-
Anasali Wakati Iko na Huzuni NyingiYesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Wakati wanafika mahali hapo penye kupendeza, katikati ya miti ya mizeituni, Yesu anaacha nyuma mitume wake munane. Pengine wanabakia kwenye muingilio wa bustani, kwa sababu anawaambia hivi: “Mukae hapa, wakati mimi ninaenda pale kusali.” Yesu anakamata mitume tatu, ni kusema, Petro, Yakobo, na Yohana, na anaenda pamoja nao mbali katika bustani. Anakuwa na huzuni nyingi na anawaambia hivi mitume wake tatu: “Nimehuzunika sana, kiasi cha kufa. Mukae hapa na muendelee kukesha pamoja na mimi.”—Matayo 26:36-38.
-
-
Anasali Wakati Iko na Huzuni NyingiYesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Wakati alikuwa mbinguni alikuwa anaona namna Waroma walikuwa wanatesa sana watu wenye walikuwa wanaua. Kwa sababu sasa yeye ni mwanadamu mwenye anaweza kusikia mambo kama vile maumivu na woga, hangojee kwa hamu mambo yenye yanakaribia kumupata. Hata hivyo, jambo lenye kumuhangaisha zaidi ni kwamba, kufa kama vile mutu mwenye alifanya makosa makubwa kunaweza kuchafua jina la Baba yake. Katika saa kidogo, atatundikwa kwenye muti kama vile mutu mwenye amekufuru.
-