-
Yesu Anapelekwa kwa Anasi, Kisha Kwa KayafaYesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Mumoja wa walinzi mwenye alikuwa anasimama pale anamupiga Yesu kofi kwenye uso na kusema hivi kwa ukali: “Je, ni vile unajibu mukubwa wa makuhani?” Lakini kwa sababu Yesu alijua kuwa hakufanya jambo fulani la mubaya, anajibu hivi: “Kama nimesema mubaya, shuhudia ubaya huo; lakini kama yale nilisema yako sawa, sababu gani unanipiga?” (Yohana 18:22, 23) Kisha Anasi anaomba Yesu apelekwe kwa Kayafa, mukwe wake.
Sasa wale wote wenye kufanyiza Sanhedrini, ni kusema, kuhani mukubwa wa sasa, wazee wa watu, na waandishi, wamekusanyika. Wanakusanyika kwenye nyumba ya Kayafa. Sheria inakataza kusambisha mutu katika usiku wa Pasaka, lakini hilo haliwazuie kuendelea na kusudi lao la mubaya.
Kwa kweli, Kikundi hicho hakitende kwa haki hata kidogo. Kisha Yesu kumufufua Lazaro, Sanhedrini iliamua kuwa Yesu anapaswa kufa. (Yohana 11:47-53) Na siku fulani zenye zilikuwa zimepita viongozi wa dini walipanga njama ya kumukamata Yesu na kumuua. (Matayo 26:3, 4) Kwa kweli, hata mbele ya kusambishwa, tayari Yesu amekwisha kuhukumiwa kifo!
-
-
Petro Anamukana Yesu Kwenye Nyumba ya KayafaYesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Kisha Yesu kukamatwa katika bustani ya Getsemane, mitume wanamuacha, wanakimbia kwa sababu wanaogopa. Hata hivyo, wawili kati yao wanaacha kukimbia. Ni Petro “na vilevile mwanafunzi mwingine,” pengine mutume Yohana. (Yohana 18:15; 19:35; 21:24) Pengine wanamukaribia Yesu wakati anapelekwa katika nyumba ya Anasi. Wakati Anasi anamutuma Yesu kwa Kuhani Mukubwa Kayafa, Petro na Yohana wanamufuata kwa mbali. Inawezekana kuwa wanaogopea maisha yao wenyewe na wanahangaika kwa sababu ya mambo yenye yatamupata Bwana wao.
-