-
Ni Nani Aliyetunga Sheria Zinazoongoza Ulimwengu Wetu?Munara wa Mulinzi—2011 | Mwezi wa 7 1
-
-
Isitoshe, wazo la kwamba hakuna kitu kinachoishikilia dunia mahali pake linatokeza swali lingine: Ni nini kinachoongoza dunia, nyota, na sayari nyingine katika mizunguko yake? Ona maneno yenye kuvutia ambayo Mungu alimwambia Ayubu: “Je, unaweza kufunga vifungo vya kundi-nyota la Kima, au, je, unaweza kufungua kamba za kundi-nyota la Kesili?” (Ayubu 38:31) Katika maisha yake marefu, Ayubu aliona makundi hayo ya nyota yakitokea na kutoweka, usiku baada ya usiku.c Lakini kwa nini yalionekana vilevile, mwaka baada ya mwaka, miaka baada ya miaka? Ni vifungo gani vilivyofunga nyota hizo na sayari nyingine mahali pake? Bila shaka, Ayubu alistaajabu sana alipowazia mambo hayo.
Kama nyota zingekuwa zimeshikizwa kwenye miviringo fulani, vifungo ambavyo Ayubu alitaja havingehitajika. Miaka 2,000 hivi ilipita kabla ya wanasayansi kupata ujuzi zaidi kuhusu “vifungo” au “kamba” hizo zisizoonekana ambazo zinashikilia nyota na sayari mahali pake, wakati zinaposonga angani. Isaac Newton na baadaye Albert Einstein walipata umaarufu kwa uvumbuzi wao kuhusu jambo hilo. Kwa kweli, Ayubu hakujua lolote kuhusu nguvu ambazo Mungu anatumia kushikilia makundi ya nyota na sayari mahali pake. Hata hivyo, baada ya maelfu ya miaka, maneno ya kitabu cha Ayubu yaliyoandikwa kwa mwongozo wa roho ya Mungu yamethibitika kuwa ya kweli tofauti na maoni ya msomi Aristoto. Hakuna mwingine anayeweza kuwa na hekima kama hiyo isipokuwa tu Mtungaji wa sheria zinazoongoza mbingu.
-
-
Ni Nani Aliyetunga Sheria Zinazoongoza Ulimwengu Wetu?Munara wa Mulinzi—2011 | Mwezi wa 7 1
-
-
c Huenda “kundi-nyota la Kima” linarejelea kundi la nyota linaloitwa Pleiades, nalo “kundi-nyota la Kesili,” linarejelea kundi la nyota linaloitwa Orion. Inachukua makumi ya maelfu ya miaka kwa nyota kama hizo kubadilika kabisa.
-