-
Maulizo ya Wasomaji WetuMunara wa Mulinzi—2014 | Mwezi wa 11 15
-
-
Jambo la kufurahisha ni kwamba, andiko la Ufunuo 11:1, 2 linapatanisha matukio hayo na wakati hekalu la kiroho lilipaswa kupimwa ao kuchunguzwa. Kitabu cha Malaki sura ya 3 kinazungumuzia uchunguzi kama huo wa hekalu la kiroho, na pia wakati wa kusafishwa kwa hekalu hilo. (Mal. 3:1-4) Kazi ya uchunguzi na ya kusafisha hekalu hilo ilichukua muda gani? Ilifanyika kuanzia mwaka wa 1914 mupaka miezi ya kwanza-kwanza ya mwaka wa 1919. Muda huo ulikamata siku 1260 (miezi 42) ao siku tatu na nusu za mufano zenye zinatajwa katika Ufunuo sura ya 11.
-