Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jy sura 48 uku. 120-uku. 121 fu. 8
  • Anafanya Miujiza, Lakini Anakataliwa Hata Katika Nazareti

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Anafanya Miujiza, Lakini Anakataliwa Hata Katika Nazareti
  • Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Anafanya Miujiza kwa Nguvu za Nani?
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Kwenye Sinagogi ya Nazareti
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Yesu Alifanya Nini Wakati Alikuwa ku Dunia?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 48 uku. 120-uku. 121 fu. 8
Watu wengi wanamufuata Yesu wakati iko anatoka kwenye nyumba ya Yairo

SURA YA 48

Anafanya Miujiza, Lakini Anakataliwa Hata Katika Nazareti

MATAYO 9:27-34; 13:54-58 MARKO 6:1-6

  • YESU ANAPONYESHA VIPOFU NA MABUBU

  • WATU KATIKA NAZARETI WANAMUKATAA

Yesu amekuwa na siku yenye mambo mengi. Kisha safari yake ya kutoka eneo la Dekapoli, Yesu aliponyesha mwanamuke mwenye kuwa na ugonjwa wa kutokwa damu na alifufua binti ya Yairo. Lakini kungali mambo mengine ya kufanya siku hiyo. Wakati Yesu iko anatoka katika nyumba ya Yairo, vipofu wawili wanaume wanamufuata na kusema kwa sauti kubwa: “Tusikilie huruma, Mwana wa Daudi.”—Matayo 9:27.

Kwa kumuita Yesu “Mwana wa Daudi,” wanaume hao wanaonyesha kama wanaamini kuwa ni muriti wa kiti cha ufalme cha Daudi na kuwa yeye ni Masiya. Yesu anafanya kama vile hasikie sauti zao, pengine ili kuona ikiwa wataendelea kuomba, na wanafanya hivyo. Wakati Yesu anaingia katika nyumba, wanaume hao wawili wanamufuata. Yesu anawauliza: “Muko na imani kwamba ninaweza kuwaponyesha?” Wanamujibu kwa uhakika wote: “Ndiyo Bwana.” Kwa hiyo, Yesu anagusa macho yao na kusema hivi: “Na ifanyike kwenu kulingana na imani yenu.”—Matayo 9:28, 29.

Mara moja wanaona! Kama vile mwanzoni aliambia wengine wenye aliponyesha, Yesu anaambia wanaume hao wasitangaze jambo lenye amefanya. Lakini kwa sababu ya furaha, wanafikia kutangaza jambo hilo mupaka maeneo ya mbali.

Wakati wanaume hao wawili wanaondoka, watu wanamuletea mwanaume mwenye haseme kwa sababu iko na pepo muchafu. Yesu anafukuza pepo huyo, na mara moja mwanaume huyo anaanza kusema. Watu wanashangaa sana kuona jambo hilo, na wanasema: “Jambo kama hili halijaonekana hata siku moja katika Israeli.” Wafarisayo wako pia hapo. Hawawezi kupinga miujiza hiyo, kwa hiyo wanarudilia mashitaka yao kuhusu ule mwenye anapatia Yesu uwezo wa kufanya miujiza. Wanasema hivi: “Anafukuza pepo wachafu kwa nguvu za mutawala wa pepo wachafu.”—Matayo 9:33, 34.

Kisha muda kidogo, Yesu anarudia Nazareti mahali kwenye alikomalia, na sasa anasindikizwa na wanafunzi wake. Kumepita karibu mwaka moja, tangu wakati alifundisha katika sinagogi ya Nazareti. Mwanzoni watu walipendezwa na mambo yenye alisema, lakini wakafikia kupinga mafundisho yake na wakajaribu kumuua. Sasa Yesu anajaribu tena kusaidia majirani wake wa zamani.

Kwenye siku ya Sabato, anarudia katika Sinagogi ili kufundisha. Watu wengi wanashangaa, na hata wanauliza: “Mutu huyu alipata wapi hekima hii na uwezo wa kufanya matendo haya yenye nguvu?” Wanasema hivi: “Je, huyu haiko mwana wa ule seremala? Mama yake haitwe Maria, na ndugu zake Yakobo, Yosefu, Simoni, na Yuda? Na dada zake, wote hawako pamoja na sisi? Basi, alipata wapi mambo haya yote?”—Matayo 13:54-56.

Watu hao wanaona kama Yesu ni mutu wa eneo lao mwenye wanajua muzuri. Pengine wanajiuliza, ‘Tulimuona vile anakomaa, sasa namna gani anaweza kuwa Masiya?’ Kwa hiyo, hata kama wanajionea ushuhuda mwingi, kutia ndani hekima nyingi ya Yesu na miujiza yake, wanamukataa. Kwa sababu wanamujua Yesu muzuri, hata watu wa jamaa yake wanashindwa kumuamini, na hilo linamusukuma Yesu aseme hivi: “Nabii anaheshimiwa kila mahali isipokuwa katika eneo lake la nyumbani na katika nyumba yake mwenyewe.”—Matayo 13:57.

Kwa kweli, Yesu anashangaa kuona vile wanakosa imani. Kwa hiyo hafanye hata muujiza moja katika eneo hilo “isipokuwa kuweka mikono yake juu ya wagonjwa wachache na kuwaponyesha.”—Marko 6:5, 6.

  • Wakati vipofu wanamuita Yesu “Mwana wa Daudi,” wanaonyesha kuwa wanaamini jambo gani?

  • Wafarisayo wanarudilia tena shitaka gani kuhusu miujiza ya Yesu?

  • Yesu anatendewa namna gani katika Nazareti, na sababu gani?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine