-
‘Mufanye Hivi kwa Kunikumbuka Mimi’Munara wa Mulinzi—2013 | Mwezi wa 12 15
-
-
9. Watu fulani wana maoni gani yasiyo ya kweli kuhusu mukate ambao Yesu alitumia?
9 Waamini fulani wanaonyesha kwamba Yesu alisema hivi: ‘Huu ni mwili wangu,’ kwa hiyo wanaamini kwamba mukate aliotumia uligeuka kimuujiza kuwa mwili halisi wa Yesu. Lakini, hiyo si kweli.a Yesu alikuwa mbele ya mitume wake waaminifu, na mukate usiotiwa chachu ambao wangekula ulikuwa vilevile mbele yao. Kwa kweli, Yesu alikuwa akizungumuza kwa njia ya mufano, kama vile alivyokuwa akifanya nyakati zingine.—Yoh. 2:19-21; 4:13, 14; 10:7; 15:1.
10. Mukate unaotumiwa kwenye Ukumbusho unafananisha nini?
10 Mukate ambao mitume waliona na ambao wangekula ulimaanisha mwili wa Yesu. Mwili gani? Wakati fulani, watumishi wa Yehova walifikiri kwamba kwa sababu Yesu alivunja mukate lakini hata mufupa wake mumoja haukuvunjwa, mukate ulimaanisha “mwili wa Kristo,” ni kusema, kutaniko la watiwa-mafuta. (Efe. 4:12; Rom. 12:4, 5; 1 Kor. 10:16, 17; 12:27) Lakini, baadaye, ilionekana kwamba ikiwa tunafikiri vizuri na kuchunguza Maandiko, tutaona kwamba mukate unamaanisha mwili wa kibinadamu wa Yesu. Yesu “aliteseka katika mwili,” hata kufikia kutundikwa. Kwa hiyo, mukate unaotumiwa kwenye Ukumbusho unafananisha mwili wa kibinadamu wa Yesu ambamo ‘alichukua zambi’ zetu.—1 Pet. 2:21-24; 4:1; Yoh. 19:33-36; Ebr. 10:5-7.
-
-
‘Mufanye Hivi kwa Kunikumbuka Mimi’Munara wa Mulinzi—2013 | Mwezi wa 12 15
-
-
15, 16. Mukate unatumiwa namna gani wakati wa Ukumbusho?
15 Wakati hotuba itakuwa karibu kumalizika, musemaji ataonyesha kwamba wakati umefika ili kufanya kama Yesu alivyofanya. Kama tulivyozungumuzia hapo juu, mifano miwili itatumiwa, ni kusema, mukate usiotiwa chachu na divai nyekundu. Mifano hiyo itakuwa kwenye meza karibu na musemaji. Musemaji atasoma katika Biblia mambo ambayo Yesu alisema na kufanya alipoanzisha Ukumbusho wa kifo chake. Kwa mufano, tunasoma hivi katika kitabu cha Mathayo: “Yesu alichukua mukate na, baada ya kutoa baraka, akaumega, akawapa wanafunzi, akasema: ‘Muchukue, mukule. Huu unamaanisha mwili wangu.’” (Mt. 26:26) Yesu alivunja mukate usiotiwa chachu vipande-vipande ili kupitishia vipande hivyo mitume wake waliokuwa kila upande. Utaona kwenye Ukumbusho tutakaofanya tarehe 14 Mwezi wa 4 vipande fulani vya mukate kwenye masahani.
-