Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ‘Ufalme Wako Uje’
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
    • 15, 16. Maneno “kizazi hiki” yanazungumuzia watu gani?

      15 Sasa, ni wakati gani kabisa Ufalme wa Mungu utakuja? Yesu hakusema kabisakabisa ni siku gani Ufalme huo utakuja. (Mt. 24:36) Lakini, kuna jambo fulani alisema ambalo linatuhakikishia kwamba Ufalme huo unakaribia sana. Yesu alisema kwamba Ufalme huo ungekuja kisha “kizazi hiki” kuona utimizo wa alama ambayo alitabiri. (Soma Mathayo 24:32-34.) Maneno “kizazi hiki,” yanazungumuzia watu gani? Acha sasa tuchunguze maneno hayo ya Yesu.

      16 “Kizazi hiki.” Je, maneno “kizazi hiki” yanamaanisha watu wasioamini? Hapana. Fikiria ni nani waliokuwa wasikilizaji wa Yesu wakati huo. Yesu alikuwa anaelezea unabii huo mitume wake ine ambao ‘walimukaribia faragani [peke yao].’ (Mt. 24:3) Kisha muda kidogo mitume wangetiwa mafuta kwa roho takatifu. Angalia pia maandiko mengine ya unabii huo. Mbele ya Yesu kusema juu ya “kizazi hiki,” alisema hivi: ‘Basi jifunzeni jambo hili kutokana na mutini kama mufano: Mara tu tawi lake changa linapokuwa jororo [teketeke] na kutoa majani, munajua kwamba kiangazi [majira ya jua kali] kiko karibu. Vilevile ninyi pia, wakati munaona mambo yote hayo, mujue kwamba iko karibu milangoni.’ Ni wafuasi watiwa-mafuta tu, ndio wangeona mambo ambayo yalitabiriwa na kuelewa maana ya mambo hayo, ni kusema, kuelewa kwamba Yesu ‘iko karibu milangoni.’ Lakini watu wasioamini hawangeelewa mambo hayo. Kwa hiyo, wakati Yesu alitumia maneno “kizazi hiki” alikuwa anafikiria wafuasi wake watiwa-mafuta.

      KIZAZI

      (Mt. 24:32-34)

      Yesu alisema kwamba Ufalme huo ungekuja kisha “kizazi hiki” kuona utimizo wa alama ambayo alitabiri (Soma fungu la 17, 18)

      Muchoro wa “kizazi hiki“kulingana na unabii wa Yesu katika Mathayo 32-34

      KIKUNDI CHA 1: Watiwa-mafuta ambao waliona mwanzo wa utimizo wa alama katika mwaka wa 1914

      KIKUNDI CHA 2: Watiwa-mafuta ambao wakati fulani waliishi kipindi kimoja na kikundi cha kwanza; wamoja kati yao wataona ile ziki kubwa

      17. Neno “kizazi” na maneno “mambo yote hayo” yanamaanisha nini?

      17 ‘Hakitapita kamwe mupaka mambo yote hayo yatokee.’ Maneno hayo yangetimia namna gani? Ili kujibu ulizo hilo, tunapaswa kwanza kujua mambo mawili: 1) maana ya neno “kizazi;” na 2) maana ya maneno “mambo yote hayo.” Mara nyingi neno “kizazi” linamaanisha watu wa miaka tofauti, ambao maisha yao yanapatana katika kipindi fulani cha wakati. Kwa kawaida kizazi hakichukue muda murefu kupita kiasi, na kina mwisho wake. (Kut. 1:6) Maneno “mambo yote hayo,” yanamaanisha matukio yote ambayo yalitabiriwa kwamba yatatokea wakati wa kipindi cha kuwapo kwa Yesu, ni kusema, kuanzia mwanzo wa kipindi hicho katika mwaka wa 1914 mupaka mwisho wa ile ‘ziki kubwa.’—Mt. 24:21.

      18, 19. Namna gani tunaweza kuelewa maneno ya Yesu kuhusu “kizazi hiki,” na kwa hiyo tunaweza kusema nini?

      18 Kwa hiyo, namna gani tunaweza kuelewa maneno ya Yesu kuhusu “kizazi hiki”? Kile kizazi kinachozungumuziwa ni vikundi viwili vya Wakristo watiwa-mafuta ambao maisha yao yanapatana katika kipindi fulani cha wakati. Kikundi cha kwanza ni wale watiwa-mafuta ambao waliona mwanzo wa utimizo wa alama katika mwaka wa 1914. Na kikundi cha pili ni wale watiwa-mafuta ambao wakati fulani waliishi kipindi kimoja na kikundi hicho cha kwanza. Hata hivyo, wamoja kati ya wale watiwa-mafuta wa kikundi cha pili wataona mwanzo wa ile ziki kubwa. Vikundi hivyo viwili vinafanyiza kizazi kimoja kwa sababu wakati fulani viliishi katika kipindi kimoja.c

      19 Tuseme nini basi? Tunajua kwamba alama ya kuwapo kwa Yesu katika Ufalme inaonekana wazi katika dunia yote. Pia, tunaona kwamba wale Wakristo watiwa-mafuta, ambao wangali wazima na wanaofanyiza sehemu ya “kizazi hiki” wamezeeka. Lakini, hawatakufa wote mbele ya ziki kubwa kuanza. Kwa hiyo, tunaweza kusema kwamba karibuni kabisa Ufalme wa Mungu utakuja na kutawala dunia yote! Tutakuwa wenye furaha sana kujionea utimizo wa maneno haya: ‘Ufalme wako uje’! Maneno yanayopatikana katika sala ambayo Yesu alitufundisha.

  • ‘Ufalme Wako Uje’
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine