SURA YA 35
Ninaweza kufanya nini juu nikuwe rafiki ya Mungu?
Magumu yenye ilimupata Jeremy njo ilifanya aone kama ni jambo ya maana sana kuwa rafiki ya Mungu. Anasema hivi: Wakati nilikuwa na miaka 12, baba yangu alituacha. Siku moja usiku nilikuwa nasali na niko ku kitanda, na nilimulilia Yehova afanye jambo fulani juu baba yangu arudie.”
Jeremy alikuwa na huzuni sana na alianza kusoma Biblia yake. Maneno yenye alisoma mu Zaburi 10:14, ilimugusa sana. Ile andiko inasema hivi juu ya Yehova: “Mwenye taabu anageuka kukuelekea wewe; wewe ndiye musaidizi wa mutoto mwenye hana baba.” Jeremy anasema hivi: “Niliona sawa vile Yehova iko anazungumuza na miye na kuniambia kama iko musaidizi wangu na Baba yangu. Kwa kweli hakuna baba muzuri sawa vile Yehova.”
IKUWE uko mu hali sawa vile ya Jeremy ao hapana, Biblia inaonyesha kama Yehova anapenda ukuwe rafiki yake. Inasema hivi: “Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.” (Yakobo 4:8) Ile inaonyesha kama Yehova anapenda ukuwe Rafiki yake hata kama hauwezi kumuona na hauko wa miaka yake.
Lakini inaomba ufanye mambo fulani juu ukuwe Rafiki ya Mungu. Kwa mufano, kama ulishapanda maua fulani mu nyumba, haiwezi komala hivi-hivi tu. Juu ikomale unapaswa kuwa unaimwangia maji na kuitia fasi yenye inafaa. Vilevile tunapaswa kufanya mambo fulani kama tunapenda kuwa marafiki wa Mungu. Sasa unaweza kufanya nini juu ukomalishe urafiki pamoja na Mungu?
Kujifunza Ni Jambo ya Maana
Juu watu wawili wakuwe marafiki sana wanapaswa kuwa wanazungumuza. Ni kusema, kila mumoja anapaswa kusikiliza mwenzake na kumuambia mawazo yake. Ni vile pia kama tunapenda kuwa marafiki wa Mungu. Kusoma na kujifunza Biblia njo njia ya kumusikiliza Mungu.—Zaburi 1:2, 3.
Lakini, pengine haufurahiake kusoma. Kuliko kusoma, vijana wengi wanapendaka kuangalia televizyo, kucheza michezo ao kupitisha wakati na marafiki wao. Lakini kama unapenda kuwa rafiki ya Mungu, haupaswe tu kufunga mikono. Unapaswa kumusikiliza kwa kujifunza Biblia.
Hata vile usiogope. Kujifunza Biblia haiko muzigo. Unaweza kufurahia kuisoma hata kama haupendake kusoma. Unapaswa kwanza kupanga programu ya kujifunza Biblia. Kijana mwanamuke mwenye kuitwa Lais anasema hivi: “Niko na programu. Ninasomaka sura moja ya Biblia kila siku kisha tu kulamuka.” Maria mwenye iko na miaka 15, naye iko na programu yake. Anasema hivi: “Ninasomaka sehemu kidogo ya Maandiko kila siku mbele nilale.”
Juu ya kuanza programu yako ya kujifunza ona kisanduku yenye kichwa, “Uijue Muzuri Biblia Yako,” kisha uandike hapa chini ni saa gani njo utakuwa unajifunza Biblia kwa dakika 30 hivi.
․․․․․
Kupanga wakati wa kujifunza ni mwanzo tu. Wakati unaanza kujifunza Biblia, utaona kama kuko sehemu za Biblia zenye hazikuwake mwepesi kuelewa. Pengine utakubaliana na hii maneno ya Jezreel mwenye iko na miaka 11. Anasema hivi: Sehemu fulani za Biblia zinakuwaka nguvu kuelewa na hazifurahishake. Kama na weye unawaza vile, usivunjike moyo. Wakati uko unasoma Biblia, ukuwe unatia mu akili kama uko unasikiliza rafiki yako, Yehova Mungu. Kadiri unajikaza kujifunza Biblia, ni vile utaifurahia, na itakuletea faida!
Kusali Ni Jambo ya Maana Sana
Sala ni zawadi ya muzuri sana. Unaweza kuzungumuza na Yehova Mungu saa yote yenye unapenda, ikuwe usiku ao muchana. Iko tayari kukusikiliza kila wakati. Zaidi ya ile, anapenda kusikiliza mambo yenye unataka kumuambia. Njo maana Biblia inakushauria hivi: “Katika kila jambo kwa sala na sala ya kumulilia Mungu pamoja na kutoa shukrani, maombi yenu yajulishwe Mungu.”—Wafilipi 4:6.
Sawa vile ile andiko inaonyesha, kuko mambo mingi yenye unaweza kuambia Yehova. Kwa mufano, unaweza kumuambia magumu yako na mambo yenye iko inakuhangaisha. Unaweza pia kumushukuru juu ya mambo yenye alishakufanyia. Kama rafiki yako anakufanyia jambo ya muzuri, unajikazaka sana kumushukuru, haiko vile? Vilevile unaweza kumushukuru Yehova juu yeye alishakufanyia mambo mingi sana kuliko marafiki wako wote.—Zaburi 106:1.
Unapenda kumushukuru Yehova juu ya mambo gani fulani? Andika ile mambo hapa chini.
․․․․․
Kwa kweli, wakati fulani na weye unaogopaka na unakuwaka na mahangaiko. Zaburi 55:22 inasema hivi: “Umutupie Yehova muzigo wako, naye atakutegemeza. Hataruhusu hata kidogo mwenye haki aanguke.”
Andika hapa chini mambo yenye inakuhangaishaka yenye ungependa kumuambia Yehova.
․․․․․
Mambo Yenye Ulishajionea mu Maisha
Kuko jambo ingine ya maana yenye hatupaswe kusahau yenye inaweza kutia nguvu urafiki wetu na Mungu. Daudi aliandika hivi: “Muonje na muone kwamba Yehova ni mwema.” (Zaburi 34:8) Daudi aliandika Zaburi ya 34 kisha kukutana na hali ya kuogopesha sana. Alikuwa anakimbia Mufalme Sauli mwenye alikuwa anapenda kumuua. Ile ilikuwa hali ya nguvu sana. Kisha alilazimika kukimbilia kwa Wafilisti wenye nao walikuwa maadui wake. Wakati Daudi aliona kama uzima wake unakuwa mu hatari, alijifanya sawa mwenda-wazimu na akakimbia.—1 Samweli 21:10-15.
Daudi hakuwaza kama aliponyoka kifo juu alikuwa mayele. Lakini alionyesha kama Yehova njo alimusaidia. Mu mustari wa ine wa ileile Zaburi ya 34 aliandika hivi: “Nilimuuliza Yehova, na akanijibu. Aliniokoa katika mambo yote yenye kuniogopesha.” (Zaburi 34:4) Kwa hiyo, mambo yenye Daudi alijionea mu maisha njo ilimufanya ashaurie wengine ‘waonje na kuona kwamba Yehova ni mwema.’
Kuko jambo fulani yenye ulishajionea mu maisha yako yenye inaonyesha kama Yehova anakuhangaikia? Kama ni vile, uiandike hapa chini. Haiko lazima ikuwe jambo fulani ya ajabu sana. Fikiria baraka zenye unapataka kila siku zenye pengine unaweza kuona kama haziko za maana sana.
․․․․․
Pengine wazazi wako wamekufundisha Biblia. Kama ni vile, ile ni baraka. Hata vile, unapaswa kufanya urafiki wa kipekee pamoja na Mungu. Mashauri yenye kuwa mu hii sura inaweza kukusaidia kufanya vile. Yehova atakubariki kama unajikaza sana kufanya vile. Biblia inasema hivi: “Muendelee kuomba, na mutapewa; muendelee kutafuta, na mutapata.”—Matayo 7:7.
ANDIKO
“Wenye furaha ni wale wenye wanatambua uhitaji wao wa kiroho”—Matayo 5:3.
PENDEKEZO
Usome kurasa ine za Biblia kila siku. Kama unafanya vile utamaliza Biblia muzima mu mwaka moja hivi.
UNAJUA . . .
Juu uko unasoma hii kitabu na uko unatumikisha mashauri ya Biblia yenye iko mu hii kitabu, ile inaonyesha kama Yehova anakuhangaikia weye kipekee.—Yohana 6:44.
MAMBO NINAPANGA KUFANYA!
Juu nipate faida wakati niko najifunza Biblia nita ․․․․․
Juu nikuwe na zoezi ya kusali nita ․․․․․
Mambo yenye ninapenda kuuliza muzazi (wazazi) wangu juu ya hii habari ni ․․․․․
UNAWAZA NINI?
● Unaweza kufanya nini juu ufurahie zaidi kujifunza Biblia?
● Juu ya nini Yehova anapenda kusikiliza sala za wanadamu hata kama hawakamilike?
● Unaweza kufanya nini juu namna yako ya kusali ikuwe muzuri zaidi?
[Wazo la fungu]
“Wakati nilikuwaka mutoto, nilikuwaka nasema mambo ileile mu sala. Leo ninajikazaka kusali juu ya mambo ya muzuri na ya mubaya ya kila siku. Juu hakuna siku mbili zenye zinafananaka, ile inanisaidiaka nisikuwe narudilia mambo ileile mu sala.”—Eve
[Kisanduku/Picha]
Uijue muzuri Biblia yako
1. Chagula habari yenye unapenda kusoma. Uombe Mungu akupatie hekima ili uelewe ile habari.
2. Uisome kwa uangalifu. Usikimbilie kumaliza. Wakati uko unasoma, uwazie mu akili mambo yenye uko unasoma. Ujiwazie uko pale kwenye mambo yenye uko unasoma iko inapitikana. Kwa mufano, jaribu kuona mambo yenye kufanyika, sikia sauti za watu, sikia harufu, na mambo ingine. Ujikaze uone tu sawa vile ulikuwaka pale!
3. Fikiri kuhusu mambo yenye umetoka kusoma. Ujiulize maulizo yenye kufuata:
● Juu ya nini Yehova aliandikishaka hii habari mu Biblia?
● Ni mufano wa watu gani njo ninapaswa kufuata, na ni mufano wa watu gani njo ninapaswa kuepuka?
● Nimejifunza mambo gani ya maana mu hii habari?
● Hii habari inanifundisha nini juu ya Yehova na namna yake ya kutenda?
4. Toa sala fupi kwa Yehova. Umuambie mambo yenye umejifunza na namna unapanga kuitumikisha mu maisha yako. Usikuwe unakosa kumushukuru Yehova kwa ajili ya zawadi yenye amekupatia, ni kusema, Neno yake, Biblia Takatifu!
[Picha]
“Neno lako ni taa ya muguu wangu, na mwangaza wa njia yangu.”—Zaburi 119:105.
[Kisanduku/Picha]
Tia mambo ya maana pa nafasi ya kwanza
Unakosaka wakati wa kusali na kujifunza Biblia? Mara mingi, ni juu ya mambo yenye unatiaka pa nafasi ya kwanza.
Pima kufanya hivi: Kamata mbeketi na utie ndani majiwe ya kabambi-kabambi. Kisha umwange ndani muchanga mupaka iyale. Mbeketi yako inayala majiwe na muchanga.
Sasa umwange ile majiwe na ile muchanga chini. Fanya tena vile: Mara hii utie kwanza muchanga mu mbeketi kisha njo utie majiwe. Majiwe inakosa fasi, haiko vile? Unawaza ni juu ya nini? Ni juu ulianza na muchanga
Ile mufano inatufundisha nini? Biblia inasema hivi: “Muhakikishe mambo ya maana zaidi.” (Wafilipi 1:10) Kama unatia mambo ya kidogo-kidogo pa nafasi ya kwanza, hautapataka wakati ya kufanya mambo ya maana zaidi mu maisha, ni kusema mambo ya kiroho. Lakini kama unafuata ile shauri ya Biblia, utapata wakati ya kufanya mambo ya kiroho na wakati kidogo ya kujifurahisha. Siri ni kujua mambo yenye unapaswa kutia pa nafasi ya kwanza!
[Picha]
Tunapaswa kufanya mambo fulani juu maua yenye tunapanda mu nyumba ikomale, vilevile tunapaswa kufanya mambo fulani juu ya kutia nguvu urafiki wetu pamoja na Mungu