Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Zawadi Zenye Zilistahili Mufalme
    Munara wa Mulinzi—2015 | Mwezi wa 3 1
    • Vikolezo mbalimbali vyenye harufu ya muzuri

      Zawadi Zenye Zilistahili Mufalme

      ‘Wanajimu kutoka sehemu za mashariki . . . wakafungua hazina zao na kumutolea zawadi, zahabu na ubani na manemane.’— Mathayo 2:1, 11.

      NI ZAWADI gani unaweza kuchagua kutolea mutu wa maana sana? Wakati wa zamani vikolezo fulani vilikuwa vya maana sana kama zahabu, vilikuwa vya bei sana na kwa hiyo vilifanyiza zawadi zenye zilistahili kupewa mufalme.a Ndiyo maana kati ya zawadi zenye wanajimu (watu wenye kutabiri matukio kwa kuangalia nyota) walipatia ‘mufalme wa Wayahudi,’ zawadi mbili zilikuwa vikolezo vyenye harufu ya muzuri.—Mathayo 2:1, 2, 11.

      Mafuta ya Zeri

      Mafuta ya Zeri

      Biblia inasema tena kama wakati malkia wa Sheba alimutembelea Mufalme Sulemani, ‘alimupatia talanta 120 za zahabu, na mafuta ya zeri kwa wingi sana, na mawe ya samani; na kulikuwa hakujapata kuwa na mafuta ya zeri kama yale ambayo malkia wa Sheba alimupatia Mufalme Sulemani.’b (2 Mambo ya Nyakati 9:9) Wafalme pia walimutumia Sulemani mafuta ya zeri ili kumuonyesha nia yao ya muzuri.—2 Mambo ya Nyakati 9:23, 24.

      Sababu gani vikolezo na vitu vingine vyenye vilitokana na vikolezo hivyo vilikuwa vya maana sana na vya bei wakati wa zamani? Kwa sababu vilikuwa na kazi nyingi za maana; kwa mufano vilitumiwa ili kupamba mwili, katika mambo ya dini, na katika mazishi. (Soma kisanduku “Namna Vikolezo Vyenye Harufu ya Muzuri Vilitumiwa Wakati wa Zamani.”) Vikolezo vilikuwa na bei sana kwa sababu watu wengi walivinunua na kwa sababu iliomba garama kubwa ili kuvisafirisha na kuviuzisha.

      KUVUKA JANGWA LA ARABIA

      Kida

      Kida

      Wakati wa zamani, mimea fulani ya vikolezo iliota katika Bonde la Yordani. Lakini, vikolezo vingine vilitoka katika inchi zingine. Biblia inataja aina mbalimbali za vikolezo. Kati ya vikolezo vilivyojulikana sana kuna zafarani, udi, zeri, mudalasini, ubani, na manemane. Zaidi ya hivyo, kulikuwa pia vikolezo vya chakula vilivyojulikana sana kama vile bizari, mnanaa, na dili.

      Vikolezo hivyo vya kigeni vilitoka katika inchi gani? Udi, kida, na mudalasini vilipatikana katika inchi zenye kujulikana leo kuwa China, India, na Sri Lanka. Vikolezo kama vile manemane na ubani vilitoka katika miti na vichaka vyenye viliota katika maeneo ya jangwa yenye kuanzia kusini mwa Arabia mupaka Somalia katika Afrika. Na nardo ni kikolezo chenye kilitoka tu India katika milima ya Himalaya.

      Zafarani

      Zafarani

      Ili kufika Israeli, vikolezo vingi vilipaswa kusafirishwa kupitia Arabia. Kulingana na kitabu kimoja, hilo lilikuwa kati ya sababu zenye zilifanya Arabia ikuwe “inchi pekee iliyosafirisha biashara kati ya eneo la Mashariki na eneo la Mangaribi” katika kipindi cha miaka 2000 mbele tu ya kuzaliwa kwa Yesu. (The Book of Spices) Katika eneo la Negebu kusini mwa Israeli kulipatikana miji ya zamani, ngome, na nafasi magari ya kukokotwa yalisimama; hivyo vyote vinaonyesha kuwa wafanyabiashara wa vikolezo walikuwa wanapita hapo. Ripoti moja ya shirika la UNESCO inasema kama nafasi hizo “zinaonyesha biashara yenye faida sana . . . kutoka Arabia ya kusini mupaka Mediterania.”

      “Vikolezo havikukuwa vikubwa-vikubwa, vilikuwa vya bei kali, na watu walivitafuta sana. Ilikuwa biashara yenye kupendwa sana.”—The Book of Spices

      Magari ya kukokotwa yenye kubeba vikolezo hivyo vyenye harufu ya muzuri yalisafiri kwa kawaida kilometre 1800 kupitia Arabia. (Ayubu 6:19) Biblia inazungumuzia wasafiri Waishmaeli waliobeba vikolezo kama vile “ubani mweusi na zeri na gome lenye utomvu” kutoka Gileadi kuenda Misri. (Mwanzo 37:25) Watoto wa Yakobo waliuzisha Yosefu, ndugu yao, kuwa mutumwa kwa wafanyabiashara hao.

  • Zawadi Zenye Zilistahili Mufalme
    Munara wa Mulinzi—2015 | Mwezi wa 3 1
    • Maelezo Juu ya Vikolezo Viwili Vyenye Yesu Alipewa

      Ubani na manemane vilitokana na umajimaji wenye kunata uliopatikana kwa kukata ngozi ya miti midogo-midogo ao vichaka vyenye miiba.

      Miti ya ubani iliota Arabia katika maeneo ya kusini yaliyo pembeni ya bahari, na miti ya manemane iliota sana katika inchi zilizo kama jangwa zenye kuitwa leo Somalia na Yemeni. Vikolezo hivyo viwili vilionwa kuwa vya maana sana kwa sababu vilikuwa na harufu ya muzuri. Yehova mwenyewe alichagua vikolezo hivyo vitumiwe katika ibada yake: manemane ilikuwa kati ya vitu vyenye vilitumiwa kutengeneza mafuta matakatifu yaliyotumiwa kutia mafuta, na ubani ulikuwa kati ya vitu vyenye vilitumiwa kutengeneza uvumba mutakatifu. (Kutoka 30:23-25, 34-37) Lakini vikolezo hivyo vilitumiwa kwa njia tofauti.

      Ubani, wenye ulitumiwa sana kama uvumba, ulipaswa kuchomwa ili kutoa harufu yake ya muzuri. Lakini umajimaji wenye kunata uliotoka katika muti wa manemane, ulitumiwa moja kwa moja. Manemane inatajwa mara tatu katika habari zenye kuhusu Yesu: alipewa zawadi ya manemane wakati alikuwa mutoto (Mathayo 2:11), alipewa manemane yenye kuchangwa na divai ili kupunguza maumivu wakati alikuwa kwenye muti wa mateso (Marko 15:23), na ilikuwa kati ya vikolezo vyenye vilitumiwa ili kutayarisha mwili wake kwa ajili ya mazishi (Yohana 19:39).

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine