaweza pia kutusaidia tuelewe kwamba bidii yetu katika kazi ya kuhubiri ni ya lazima sana. Namna gani? Matone kidogo ya yanasaidia kwa kiasi fulani, lakini ikiwa kuna matone mengi ya umande, udongo unajaa umajimaji mwingi. Vilevile, tunaweza kuona kuwa hatutimize mambo mengi katika kazi ya kuhubiri. Lakini kutumika pamoja na mamilioni ya ndugu na dada kunatusaidia tuhubirie “mataifa yote.” (Mathayo 24:14) Kazi yetu ya kuhubiri italetea wengine baraka ya Yehova? Ndiyo, ujumbe wetu utakuwa kama vile tu umande, ni kusema, wenye kutuliza, wenye kutia nguvu, na wenye kufanya uzima uendelee!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine