Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/6 uku. 7-9
  • Umeonja Mukate wa Uzima?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Umeonja Mukate wa Uzima?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MUKATE WA KUTEGEMEZA MOYO WA MWANADAMU ANAYEWEZA KUFA
  • MUKATE WA UZIMA
  • Yesu Ni “Mukate wa Uzima”
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Muujiza wa Mikate Wenye Yesu Alifanya
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/6 uku. 7-9
Baba Muisraeli anavunja mukate na kupatia watoto wake

Umeonja Mukate wa Uzima?

WATEMBEAJI walikuwa na njaa. Kutembelea maeneo ya kihistoria ya muji wa Bethlehemu wa zamani kuliwafanya wawe na hamu kubwa ya kula, na walitaka kujaribu kitu fulani kisicho cha kawaida. Mumoja kati yao aliona mukahawa ambako wanapika falafel, ni kusema, njegere tamu inayochangwa na tomate, vitunguu, na mboga zingine za majani na inayoliwa pamoja na mukate unaoitwa pita. Chakula hicho kitamu kiliwapatia nguvu za kuendelea na matembezi yao.

Watembeaji hao walikuwa hawajue mukate pita, chakula cha hali ya chini, kwa hiyo kukula mukate huo, lilikuwa jambo kubwa la kutokusahau ambalo walipitia siku hiyo. Jina Bethlehemu linamaanisha “Nyumba ya Mukate,” na mukate umetengenezwa katika muji huo kwa maelfu ya miaka. (Ruthu 1:22; 2:14) Mukate unaoitwa pita ni kati ya mikate ya kawaida katika muji wa Bethlehemu leo.

Karibu miaka elfu ine iliyopita, katika muji uliokuwa karibu kusini mwa Bethlehemu, Sara, bibi ya Abrahamu, alitengeneza ‘keki za muviringo’ ili kuwalisha wageni watatu ambao hakuwa anatazamia. (Mwanzo 18:6) Inawezekana “unga laini” ambao Sara alitumia ulitokana na aina fulani ya ngano ao ulitokana na shayiri. Sara alipaswa kutayarisha mukate huo haraka na labda aliupika kwenye mawe yenye kuwa moto.—1 Wafalme 19:6.

Kama habari hii inavyoonyesha, familia ya Abrahamu ilitayarisha na kupika mukate wa kula wao wenyewe. Kwa sababu ya maisha yao ya kuhama-hama, inawezekana Sara na vijakazi wake hawangepika mukate katika aina ya majiko (fours) yaliyotumiwa katika muji wake wa Uru. Alitumia mbegu ya asili ili kutayarisha unga laini. Hiyo ilipaswa kuwa kazi ngumu iliyofanywa kwa kutumia jiwe la kusagia la mukononi na labda kino na mutwangio.

Miaka mia ine baadaye, Sheria ya Musa ilionyesha kwamba jiwe la kusagia halingepaswa kuchukuliwa kuwa rehani kwa ajili ya mukopo, kwa kuwa ilikuwa njia iliyomusaidia mutu kuishi. (Kumbukumbu la Torati 24:6) Mungu aliona jiwe la kusagia kuwa la maana kwa sababu bila jiwe hilo, familia haingetengeneza mukate wao wa kila siku.—Soma kisanduku “Kusaga Unga na Kutengeneza Mikate Kila Siku Katika Nyakati za Biblia.”

MUKATE WA KUTEGEMEZA MOYO WA MWANADAMU ANAYEWEZA KUFA

Maandiko yanazungumuzia mukate karibu mara 350, na waandikaji wa Biblia walitumia mara nyingi neno mukate ili kumaanisha chakula. Yesu alionyesha kwamba wale wanaomutumikia Mungu wanaweza kusali kwa uhakika hivi: ‘Utupe leo mukate wetu kwa ajili ya siku hii.’ (Mathayo 6:11) Hapa, neno ‘mukate’ linamaanisha chakula kwa ujumla, na kwa kusema hivyo, Yesu alionyesha kwamba tunaweza kumutegemea Mungu ili tupate chakula chetu cha kila siku.—Zaburi 37:25.

Hata hivyo, kuna kitu fulani cha maana sana kuliko mukate, ao chakula. Yesu alisema hivi: ‘Mwanadamu ataishi, si kwa mukate tu, bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Yehova.’ (Mathayo 4:4) Yesu alisema juu ya wakati ambapo Waisraeli walitegemea kabisa vitu vyenye Mungu aliwatolea. Mupango huo ulianza kisha tu kuondoka kwao Misri. Kulikuwa kumepita karibu mwezi mumoja tangu walipoingia katika Jangwa la Sinai, na chakula chao kilikuwa kimepunguka. Waisraeli waliogopa kwamba watakufa na njaa katika jangwa hilo, wakaanza kulalamika kwa uchungu hivi: ‘Tulikuwa tunakula mukate na kushiba’ huko Misri.—Kutoka 16:1-3.

Bila shaka, mukate wa Misri ulikuwa mutamu. Wakati wa Musa, mafundi wa kutengeneza mikate walikuwa wakiwatolea watu wa Misri aina mbalimbali za mikate na keki. Lakini Yehova hakuwa anakusudia kuwaacha watu wake bila mukate wa aina yoyote. Aliwaahidi hivi: ‘Tazama, nitawanyeshea mukate kutoka mbinguni.’ Kwa kweli, mukate huo kutoka mbinguni ulionekana asubuhi sana, kilikuwa “kitu laini chenye chembechembe” kilichoonekana kama umande ao barafu. Waisraeli walipokiona mara ya kwanza waliuliza hivi: “Ni nini hiki?” Musa akawafasiria hivi: ‘Ni mukate ambao Yehova amewapa ninyi uwe chakula.’ Waliita mukate huo mana,a na uliwalisha kwa miaka 40 iliyofuata.—Kutoka 16:4, 13-15, 31.

Waisraeli wanaokusanya mana, mukate kutoka mbinguni

Kwanza, Waisraeli walipendezwa na mana hiyo iliyotokea kimuujiza. Ilikuwa na onjo kama la “keki bapa zenye asali,” na kulikuwa kiasi cha kutosha kwa ajili ya kila mutu. (Kutoka 16:18) Lakini kisha wakati kupita, walianza kukumbuka aina mbalimbali za chakula walikuwa wanakula huko Misri. Walinungunika hivi: ‘Macho yetu hayaone chochote isipokuwa mana.’ (Hesabu 11:6) Baadaye walisema kwa hasira hivi: ‘Nafsi yetu imeuchukia huu mukate wa kuzaraulika.’ (Hesabu 21:5) Mwishowe, ‘mukate kutoka mbinguni’ uliwachukiza na wakaukataa.—Zaburi 105:40.

MUKATE WA UZIMA

Kwa wazi, mukate, kama vitu vingine vyote, unaweza kuonwa kwa vyepesi kuwa kitu cha ovyoovyo. Lakini Biblia inazungumuzia mukate wa aina ya pekee ambao haupaswi kuzarauliwa. Mukate huo, ambao Yesu alilinganisha na mana yenye Waisraeli walikataa hivyo bila adabu, ungeleta faida za milele.

Yesu aliwaambia wasikilizaji wake hivi: ‘Mimi ndio mukate wa uzima. Mababu zenu walikula mana nyikani [ao katika jangwa] na bado wakakufa. Huu ndio mukate ambao unashuka kutoka mbinguni, ili yeyote apate kula [mukate huo] na asikufe. Mimi ndio mukate ulio hai ulioshuka kutoka mbinguni; yeyote akikula mukate huu ataishi milele; na, kwa kweli, mukate ambao nitatoa ni mwili wangu kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.’—Yohana 6:48-51.

