Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jy sura 8 uku. 24-uku. 25 fu. 5
  • Wanakimbia Mutawala Mukali

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wanakimbia Mutawala Mukali
  • Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Alikuwa Baba Muzuri wa Familia, na Mwanaume Mwaminifu
    Tuige Imani Yao
  • Aliilinda Familia Yake, Akawaandalia, na Akavumilia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Yehova Alimulinda Yesu
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
Ona Habari Zaidi
Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 8 uku. 24-uku. 25 fu. 5
Mufalme Herode anatoa amri ya kuua watoto wote wanaume katika Betlehemu

SURA YA 8

Wanakimbia Mutawala Mukali

MATAYO 2:13-23

  • FAMILIA YA YESU INAKIMBILIA MISRI

  • YOSEFU ANAHAMIA NAZARETI PAMOJA NA FAMILIA YAKE

Yosefu anamuamusha Maria ili kumupatia ujumbe wa haraka. Malaika wa Yehova ametoka tu kumutokea Yosefu katika ndoto na kumuambia hivi: “Simama, chukua ule mutoto mudogo na mama yake na ukimbilie Misri, na ukae kule mupaka wakati nitakuambia urudie; kwa maana Herode iko karibu kutafuta ule mutoto mudogo ili amuue.”—Matayo 2:13.

Bila kukawia, Yosefu, Maria na mutoto wao wanakimbia usiku. Wanafanya hivyo mbele ya wakati, kwa sababu Herode anatambua kama wanaume hao wenye elimu ya nyota wamemudanganya. Alikuwa amewaambia wamuletee habari. Lakini, walitoka katika inchi bila kufanya hivyo. Herode anakasirika sana. Kwa sababu anapenda kumuua Yesu, anatoa amri ya kuua watoto wote wanaume wa miaka mbili na kushuka wenye kuwa katika Betlehemu na maeneo yenye kuzunguka Betlehemu. Uamuzi huo ulitegemea habari yenye alisikia kupitia watu wenye elimu ya nyota wenye walitoka Mashariki.

Askari anamunyanganya mama mutoto wake mwanaume

Kuua watoto wote wanaume ni jambo lenye kuumiza sana! Hatuwezi kujua ni watoto ngapi waliuawa, lakini machozi na kilio cha mama wenye huzuni vinatimiza unabii wa Biblia wenye ulitolewa na Yeremia, nabii wa Mungu.—Yeremia 31:15.

Wakati huo, Yosefu na familia yake walikuwa wamekimbilia Misri, na wanaendelea kuishi huko. Kisha, usiku fulani malaika wa Yehova anamutokea tena Yosefu katika ndoto. Malaika huyo anamuambia hivi: “Simama, chukua ule mutoto na mama yake na uende katika inchi ya Israeli, kwa sababu wale wenye walikuwa wanatafuta uzima wa ule mutoto wamekufa.” (Matayo 2:20) Kwa hiyo, Yosefu anaamua sasa kama familia inaweza kurudia katika inchi yao. Hilo linatimiza unabii mwingine wa Biblia: Mwana wa Mungu anaitwa kutoka Misri.—Hosea 11:1.

Inaonekana Yosefu anapanga kuishi na familia yake katika Yudea, pengine karibu na muji wa Betlehemu kwenye walikuwa wanaishi mbele wakimbilie Misri. Lakini anasikia kuwa mutoto muovu wa Herode mwenye kuitwa Arkelao ndiye sasa mufalme wa Yudea. Katika ndoto ingine, Mungu anamuonya Yosefu juu ya hatari ya kuenda Yudea. Kwa hiyo Yosefu na familia yake wanasafiri kuenda mbali kaskazini na wanakaa katika muji wa Nazareti katika eneo la Galilaya, mbali na makao makubwa ya maisha ya kidini ya Wayahudi. Yesu anakomalia katika eneo hilo, na hilo linatimiza unabii mwingine wa Biblia wenye kusema: “Ataitwa Munazareti.”—Matayo 2:23.

  • Wakati watu wenye elimu ya nyota hawarudie, Mufalme Herode anafanya nini, na namna gani mutoto mudogo Yesu analindwa?

  • Wakati wanarudia kutoka Misri, sababu gani Yosefu na familia yake hawarudie Betlehemu?

  • Ni unabii gani mbalimbali unatimia katika kipindi hiki cha wakati?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine