Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jy sura 117 uku. 270-uku. 271
  • Chakula cha Mangaribi cha Bwana

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Chakula cha Mangaribi cha Bwana
  • Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kristo Anasalitiwa na Kufungwa
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Chakula cha Mangaribi cha Mwisho cha Yesu
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Pasaka ya Mwisho ya Yesu Inakaribia
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Chakula cha Bwana​—Ukumbusho Unaomuletea Mungu Heshima
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Ona Habari Zaidi
Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 117 uku. 270-uku. 271
Yesu anaanzisha Chakula cha Mangaribi cha Bwana pamoja na mitume wake waaminifu 11

SURA YA 117

Chakula Cha Mangaribi Cha Bwana

MATAYO 26:21-29 MARKO 14:18-25 LUKA 22:19-23 YOHANA 13:18-30

  • YUDA ANAONYESHWA KUWA MUSALITI

  • YESU ANAANZISHA CHAKULA CHA UKUMBUSHO

Kisha tu kuanza kwa mangaribi hii, Yesu alifundisha mitume wake somo la unyenyekevu kwa kuwanawisha miguu. Sasa inaonekana kwamba kisha chakula cha Pasaka, anataja unabii huu wa Daudi: “Mutu mwenye nilikuwa ninaishi naye kwa amani, mwenye nilitumainia, mwenye alikuwa anakula mukate wangu, ameinua kisigino chake juu yangu.” Kisha anaeleza hivi: “Mumoja wenu atanisaliti.”—Zaburi 41:9; Yohana 13:18, 21.

Mitume wanaangaliana, na kila mumoja anauliza: “Bwana, je, ni mimi?” Hata Yuda naye anauliza. Petro anamwambia Yohana, mwenye kukaa pembeni ya Yesu kwenye meza, amuulize. Kisha Yohana anamukaribia Yesu na kumuuliza: “Bwana, ni nani?”—Matayo 26:22; Yohana 13:25.

Yesu anajibu hivi: “Ni ule mwenye nitapatia kipande cha mukate chenye ninaingiza katika bakuli.” Na kisha kuingiza mukate katika bakuli, anamupatia Yuda, na kusema hivi: “Kwa kweli, Mwana wa binadamu anaenda zake, kama vile iliandikwa juu yake, lakini ole kwa ule mutu mwenye anamusaliti Mwana wa binadamu! Ingekuwa muzuri zaidi kwa mutu huyo kama hangezaliwa.” (Yohana 13:26; Matayo 26:24) Kisha Shetani anaingia ndani ya Yuda. Yuda alikuwa tayari muovu, sasa anajiachilia kufanya mapenzi ya Ibilisi na kuwa “mwana wa uharibifu.”—Yohana 6:64, 70; 12:4; 17:12.

Yesu anamuambia Yuda: “Kile unafanya, ukifanye mbio sana.” Mitume wengine wanawaza kama Yesu anamuambia: “‘Nunua vitu vyenye tuko navyo lazima kwa ajili ya sikukuu,’ ao kwamba apatie maskini kitu fulani.” (Yohana 13:27-30) Lakini haiko hivyo, Yuda anaenda kumusaliti Yesu.

Mangaribi hiyohiyo, wakati wa chakula cha Pasaka, Yesu anaanzisha aina mupya ya chakula. Anakamata mukate, anatoa sala ya shukrani, anauvunja, na kuutolea mitume wake ili waukule. Anasema hivi: “Huu unamaanisha mwili wangu wenye utatolewa kwa ajili yenu. Muendelee kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.” (Luka 22:19) Kipande cha mukate kinapitishwa kati yao, na mitume wanakikula.

Sasa Yesu anakamata kikombe cha divai, anatoa sala ya shukrani, na kisha anakipitishia mitume. Kila mumoja wao anakunywa, kisha Yesu anasema: “Kikombe hiki kinamaanisha agano jipya kwa musingi wa damu yangu, yenye itamwangwa kwa ajili yenu.”—Luka 22:20.

Kwa kufanya hivyo, Yesu anaanzisha ukumbusho wa kifo chake wenye wafuasi wake wanapaswa kufanya kila mwaka tarehe 14 Mwezi wa Nisani. Itawakumbusha mambo yenye Yesu na Baba yake wamefanya ili kuwezesha wanadamu wenye imani waponyoke hukumu ya zambi na kifo. Ukumbusho unapita mambo yenye Pasaka ililetea Wayahudi kwa sababu unaletea wanadamu wenye imani ukombozi wa kweli.

Yesu anasema kama damu yake “itamwangwa kwa ajili ya wengi kwa musamaha wa zambi.” Mitume wake waaminifu na wengine wengi wako kati ya watu wengi wenye wanapata musamaha huo. Ni wao watakuwa naye katika Ufalme wa Baba yake.—Matayo 26:28, 29.

  • Yesu anataja unabii gani wa Biblia kuhusu rafiki wa karibu, na anautumia namna gani?

  • Yesu anamuambia Yuda afanye nini, lakini mitume wengine wanaelewa maneno yake namna gani?

  • Ni tukio gani la mupya Yesu anaanzisha, na liko na kusudi gani?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine