Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w12 1/5 uku. 3-4
  • Yesu Angejibuje?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yesu Angejibuje?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jinsi Wakristo Wanavyoweza Kuwasaidia Wengine
  • “Si Sehemu ya Ulimwengu”
  • Mafundisho ya Kikristo Yanasaidiaje Jamii?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Je, Ulijua?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Dini Inapaswa Kujiingiza mu Mambo ya Politike?
    Habari Zingine
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 1/5 uku. 3-4

Yesu Angejibuje?

Leo, watu wanaodai kumwogopa Mungu wanahisi kwamba dini inapaswa kujihusisha na siasa. Wanaamini kwamba dini inaweza kusaidia katika kutatua matatizo ya wanadamu. Hata hivyo, waamini wengine wanyoofu wanafikiri kwamba dini na siasa hazipaswi kuchanganywa. Wewe binafsi unafikiri dini inatimiza fungu gani katika siasa? Je, dini inapaswa kushirikiana na siasa?

YESU KRISTO ametajwa kuwa “mtu mwenye uvutano mkubwa zaidi katika historia ya kidini ya wanadamu.” Fikiria kama tungeweza kumuuliza Yesu swali hili, Je, dini inapaswa kujihusisha na siasa? Yesu angejibuje? Alipokuwa duniani, alijibu swali hilo kupitia maneno na matendo yake. Kwa mfano, katika Mahubiri yake ya Mlimani yanayojulikana sana, Yesu alitoa miongozo inayoweza kuwasaidia wafuasi wake kutambua jukumu wanalopaswa kutimiza katika jamii. Acha tuchunguze mambo fulani katika mahubiri hayo yanayojulikana sana.

Jinsi Wakristo Wanavyoweza Kuwasaidia Wengine

Yesu alieleza mtazamo ambao wafuasi wake wanapaswa kuwa nao kuelekea watu ulimwenguni. Alisema hivi: “Ninyi ndio chumvi ya dunia; lakini chumvi ikipoteza nguvu zake, ladha yake itarudishwaje? Haitumiki tena kwa kitu chochote bali ni ya kutupwa nje ili ikanyagwe-kanyagwe na watu. Ninyi ndio nuru ya ulimwengu. . . . Acheni nuru yenu iangaze mbele ya watu, ili wapate kuona matendo yenu mazuri na kumpa utukufu Baba yenu aliye mbinguni.” (Mathayo 5:13-16) Kwa nini Yesu alisema wafuasi wake ni kama chumvi na nuru?

Maneno ya Yesu yanadokeza kwamba wafuasi wake ni kama chumvi kwa wanadamu wote, bali si kwa kikundi fulani kidogo. Wao ni kama nuru, si kwa watu wachache, bali kwa watu wote wanaotaka kuona vizuri. Kwa kutumia maneno hayo ya mfano, Yesu alionyesha waziwazi kwamba hakutaka wafuasi wake wajitenge na jamii. Kwa nini?

Fikiria mambo yafuatayo: Chumvi haiwezi kuhifadhi chakula ikiwa haitachanganywa na chakula chenyewe. Taa haiwezi kuangaza chumbani ikiwa haitawekwa ndani ya chumba hicho. Hivyo, ni rahisi kuelewa ni kwa nini Yesu hakuwaamuru wanafunzi wake wajitenge na kwenda katika sehemu fulani ya dunia ili kuanzisha jamii za waamini. Wala hakuwaambia wafuasi wake wajitenge na watu ulimwenguni na waishi katika mashirika ya kidini. Badala yake, kama vile chumvi inavyopaswa kugusa chakula na pia nuru inavyopaswa kuangaza gizani, ndivyo Wakristo wanavyopaswa kuwasaidia watu wengine kuboresha maisha yao.

“Si Sehemu ya Ulimwengu”

Hata hivyo, maagizo ya Yesu kwamba wafuasi wake wanapaswa kushirikiana na watu wengine yanatokeza swali muhimu kuhusu mtazamo wa Wakristo kuelekea siasa. Kwa nini? Muda mfupi kabla ya kifo chake, Yesu alisali hivi kwa Mungu kwa ajili ya wafuasi wake: “Ninakuomba, si kwamba uwatoe ulimwenguni, bali uwalinde kwa sababu ya yule mwovu. Wao si sehemu ya ulimwengu, kama vile ambavyo mimi si sehemu ya ulimwengu.” (Yohana 17:15, 16) Hivyo basi, Wakristo wanawezaje kutokuwa sehemu ya ulimwengu, na wakati uleule, wajihusishe na jamii yao? Ili kujua jambo hilo, acheni tuchunguze maswali mengine matatu:

• Yesu alikuwa na maoni gani kuhusu siasa?

• Wakristo wanapaswa kufanya nini leo?

• Mafundisho ya Kikristo yanasaidiaje jamii?

[Blabu katika ukurasa wa 4]

Yesu alionyesha waziwazi kwamba hakutaka wafuasi wake wajitenge na jamii

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine