Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/8 uku. 3-4
  • Ni Nini Kinatokea Kisha Mutu Kufa?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ni Nini Kinatokea Kisha Mutu Kufa?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Watu waliokufa wako katika hali gani?
  • Kutakuwa Ufufuo!
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Kifo Si Mwisho wa Mambo Yote!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Tumaini la Kweli juu ya Watu Tuliowapenda Waliokufa
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Watu wa Familia na Marafiki Wako Wenye Walishakufa Wanaweza Kuishi Tena!
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/8 uku. 3-4

HABARI KUBWA | WATU WALIOKUFA—WANAWEZA KUISHI TENA?

Ni Nini Kinatokea Kisha Mutu Kufa?

Watu wazima na watoto wanakusanyika pembeni ya sanduku lenye kuwa na maiti kwenye kaburi

“Niliwaza kuko nafasi tatu kwenye mutu anaweza kwenda kisha kufa: mbinguni, katika moto wa mateso, ao katika pirigatori. Nilijua kama sikukuwa mutu muzuri sana ili kwenda mbinguni ao mubaya sana ili kwenda katika moto wa mateso. Sikujua muzuri ni nini inafanyika katika pirigatori. Na nilikuwa sijasoma mambo hayo yote katika Biblia. Ni watu tu walikuwa wanasema hivyo.”—Lionel.

“Nilifundishwa kama watu wote wanaenda mbinguni kisha kufa, lakini sikuamini kabisa jambo hilo. Niliwaza kifo ni mwisho wa mambo yote na hakuna tumaini lolote kwa ajili ya watu waliokufa.”—Fernando.

Umekwisha kujiuliza hivi: ‘Ni nini kinatokea kabisa kisha mutu kufa? Watu waliokufa wenye tulikuwa tunapenda wanateseka nafasi fulani? Tutawaona tena siku moja? Ni nini kinaweza kutusaidia tusadiki kama tutawaona tena?’ Tafazali, ona mambo Biblia inafundisha. Kwanza, tuone Biblia inafananisha kifo na nini. Kisha, tutazungumuzia tumaini lenye Neno la Mungu, Biblia, linatoa.

Watu waliokufa wako katika hali gani?

JIBU LA BIBLIA: ‘Walio hai [wazima] wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajui lolote kamwe, wala hawana malipo tena, kwa maana kumbukumbu lao limesahauliwa. Yote ambayo mukono wako unapata kufanya, yafanye kwa nguvu zako zote, kwa maana hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi wala hekima katika Kaburi, mahali unapokwenda.’a—Mhubiri 9:5, 10.

Kwa kifupi, Kaburi ni mahali watu wanaenda kisha kufa; ni hali ao nafasi ya mufano kwenye hakuna ufahamu ao kazi yoyote. Mwanaume muaminifu Ayubu alielewa kuwa Kaburi ni nini? Alipoteza mali yake yote na watoto wake wote siku moja, na kisha majipu (vidonda) yenye kuleta maumivu sana yalimuota kwenye mwili wote. Alimuomba Mungu hivi: “Ungenificha katika Kaburi, kwamba ungenificha.” (Ayubu 1:13-19; 2:7; 14:13) Ni wazi kuwa Ayubu alielewa kama Kaburi ni nafasi ya kupumzikia, lakini hakuelewa kama ni nafasi ya moto wa mateso kwenye maumivu yake yangekuwa mengi zaidi.

Kuko jambo lingine la kutusaidia tuelewe hali ya watu waliokufa. Tunaweza kuchunguza habari za Biblia juu ya watu munane wenye walifufuliwa.—Soma kisanduku “Ufufuo Munane Wenye Kuzungumuziwa Katika Biblia.”

Kati ya wale watu munane wenye walifufuliwa, hakuna hata mumoja wao mwenye alisema kama alikuwa nafasi ya furaha ao ya mateso. Ikiwa watu hao walienda nafasi kama hiyo wakati walikufa, wangeambia watu juu ya jambo hilo. Na habari hiyo ingeandikwa katika Biblia ili watu wote waisome, haiko vile? Katika Maandiko, hakuna habari ya namna hiyo. Kwa kweli, watu hao munane hawakusema kitu juu ya habari hiyo. Sababu gani? Ni kwa sababu wakati walikuwa wamekufa, walikuwa katika hali ya kutojua kitu, kama vile katika usingizi muzito. Kwa kweli, wakati fulani Biblia inafananisha kifo na usingizi. Kwa mufano, wanaume waaminifu Daudi na Stefano ‘walilala usingizi katika kifo.’—Matendo 7:60; 13:36.

Basi, kuko tumaini gani kwa ajili ya watu waliokufa? Wanaweza kuamuka katika usingizi huo?

a Katika Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, neno “Kaburi” linatumiwa ili kutafsiri neno la Kiebrania “Sheoli” na neno la Kigiriki “Hadesi.” Biblia fulani zinatumia neno “kuzimu,” lakini Maandiko hayaonyeshe kuwa kuko nafasi kwenye roho za watu zinaendelea kuishi kisha watu kufa.

UFUFUO MUNANE WENYE KUZUNGUMUZIWA KATIKA BIBLIAb

Mutoto mwanaume wa mujane: Nabii Eliya alifufua mutoto mwanaume wa mujane (mwanamuke mwenye alifiwa na bwana) mwenye aliishi katika muji wa Sarefathi, kaskazini mwa Israeli.—1 Wafalme 17:17-24.

Mutoto mwanaume Mushunamu: Kisha kifo cha Eliya, Elisha mwenye alikuwa sasa nabii, alimufufua mutoto mwanaume fulani katika muji wa Shunemu na kumurudisha kwa wazazi wake.—2 Wafalme 4:32-37.

Mwanaume mwenye alitupwa katika kaburi: Maiti ya mwanaume mumoja mwenye alitoka tu kufa ilitupwa haraka-haraka katika kaburi kwenye kulikuwa mifupa ya nabii Elisha. Mwanaume huyo alifufuka wakati maiti yake iligusa mifupa ya nabii Elisha.—2 Wafalme 13:20, 21.

Mutoto mwanaume wa mujane wa Naini: Yesu alizuia watu wenye walikuwa wanaenda kuzika mutoto fulani mwanaume inje ya muji wa Naini, akamufufua na kisha akamurudisha kwa mama yake mwenye alikuwa na huzuni nyingi.—Luka 7:11-15.

Mutoto mwanamuke wa Yairo: Yairo, mukubwa wa sinagogi, alimuomba Yesu aponyeshe mutoto wake mwanamuke mwenye alikuwa mugonjwa. Wakati kidogo kisha mutoto huyo kufa, Yesu alimufufua.—Luka 8:41, 42, 49-56.

Lazaro, rafiki ya Yesu: Siku ine kisha Lazaro kufa, Yesu alimufufua mbele ya watu wengi.—Yohana 11:38-44.

Dorkasi: Mutume Paulo alifufua mwanamuke huyo mwenye alipendwa sana na watu. Alikuwa anajulikana kwa sababu ya matendo yake ya muzuri.—Matendo 9:36-42.

Eutiko: Mutume Paulo alifufua kijana Eutiko mwenye alikufa wakati alianguka kwenye dirisha la juu.—Matendo 20:7-12.

b Ufufuo wa maana zaidi, ni kusema, ufufuo wa Yesu Kristo, ulikuwa tofauti sana na ufufuo huo munane. Tutaona jambo hilo katika habari yenye kufuata.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine