Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb17 Mwezi wa 12 uku. 5
  • Sehemu Mupya Kwenye Mukutano Wetu wa Katikati ya Juma

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sehemu Mupya Kwenye Mukutano Wetu wa Katikati ya Juma
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mufalme Anaingia Yerusalemu Akiwa Juu ya Mwana-punda
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • A7-G Matukio Makubwa ya Maisha ya Yesu Katika Dunia—Utumishi wa Mwisho wa Yesu Katika Yerusalemu (Sehemu ya 1)
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • Yehova Anaona “Amina” Yako Kuwa ya Maana
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
mwb17 Mwezi wa 12 uku. 5
Injili ya Mathayo katika Biblia New World Translation ya funzo yenye kupatikana kwenye jw.org

MAISHA YA MUKRISTO

Sehemu Mupya Kwenye Mukutano Wetu wa Katikati ya Juma

Kuanzia Mwezi wa 1, 2018, mukutano wetu wa katikati ya juma utakuwa na habari mbalimbali zenye zimechukuliwa katika Biblia New World Translation of the Holy Scriptures (nwtsty) ya funzo yenye kupatikana kwenye jw.org; tutachunguza habari hizo hata kama hazijapatikana katika luga yetu. Tuko hakika kama habari hizo zitatusaidia tujitayarishe muzuri kwa ajili ya mikutano. Jambo la maana zaidi, habari hizo zinaweza kutusaidia tumukaribie zaidi Baba yetu mwenye upendo, Yehova!

KWA AJILI YA FUNZO

Sehemu hiyo inatutolea habari zaidi kuhusu tabia, luga, na eneo zenye kuzungumuziwa katika maandiko mbalimbali ya Biblia.

Mathayo 12:20

Utambi wa kitani unaotoa moshi: Taa yenye ilitumiwa sana ilikuwa chombo kidogo cha udongo chenye kilijazwa mafuta ya muzeituni. Utambi ulinyonya mafuta ili kuwasha moto. Maneno ya Kigiriki yenye kutafsiriwa “utambi wa kitani unaofifia” yanaweza kumaanisha utambi wenye unatoa moshi kwa sababu majivu inafanya mwangaza wa moto ufifie ao uzimike. Unabii wa Isaya 42:3 ulizungumuzia namna Yesu angewasikilia watu huruma; hangezima mwangaza wa moto wa mwisho wa tumaini la watu wapole na wenye kuteswa.

Mathayo 26:13

Kwa kweli: Kigiriki, a·menʹ, Kiebrania ʼa·menʹ, maana yake “ikuwe hivyo,” ao “bila shaka.” Yesu alizoea kutumia maneno hayo mbele ya kutaja jambo, unabii, ao ahadi fulani; kwa kufanya hivyo alionyesha kama ni ya kweli kabisa na yenye kutegemeka. Wakati maneno hayo yanarudiliwa mara mbili (a·menʹ a·menʹ), kama vile katika Injili ya Yohana, maneno hayo ya Yesu yanatafsiriwa “kwa kweli kabisa.”​—Yoh 1:51.

PICHA NA VIDEO

Picha, karte, na video zenye hazina sauti zinaonyesha habari zaidi kuhusu mambo yenye kuzungumuziwa katika Biblia.

Betfage, Mulima wa Mizeituni, na Yerusalemu

Katika video hii fupi, tunaenda Yerusalemu kupitia upande wa mashariki kutokea kijiji chenye kuitwa leo et-Tur (chenye pengine ndiyo Betfage yenye kutajwa katika Biblia) na tunasimamia kwenye sehemu ya juu zaidi ya Mulima wa Mizeituni. Betania ilikuwa upande wa mashariki wa Betfage, upande wa mashariki wa Mulima wa Mizeituni. Wakati Yesu na wanafunzi wake walikuja Yerusalemu, mara nyingi walilala Betania, kwenye leo kunapatikana muji wa el-Azariye (Al Eizariya), neno la Kiarabu lenye kumaanisha “Mahali pa Lazaro.” Bila shaka Yesu alikuwa analala katika nyumba ya Marta, Maria na Lazaro. (Mt 21:17; Mk 11:11; Luka 21:37; Yoh 11:1) Wakati alikuwa anaenda kwao Yerusalemu, pengine Yesu alikuwa anafuata njia yenye kufanana na ile yenye kuonyeshwa katika video. Wakati alienda Yerusalemu tarehe 9 mwezi wa Nisani, mwaka wa 33, pengine alipanda juu ya punda katika muji wa Betfage na kuenda kwenye Mulima wa Mizeituni.

Barabara yenye pengine Yesu alitembelea kutoka Betania kuenda Yerusalemu
  1. Barabara ya kutoka Betania kuenda Betfage

  2. Betfage

  3. Mulima wa Mizeituni

  4. Bonde la Kidroni

  5. Hekalu la Milimani

Musumari ndani ya mufupa wa kisingino (sehemu ya nyuma ya muguu)

Mufupa wa kisingino cha mutu wenye kutobolewa na musumari wa chuma

Picha ya mufupa wa kisingino cha mutu wenye kutobolewa na musumari wa chuma wenye urefu wa sentimetre 11.5. Mufupa wenye ulivumbuliwa katika mwaka wa 1968, wakati walikuwa natafuta vitu vya zamani katika udongo huko Yerusalemu, ni wa wakati wa Waroma. Kuvumbua mufupa huo kunaonyesha kama pengine wakati walitundika mutu kwenye muti walitumia misumari. Pengine musumari huo unafanana na ule wenye askari walitumia ili kumutundika Yesu Kristo kwenye muti. Waliupata katika sanduku moja la majiwe lenye kuitwa sanduku la mifupa, mwenye walikuwa wanaweka mifupa ya mutu kisha mwili wake kuoza. Jambo hilo linaonyesha kama mutu mwenye alitundikwa kwenye muti angezikwa katika kaburi.​—Mt 27:35.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine