-
Yesu Anaponyesha Kijana Mwanaume Mwenye Kuwa na Pepo MuchafuYesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Wakati Yesu, Petro, Yakobo, na Yohana wanashuka kutoka kwenye mulima, wanakutana na watu wengi sana. Kuko jambo lenye haliendeke. Waandishi wanazunguka wanafunzi wa Yesu, na wako wanabishana nao. Watu wanashangaa kumuona Yesu, na wanaenda mbio ili kumusalimia. Anawauliza hivi: “Munabishana nao juu ya jambo gani?”—Marko 9:16.
-
-
Yesu Anaponyesha Kijana Mwanaume Mwenye Kuwa na Pepo MuchafuYesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Inaonekana waandishi wako wanasema wanafunzi mubaya kwa sababu wameshindwa kuponyesha kijana huyo, pengine kwa kuzarau bidii yao. Kwa hiyo, kuliko kujibia baba ya kijana huyo mwenye huzuni, Yesu anaambia watu hivi: “Enyi kizazi chenye hakina imani na chenye kupotoka, nitaendelea kuwa pamoja na ninyi mupaka wakati gani? Nitawavumilia mupaka wakati gani?” Bila shaka, maneno hayo yenye nguvu yanahusu waandishi wenye walikuwa wanavuruga wanafunzi wa Yesu wakati hakukuwa pamoja nao. Yesu anageuka kwenye baba ya kijana huyo iko na kusema hivi: “Mumulete hapa.”—Matayo 17:17.
-