Wengi kati ya wasikilizaji wa Yesu hawakuelewa maana ya maneno ya mufano ‘mukate’ na “mwili” yenye Yesu alitumia. Lakini, mufano huo ulikuwa wenye kufaa sana. Mukate wa kwelikweli ulilisha Wayahudi kila siku, kama vile tu mana ilivyowalisha Waisraeli kwa miaka 40 katika jangwa. Hata ikiwa mana ilikuwa zawadi kutoka kwa Mungu, haikutoa uzima wa milele. Kwa upande mwingine, zabihu ya Yesu ndiyo tu iliyotolea wale wanaomuamini zawadi kama hiyo. Kwa kweli, yeye ni ‘mukate wa uzima.’

Labda unaposikia njaa, unachukua kipande cha mukate. Na labda unamushukuru pia Mungu kwa sababu umepata ‘mukate wako kwa ajili ya siku hiyo.’ (Mathayo 6:11) Hata ikiwa tunafurahia chakula kitamu, tusisahau hata siku moja ulazima wa ‘mukate wa uzima,’ maana yake, Yesu Kristo.

Tofauti na Waisraeli wa wakati wa Musa waliokosa shukrani, namna gani tunaweza kuonyesha kwamba hatuzarau mukate huo wa bei sana? Yesu alisema hivi: ‘Ikiwa munanipenda, mutazishika amri zangu.’ (Yohana 14:15) Ikiwa tunashika amri za Yesu, tuna tumaini la kula mukate kwa furaha milele na milele.—Kumbukumbu la Torati 12:7.

a Inawezekana neno “mana” linatokana na maneno la Kiebrania “man hu’?” yanayomaanisha “ni nini hiki?”

Kusaga Unga na Kutengeneza Mikate Kila Siku Katika Nyakati za Biblia

Mwanamuke anasaga unga kwa mukono

Kusaga unga. Mara nyingi, mwanamuke alitayarisha unga kwa mukono, hiyo ilikuwa moja kati ya kazi za nyumbani zenye alipaswa kufanya asubuhi sana. (Methali 31:15; Mathayo 24:41) Katika nyakati za wazee wa ukoo, ngano yenye watu walipanda kikawaida ilikuwa aina ya ngano iliyotokeza mbegu zilizokuwa ngumu kutoa ndani ya maganda. Hilo lilifanya kazi iwe ngumu, iliomba kutwanga ndani ya kino ao kusaga kwa kutumia jiwe la kusagia la mukononi. Kwanza, ngano hiyo iliomba itiwe maji, itwangwe, na kukaushwa kwenye jua. Kisha, ilipepetwa ili kutenganisha mbegu na maganda mbele ya kuanza kuisaga.

Kusaga unga wa kutosha kwa ajili ya familia kungechukua saa nyingi, na ‘sauti ya jiwe la kusagia la mukononi’ ilisikiwa sana katika miji mbalimbali nyakati za Biblia. (Yeremia 25:10) Majiwe makubwa ya kusagia yanayoongozwa na wanyama yalianza pia kutumiwa wakati kazi hiyo ilianza kufanywa na wasagaji kuliko kufanywa na wanawake.—Mathayo 18:6.

Mwanamuke anatosha mikate yenye kupikwa ndani ya jiko ndogo

Kutengeneza mukate. Kazi ya kufuata katika kazi za kawaida za kila siku ilikuwa kutengeneza mukate. Mwanamuke alipaswa kuchanga unga pamoja na maji, kuponda muchanganyiko huo, na kisha kupika mukate. (Mwanzo 18:6) Watu fulani walipika mukate kwenye majiwe ya moto; wengine walitumia majiko madogo-madogo. (Mambo ya Walawi 2:4; Isaya 44:15) Watu wenye kujulikana sana, kama vile Mafarao, walitegemea mafundi wa kutengeneza mikate ili wawatengenezee mukate wao, lakini miaka iliyofuata baadaye hata watu wa kawaida pia walianza kununua mukate. (Mwanzo 40:17; 1 Samweli 8:13; Isaya 55:2) Katika siku za Yeremia, muji wa Yerusalemu ulikuwa na “barabara ya waokaji [watu wanaotengeneza mikate],” na katika nyakati za Nehemia, munara moja kati ya minara ya muji huo uliitwa ‘Munara wa Majiko.’—Yeremia 37:21; Nehemia 12:38.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine