-
Zawadi Zenye Zilistahili MufalmeMunara wa Mulinzi—2015 | Mwezi wa 3 1
-
-
Zawadi Zenye Zilistahili Mufalme
‘Wanajimu kutoka sehemu za mashariki . . . wakafungua hazina zao na kumutolea zawadi, zahabu na ubani na manemane.’— Mathayo 2:1, 11.
NI ZAWADI gani unaweza kuchagua kutolea mutu wa maana sana? Wakati wa zamani vikolezo fulani vilikuwa vya maana sana kama zahabu, vilikuwa vya bei sana na kwa hiyo vilifanyiza zawadi zenye zilistahili kupewa mufalme.a Ndiyo maana kati ya zawadi zenye wanajimu (watu wenye kutabiri matukio kwa kuangalia nyota) walipatia ‘mufalme wa Wayahudi,’ zawadi mbili zilikuwa vikolezo vyenye harufu ya muzuri.—Mathayo 2:1, 2, 11.
Mafuta ya Zeri
Biblia inasema tena kama wakati malkia wa Sheba alimutembelea Mufalme Sulemani, ‘alimupatia talanta 120 za zahabu, na mafuta ya zeri kwa wingi sana, na mawe ya samani; na kulikuwa hakujapata kuwa na mafuta ya zeri kama yale ambayo malkia wa Sheba alimupatia Mufalme Sulemani.’b (2 Mambo ya Nyakati 9:9) Wafalme pia walimutumia Sulemani mafuta ya zeri ili kumuonyesha nia yao ya muzuri.—2 Mambo ya Nyakati 9:23, 24.
Sababu gani vikolezo na vitu vingine vyenye vilitokana na vikolezo hivyo vilikuwa vya maana sana na vya bei wakati wa zamani? Kwa sababu vilikuwa na kazi nyingi za maana; kwa mufano vilitumiwa ili kupamba mwili, katika mambo ya dini, na katika mazishi. (Soma kisanduku “Namna Vikolezo Vyenye Harufu ya Muzuri Vilitumiwa Wakati wa Zamani.”) Vikolezo vilikuwa na bei sana kwa sababu watu wengi walivinunua na kwa sababu iliomba garama kubwa ili kuvisafirisha na kuviuzisha.
KUVUKA JANGWA LA ARABIA
Kida
Wakati wa zamani, mimea fulani ya vikolezo iliota katika Bonde la Yordani. Lakini, vikolezo vingine vilitoka katika inchi zingine. Biblia inataja aina mbalimbali za vikolezo. Kati ya vikolezo vilivyojulikana sana kuna zafarani, udi, zeri, mudalasini, ubani, na manemane. Zaidi ya hivyo, kulikuwa pia vikolezo vya chakula vilivyojulikana sana kama vile bizari, mnanaa, na dili.
Vikolezo hivyo vya kigeni vilitoka katika inchi gani? Udi, kida, na mudalasini vilipatikana katika inchi zenye kujulikana leo kuwa China, India, na Sri Lanka. Vikolezo kama vile manemane na ubani vilitoka katika miti na vichaka vyenye viliota katika maeneo ya jangwa yenye kuanzia kusini mwa Arabia mupaka Somalia katika Afrika. Na nardo ni kikolezo chenye kilitoka tu India katika milima ya Himalaya.
Zafarani
Ili kufika Israeli, vikolezo vingi vilipaswa kusafirishwa kupitia Arabia. Kulingana na kitabu kimoja, hilo lilikuwa kati ya sababu zenye zilifanya Arabia ikuwe “inchi pekee iliyosafirisha biashara kati ya eneo la Mashariki na eneo la Mangaribi” katika kipindi cha miaka 2000 mbele tu ya kuzaliwa kwa Yesu. (The Book of Spices) Katika eneo la Negebu kusini mwa Israeli kulipatikana miji ya zamani, ngome, na nafasi magari ya kukokotwa yalisimama; hivyo vyote vinaonyesha kuwa wafanyabiashara wa vikolezo walikuwa wanapita hapo. Ripoti moja ya shirika la UNESCO inasema kama nafasi hizo “zinaonyesha biashara yenye faida sana . . . kutoka Arabia ya kusini mupaka Mediterania.”
“Vikolezo havikukuwa vikubwa-vikubwa, vilikuwa vya bei kali, na watu walivitafuta sana. Ilikuwa biashara yenye kupendwa sana.”—The Book of Spices
Magari ya kukokotwa yenye kubeba vikolezo hivyo vyenye harufu ya muzuri yalisafiri kwa kawaida kilometre 1800 kupitia Arabia. (Ayubu 6:19) Biblia inazungumuzia wasafiri Waishmaeli waliobeba vikolezo kama vile “ubani mweusi na zeri na gome lenye utomvu” kutoka Gileadi kuenda Misri. (Mwanzo 37:25) Watoto wa Yakobo waliuzisha Yosefu, ndugu yao, kuwa mutumwa kwa wafanyabiashara hao.
-