Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jy sura 115 uku. 266-uku. 267 fu. 3
  • Pasaka ya Mwisho ya Yesu Inakaribia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Pasaka ya Mwisho ya Yesu Inakaribia
  • Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Siku Hii Itakuwa Ukumbusho Kwenu”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Chakula cha Mangaribi cha Bwana
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Kristo Anasalitiwa na Kufungwa
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 115 uku. 266-uku. 267 fu. 3
Yuda anakuja kuwaona viongozi wa dini na anawauliza watamupatia nini ili amusaliti Yesu

SURA YA 115

Pasaka Ya Mwisho Ya Yesu Inakaribia

MATAYO 26:1-5, 14-19 MARKO 14:1, 2, 10-16 LUKA 22:1-13

  • YUDA ISKARIOTE ANALIPWA ILI KUMUSALITI YESU

  • MITUME WAWILI WANATAYARISHA PASAKA

Yesu anamaliza kufundisha mitume wake ine kwenye Mulima wa Mizeituni, akijibia ulizo lao kuhusu kuwapo kwake na umalizio wa mupangilio wa mambo.

Amekuwa na mambo mengi ya kufanya kabisa tarehe 11 Mwezi wa Nisani! Pengine ni wakati wako wanarudia Betania ili kulala ndio Yesu anawaambia mitume wake hivi: “Munajua kama kisha siku mbili kutakuwa Pasaka, na Mwana wa binadamu atatolewa ili auawe kwenye muti.”—Matayo 26:2.

Inaonekana kama, siku yenye kuja, Siku ya Tatu, Yesu na mitume wake watapitisha siku yenye kutulia. Siku ya Pili, alihukumu viongozi wa dini na kufunua unafiki wao waziwazi. Wanatafuta sasa kumuua. Kwa hiyo, Yesu anaepuka kujionyesha waziwazi kwenye tarehe 12 Mwezi wa Nisani ili kusikuwe jambo la kumuzuia kufanya Pasaka pamoja na mitume wake mangaribi yenye kufuata kisha jua kushuka, mwanzo wa tarehe 14 Mwezi wa Nisani.

Lakini viongozi wa dini na wazee wa watu hawajatulia mbele ya Pasaka. Wanakusanyika katika uwanja wa kuhani mukubwa Kayafa. Sababu gani? Wanakasirika sababu Yesu amekuwa akifunua unafiki wao waziwazi. Sasa wote pamoja wanatafuta namna ya “kumukamata Yesu kwa ujanja na kumuua.” Namna gani na wakati gani watafanya hivyo? Wanasema hivi: “Tusimukamate kwenye sikukuu, ili kusitokee fujo katikati ya watu.” (Matayo 26:4, 5) Wanaogopa kwa sababu wanajua kama watu wengi wanamufurahia Yesu.

Kisha viongozi wa dini wanapata mugeni. Wanashangaa kuona kwamba ni mumoja kati ya mitume wa Yesu. Shetani ameingiza katika moyo wake wazo la kumusaliti Bwana wake! Yuda anawauliza: “Mutanipatia nini ili nimusaliti kwenu?” (Matayo 26:15) Kisha kupendezwa na wazo hilo, ‘wanasikilizana kumupatia feza.’ (Luka 22:5) Ngapi? Wanasikilizana kwa furaha kumupatia vipande 30 vya feza. Hiyo inaweza kuwa vipande 30 vya shekeli vyenye kulingana na bei ya mutumwa. (Kutoka 21:32) Kwa kufanya hivyo, viongozi wa dini wanamuzarau Yesu, na kuonyesha kama hana faida. Sasa Yuda anaanza “kutafuta nafasi ya muzuri ya kumusaliti kwao bila watu wengi kuwa karibu.”—Luka 22:6.

Nisani 13 inaanza Siku ya Tatu kisha jua kutua, na huu ndio usiku wa sita, usiku wa mwisho wenye Yesu anapitisha Betania. Siku yenye kufuata, matayarisho ya mwisho yanapaswa kufanywa kwa ajili ya Pasaka. Mbele tarehe 14 Mwezi wa Nisani kuanza itaomba kupata mwana kondoo mwenye atachinjwa na kuchomwa bila kutosha sehemu yoyote. Watakulia wapi, na ni nani atatayarisha chakula? Yesu hakutoa maelezo yoyote juu ya mambo hayo. Kwa hiyo Yuda hana habari yoyote ya kutolea wakubwa wa makuhani.

Petro na Yohana wanafuata mwanaume mwenye kubeba mutungi wa maji

Siku ya Ine, pengine kisha tu muchana-kati, akiwa Betania Yesu anatuma Petro na Yohana, anawaambia: “Muende na mututayarishie Pasaka ili tuikule.” Wanajibu: “Ni wapi unataka tuitayarishie?” Yesu anawaambia hivi: “Wakati mutaingia katika muji, mwanaume mumoja mwenye kubeba mutungi wa maji atakutana na ninyi. Mumufuate katika nyumba yenye ataingia. Na muambie mwenye nyumba hiyo, ‘Mwalimu anakuambia: “Kiko wapi chumba cha wageni chenye ninaweza kukulia ndani Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?”’ Na mutu huyo atawaonyesha chumba kikubwa cha juu chenye kuwa na vifaa. Muitayarishie mule.”—Luka 22:8-12.

Bila shaka mwenye nyumba huyo ni mwanafunzi wa Yesu. Pengine anatazamia Yesu amuombe atumie nyumba yake kwa ajili ya sherehe hiyo. Wakati wanafunzi hao wawili wanaingia Yerusalemu, wanakuta kila kitu kiko kama vile Yesu aliwaambia. Wanahakikisha kwamba mwana kondoo ametayarishwa na kwamba kila kitu kiko tayari ili Yesu na mitume wake 12 wakule Pasaka.

  • Inaonekana Yesu anafanya mambo gani Siku ya Tatu, tarehe 12 Mwezi wa Nisani, na sababu gani?

  • Sababu gani viongozi wa dini wanakutana, na sababu gani Yuda anaenda kuwaona?

  • Siku ya Ine Yesu anatuma nani katika Yerusalemu, na wanafanya nini?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine