Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 15/8 uku. 28-30
  • Elisha Aliona Magari ya Vita Yenye Moto​—Je, Wewe Pia Unayaona?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Elisha Aliona Magari ya Vita Yenye Moto​—Je, Wewe Pia Unayaona?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ELISHA ANAANZA KUMUTUMIKIA ELIYA
  • ELISHA ALISHIKAMANA NA MUGAWO WAKE
  • “OMBA LILE NINALOPASWA KUKUTENDEA”
  • MAMBO AMBAYO ELISHA ALIONA
  • ELISHA ALIMUTUMAINIA YEHOVA
  • Jeshi la Yehova Lenye Farasi na Magari ya Vita ya Moto
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Namna Wazee Wanazoeza Wengine ili Wafikie Madaraka
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 15/8 uku. 28-30
[Picha katika ukurasa wa 28]

Elisha Aliona Magari ya Vita Yenye Moto​—Je, Wewe Pia Unayaona?

Mufalme wa Siria alikuwa akimuwinda nabii wa Mungu Elisha na alimupata kwenye muji wa Dothani, muji wenye kuzungukwa na kuta unaopatikana juu ya mulima. Usiku, mutawala wa Siria alituma farasi, magari ya vita, na vikundi vya askari huko Dothani. Ilipokuwa asubuhi, majeshi yake yalikuwa yameuzunguka muji huo.​—2 Fal. 6:13, 14.

Mutumishi wa Elisha alipoamuka na kwenda inje, aliona watu hao waliokuja kumukamata nabii. Kwa hiyo, alilia hivi: “Ole, bwana wangu! Tutafanya nini?” Lakini, Elisha alimuambia hivi: “Usiogope, kwa maana wale walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.” Kisha nabii huyo alisali hivi: ‘Ee Yehova, tafazali fungua macho yake, ili aone.’ Masimulizi hayo yanaendelea hivi: ‘Mara moja Yehova akafungua macho ya yule mutumishi, hivi kwamba akaona; na, tazama! lile eneo lenye milima lilikuwa limejaa farasi na magari ya vita yenye moto kumuzunguka Elisha pande zote.’ (2 Fal. 6:15-17) Jambo hili na mambo mengine yaliyotokea katika maisha ya Elisha yanatufundisha nini?

Elisha alibaki mutulivu hata ikiwa jeshi la Siria lilikuwa limeuzunguka muji kwa sababu alimutumainia Yehova na aliona namna Mungu alivyotumia nguvu zake ili kumulinda. Hatutazamie miujiza leo, lakini tunajua kwamba Yehova anawalinda watumishi wake kwa ujumla. Sisi pia tumezungukwa na farasi na magari ya vita yenye moto katika maana fulani. Ikiwa ‘tunaona’ magari hayo kwa macho yetu ya imani na ikiwa siku zote tunamutegemea Mungu, ‘tutakaa kwa usalama’ na tutapokea baraka za Yehova. (Zab. 4:8) Acheni tuone namna tunavyoweza kufaidika na mambo mengine yaliyotokea katika maisha ya Elisha.

ELISHA ANAANZA KUMUTUMIKIA ELIYA

Wakati mumoja, Elisha alipokuwa analima shamba, nabii Eliya alimukaribia na kumutupia vazi lake. Elisha alijua maana ya jambo hilo. Kwa hiyo, alifanya karamu, aliwaaga baba na mama yake, na aliondoka nyumbani kwao ili aende kumutumikia Eliya. (1 Fal. 19:16, 19-21) Kwa kuwa Elisha alikuwa tayari kuacha shuguli zake ili awe na wakati mwingi wa kumutumikia Mungu, Yehova alimutumia na baadaye alikuwa nabii pa nafasi ya Eliya.

Labda Elisha alimutumikia Eliya kwa miaka sita. Kwa miaka yote hiyo, ni Elisha aliyekuwa ‘akimimina maji juu ya mikono ya Eliya.’ (2 Fal. 3:11) Katika siku hizo, kwa kawaida watu hawakutumia kanya, vijiko, visu ao vitu vingine vinavyotumiwa ili kula chakula. Kisha kumaliza kula, mutumishi alinawisha bwana wake mikono. Kwa hiyo, kazi fulani ambazo Elisha alifanya zilikuwa za hali ya chini. Hata hivyo, aliona kumutumikia Eliya kuwa pendeleo.

Leo, Wakristo wengi wako katika namna mbalimbali za utumishi wa wakati wote. Wanafanya hivyo kwa sababu wanachochewa na imani na wanatamani kutumia nguvu zao kadiri wanavyoweza ili kumutumikia Yehova. Migawo ya wengine inawaomba waache familia zao, kwa hiyo wanaenda kufanya kazi ambazo wengi wanaona kuwa za hali ya chini, kama vile kutumika kwenye Beteli, katika ujenzi wa majengo ya ibada na mambo mengine. Kwa kuwa Yehova anaona kazi hizo kuwa za maana sana, Mukristo yeyote hawapaswi kuziona kuwa za hali ya chini ao zenye kuzaraulisha.​—Ebr. 6:10.

