Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Alimufungulia Mungu Moyo Katika Sala
    Tuige Imani Yao
    • 15, 16. (a) Kwa sababu Hana anamufungulia Yehova moyo, na anaendelea kumuabudu kwenye hema ya ibada, anajisikia namna gani? (b) Namna gani tunaweza kufuata mufano wa Hana tunapolemewa na magumu ao huzuni?

      15 Matokeo yanakuwa namna gani wakati Hana anamufungulia Yehova moyo na anaendelea kumuabudu kwenye hema ya ibada? Biblia inasema hivi: ‘Mwanamuke huyo akaenda zake, akakula chakula, na uso wake haukuwa tena na huzuni.’ (1 Sam. 1:18, La Sainte Bible en Swahili de la R. D. Congo) Hana anajisikia mwenye kutulizwa. Tunaweza kusema kama alitia uzito wa mahangaiko yake kwenye mabega ya mutu mwenye nguvu sana kuliko yeye, ni kusema, Baba yake wa mbinguni. (Soma Zaburi 55:22.) Je, kuna tatizo lolote linaloweza kumushinda? Hakuna hata kidogo: iwe jana, iwe leo ao kesho!

      16 Tunapojisikia kulemewa, magumu yanatupita ao tuna huzuni kupita kiasi, ni vizuri kufuata mufano wa Hana na kuzungumuza na Yehova ‘Musikiaji wa sala’ bila kusita. (Zab. 65:2) Tukifanya hivyo kwa imani, kuliko kuwa na huzuni, tutakuwa na “amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote.”—Flp. 4:6, 7.

  • Alimufungulia Mungu Moyo Katika Sala
    Tuige Imani Yao
    • 18 Ni wakati gani kabisa Penina alitambua kuwa uchokozi wake haumuhuzunishe tena Hana? Biblia haizungumuzie jambo hilo, lakini maneno ‘uso wake haukuwa tena na huzuni,’ yanaonyesha kama kuanzia wakati huo Hana alirudiliwa na furaha yake. Kwa vyovyote, Penina aliona kama mazarau yake hayakuwa na matokeo juu ya Hana. Na Biblia haitaje tena jina la Penina.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine