-
Mafundisho ya Kikristo Yanasaidiaje Jamii?Munara wa Mulinzi—2012 | Mwezi wa 5 1
-
-
Kutii amri ya Yesu ya ‘kufanya wanafunzi’ kunahusiana na kufuata mashauri yake ya kuwa kama chumvi na nuru kwa ulimwengu. (Mathayo 5:13, 14) Mambo hayo yanahusianaje? Na kazi hiyo inaweza kuwasaidiaje watu?
-
-
Mafundisho ya Kikristo Yanasaidiaje Jamii?Munara wa Mulinzi—2012 | Mwezi wa 5 1
-
-
Vipi kuhusu mfano wa nuru? Kama vile tu mwezi unavyoangaza nuru kutoka kwenye jua, ndivyo wafuasi wa Kristo wanavyoangaza “nuru” kutoka kwa Yehova Mungu. Wanaangaza nuru hiyo kupitia ujumbe wenye kuelimisha wanaohubiri na pia kupitia matendo yao mazuri.—1 Petro 2:12.
Zaidi ya hayo, Yesu alieleza uhusiano uliopo kati ya kuwa nuru na kuwa mwanafunzi aliposema: “Watu huwasha taa na kuiweka, si chini ya kikapu cha kupimia, bali juu ya kinara cha taa, nayo huangazia watu wote waliomo ndani ya nyumba. Vivyo hivyo acheni nuru yenu iangaze mbele ya watu.” Taa inayong’aa ambayo imewekwa juu ya kinara inaonekana na watu wote wanaoizunguka. Vilevile, kazi ya kuhubiri na matendo mengine mazuri ambayo Wakristo wa kweli wanatenda yanapaswa kuonekana waziwazi na watu wanaowazunguka. Kwa nini? Yesu alisema kwamba wale wanaoona matendo hayo mazuri watamtukuza Mungu bali si Wakristo.—Mathayo 5:14-16.
Daraka la Wakristo Wote
Yesu aliposema, “Ninyi ndio nuru ya ulimwengu” na “acheni nuru yenu iangaze,” alikuwa akiwaagiza wanafunzi wake wote. Amri ambayo Yesu alitoa haiwezi kutimizwa na watu wachache waliotawanyika katika dini mbalimbali. Badala yake, waamini wote ni “nuru.” Mashahidi wa Yehova milioni saba hivi ambao wanaishi katika nchi zaidi ya 235, wanaamini kwamba wana jukumu la kuwatembelea jirani zao na kuwaeleza kuhusu ujumbe ambao Kristo anataka wafuasi wake watangaze.
-