ELISHA ALISHIKAMANA NA MUGAWO WAKE

Mbele ya ‘kumuchukua Eliya kwenda juu kuelekea mbinguni katika zoruba ya upepo,’ Yehova alimwambia aondoke Gilgali mupaka Beteli. Eliya alimuambia Elisha, mutumishi wake, asimufuate, lakini yeye alimujibu hivi: “Mimi sitakuacha.” Walipoendelea na safari, Eliya alimuambia tena mara mbili abaki, lakini Elisha hakukubali. (2 Fal. 2:1-6) Elisha alishikamana na Eliya kama vile Ruthu alivyoshikamana na Naomi. (Rut. 1:8, 16, 17) Sababu gani? Ni wazi kwamba ilikuwa sababu Elisha alifurahia sana pendeleo ambalo Mungu alimutolea la kuwa mutumishi wa Eliya.

Elisha alituachia mufano muzuri. Ikiwa tunapewa pendeleo fulani la utumishi katika tengenezo la Mungu, tutaliona kuwa la maana sana ikiwa tunaamini katika moyo wetu kwamba ni Yehova ndiye tunayetumikia. Hakuna pendeleo nzuri zaidi kuliko kumutumikia Mungu.​—Zab. 65:4; 84:10.

“OMBA LILE NINALOPASWA KUKUTENDEA”

Kadiri wanaume hao wawili walivyoendelea na safari yao, Eliya alimuambia Elisha hivi: “Omba lile ninalopaswa kukutendea kabla sijachukuliwa kutoka kwako.” Ombi la Elisha lilifanana na lile ambalo Sulemani alifanya miaka fulani hapo zamani kwa sababu lilihusu mambo ya kiroho. Elisha aliomba ‘sehemu mbili za roho ya Eliya zije juu yake.’ (1 Fal. 3:5, 9; 2 Fal. 2:9) Katika Israeli, muzaliwa wa kwanza alipaswa kupokea sehemu mbili za uriti. (Kum. 21:15-17) Kwa hiyo basi, Elisha alitaka atambuliwe kuwa muriti wa kiroho wa Eliya. Zaidi ya hilo, inaonekana kwamba Elisha alitaka kuwa na roho ya ujasiri kama ile ya Eliya, aliyekuwa “na wivu kwelikweli kwa ajili ya Yehova.”​—1 Fal. 19:13, 14.

Eliya alitenda namna gani kuhusiana na ombi la mutumishi wake? Nabii huyo alimuambia Elisha hivi: “Umeomba jambo gumu. Ukiniona wakati nitakapochukuliwa kutoka kwako, itakuwa hivyo kwako; lakini kama sivyo, haitakuwa hivyo.” (2 Fal. 2:10) Inaonekana kwamba jibu la Eliya lilikuwa na maana mbili. Kwanza, ni Mungu tu ndiye angeamua ikiwa Elisha atapewa jambo aliloomba. Pili, ikiwa Elisha angependa kupewa jambo aliloomba, alipaswa kuazimia kubaki na Eliya hata kutokee nini.

MAMBO AMBAYO ELISHA ALIONA

Mungu alijibu namna gani ombi la Elisha la kutaka apewe sehemu mbili za roho ya Eliya? Masimulizi hayo yanaendelea hivi: ‘Na ikawa kwamba walipokuwa wanatembea, wakizungumuza huku wakitembea, tazama! gari la vita lenye moto na farasi wenye moto, nao wakawatenganisha hao wawili; na Eliya akaanza kupanda katika ile zoruba ya upepo kuelekea mbinguni. Wakati huo wote Elisha alikuwa akiona jambo hilo.’a Hivyo ndivyo Yehova alivyojibu ombi la Elisha. Elisha alimuona Eliya akichukuliwa kutoka kwake, alipokea sehemu mbili ya roho ya Eliya, na alifikia kuwa muriti wa kiroho wa nabii huyo.​—2 Fal. 2:11-14.

Elisha aliokota vazi ambalo lilikuwa limeanguka kutoka kwa Eliya na kulivaa. Vazi hilo lilimutambulisha kuwa nabii wa Mungu. Jambo lingine lililoonyesha kwamba Elisha alikuwa amechaguliwa kuwa nabii lilionekana baadaye alipofanya muujiza wa kugawanya maji ya Muto Yordani.

Bila shaka, Elisha alishangazwa sana na mambo aliyoona wakati Eliya alichukuliwa katika zoruba ya upepo. Sababu gani? Sababu si jambo la kawaida kuona gari la vita lenye moto na farasi zenye moto! Mambo hayo yalihakikisha kwamba Yehova alijibu ombi la Elisha. Bila shaka, Mungu anapojibu sala zetu, sisi hatuone katika maono magari ya vita yenye moto ao farasi zenye moto. Lakini tunaweza kutambua kwamba Mungu anatumia nguvu zake kubwa ili mapenzi yake yafanyike. Na tunapoona namna Yehova anavyobariki sehemu inayoonekana ya tengenezo lake hapa duniani, ni kama vile ‘tunaona’ gari lake la mbinguni likisonga mbele.​—Eze. 10:9-13.

Elisha alijionea mambo mengi yaliyomuhakikishia kwamba Yehova ana nguvu nyingi sana. Zaidi ya hayo, roho takatifu ya Mungu ilimuwezesha Elisha kufanya miujiza 16​—hesabu hiyo ilizidi mara mbili hesabu ya miujiza ambayo Eliya alifanya.b Mara ya pili ambayo Elisha aliona farasi na magari ya vita yenye moto ilikuwa wakati ambao majeshi yalizunguka muji wa Dothani kama ilivyoelezwa mwanzoni mwa habari hii.

ELISHA ALIMUTUMAINIA YEHOVA

Ijapokuwa alizungukwa na maadui huko Dothani, Elisha alibaki mutulivu. Sababu gani? Sababu alikuwa amesitawisha imani yenye nguvu kumuelekea Yehova. Sisi pia tunahitaji imani kama hiyo. Kwa hiyo, tunapaswa kumuomba Mungu roho yake takatifu ili tuwe na imani na sifa zingine za tunda la roho ya Mungu.​—Lu. 11:13; Gal. 5:22, 23.

Jambo lililotokea huko Dothani lilimutolea pia Elisha sababu nzuri ya kumutumainia Yehova na majeshi yake yasiyoonekana anayotumia ili kulinda watumishi wake. Nabii huyo alitambua kwamba Mungu alikuwa ametuma majeshi ya malaika zake ili wazunguke muji na wale askari waliokuwa wameuzingira. Kwa kuwafanya maadui hao wawe vipofu, Mungu aliokoa kimuujiza Elisha na mutumishi wake. (2 Fal. 6:17-23) Wakati huo wa hatari, kama vile nyakati zingine, Elisha alionyesha imani na alimutumainia Yehova kabisa.

Kama Elisha, acheni tumutumainie Yehova Mungu. (Met. 3:5, 6) Tukifanya hivyo, “Mungu mwenyewe atatuonyesha kibali na kutubariki.” (Zab. 67:1) Bila shaka, hatuzungukwe leo na magari ya vita yenye moto na farasi zenye moto. Hata hivyo, wakati wa ‘ziki kubwa’ inayokaribia, Yehova atalinda familia yetu ya ulimwenguni pote ya ndugu na dada. (Mt. 24:21; Ufu. 7:9, 14) Tunapongojea wakati huo, acheni tukumbuke siku zote kwamba “Mungu ni kimbilio letu.”​—Zab. 62:8.

a Eliya hakwenda katika mbingu za juu ambako Yehova na malaika zake wanaishi. Soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 15/09/1997, ukurasa wa 15.

b Soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 01/08/2005, ukurasa wa 10.

USHINDI MBALIMBALI WA KISHERIA WA HIVI KARIBUNI

  • 243 Hesabu ya sasa ya ushindi mbalimbali wa kisheria kwenye mahakama makubwa ulimwenguni ambao Mashahidi wa Yehova wamepata

  • Ufaransa​—Dola milioni 8.2 Zilizorudishwa

    Hizo ndizo feza ambazo serikali ya Ufaransa iliwarudishia Mashahidi wa Yehova tarehe 11 Mwezi wa 12, 2012 kisha kesi iliyofanya miaka 15

  • Ugiriki​—Baraza la Taifa

    Tarehe 2 Mwezi wa 11, 2012, Baraza la Taifa la Ugiriki lilitambua kwamba Mashahidi wa Yehova, ambao wanajulikana sana kuwa dini ya Kikristo, wana haki ya kuwa na majengo ya ibada

  • 20 Hesabu ya kesi ambazo Mashahidi wa Yehova walishinda katika Mahakama ya Ulaya ya Haki za Kibinadamu tangu Mwezi wa 4, 2000

  • Korea Kusini​—Uamuzi wa Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Kibinadamu

    Tarehe 25/10/2012 - Korea Kusini iliombwa kuwalipa Mashahidi wa Yehova 388 kwa sababu ya kukataa kuheshimu haki yao ya kutojiunga na jeshi kwa sababu ya zamiri

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine