Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jy sura 95 uku. 222-uku. 223 fu. 9
  • Anafundisha Kuhusu Kuvunja Ndoa na Somo Kuhusu Watoto

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Anafundisha Kuhusu Kuvunja Ndoa na Somo Kuhusu Watoto
  • Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Heshimia “Kile Chenye Mungu Ameunganisha”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • “Kile Chenye Mungu Ameunganisha . . .”
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 95 uku. 222-uku. 223 fu. 9
Watu wanamuletea Yesu watoto wao

SURA YA 95

Anafundisha Kuhusu Kuvunja Ndoa Na Kupenda Watoto

MATAYO 19:1-15 MARKO 10:1-16 LUKA 18:15-17

  • YESU ANAONYESHA MAWAZO YA MUNGU KUHUSU KUVUNJA NDOA

  • ZAWADI YA KUBAKIA BILA KUOA AO KUOLEWA

  • NI JAMBO LA LAZIMA KUWA KAMA WATOTO WADOGO

Yesu na wanafunzi wake wanatoka Galilaya, na wanavuka Muto Yordani na wanakamata njia ya kusini yenye kupitia Perea. Mara ya mwisho, wakati alikuwa Perea, alitajia Wafarisayo kanuni ya Mungu kuhusu kuvunja ndoa. (Luka 16:18) Sasa, Wafarisayo wanatokeza habari hiyo ili kujaribu Yesu.

Musa aliandika kwamba mwanaume angevunja ndoa na bibi yake kwa sababu ya “jambo fulani lenye halifae” juu ya bibi huyo. (Kumbukumbu la Torati 24:1) Kuko mawazo yenye kuwa tofauti kuhusu sababu zenye zinaweza kufanya ndoa ivunjike. Watu fulani wanaamini kama makosa kidogo-kidogo yako kati ya sababu hizo. Kwa hiyo, Wafarisayo wanauliza hivi: “Je, inaruhusiwa mwanaume kuvunja ndoa na bibi yake kwa sababu yoyote?”—Matayo 19:3.

Kuliko kutumia mawazo ya watu, kwa hekima, Yesu anataja mupango huu wa Mungu kuhusu ndoa: “Je, hamukusoma kama ule mwenye aliwaumba tangu mwanzo aliwafanya mwanaume na mwanamuke na alisema: ‘Kwa sababu hiyo mwanaume atamuacha baba yake na mama yake na atashikamana na bibi yake, na hao wawili watakuwa mwili mumoja’? Na hivyo hawako wawili tena, lakini mwili mumoja. Kwa hiyo, kile chenye Mungu ameunganisha, mutu yeyote asikitenganishe.” (Matayo 19:4-6) Wakati Mungu alianzisha ndoa kati ya Adamu na Eva hakufanya mupango wa kuvunja ndoa yao.

Wafarisayo wanaanzisha ubishi na Yesu kwa kuuliza hivi: “Basi, sababu gani Musa aliagiza kupatia bibi cheti cha kumufukuza na kuvunja naye ndoa?” (Matayo 19:7) Yesu anawaambia hivi: “Musa aliwaruhusu kuvunja ndoa na bibi zenu kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, lakini haikukuwa vile tangu mwanzo.” (Matayo 19:8) “Mwanzo” huo haukuanza siku za Musa; ulianza wakati Mungu alianzisha ndoa katika Edeni.

Kisha, Yesu anawaonyesha kweli hii ya maana: “Ninawaambia ninyi kwamba kila mutu mwenye anavunja ndoa na bibi yake, kama haiko tu kwa sababu ya uasherati [Kigiriki, por·neiʹa], na kumuoa mwingine anafanya uzinifu.” (Matayo 19:9) Kwa hiyo, kulingana na Maandiko, sababu ya kuvunja ndoa ni uasherati tu.

Hilo linafanya wanafunzi waseme hivi: “Kama mambo yako vile kati ya mwanaume na bibi yake, ni muzuri mutu asioe.” (Matayo 19:10) Ni wazi kwamba, wakati mutu anafikiria kufunga ndoa anapaswa kuiona kuwa ya maisha yote!

Kuhusu kubakia bila kuoa ao kuolewa, Yesu anaeleza kwamba, watu fulani wanazaliwa wakiwa matowashi, ni kusema, wakiwa bila tamaa ya kitendo cha ndoa. Wengine wanageuzwa kuwa matowashi, kwa kulemazwa viungo vya uzazi. Lakini, wengine wanazuia tamaa yao ya kufurahia kitendo cha ndoa. Wanafanya hivyo ili waweze kufanya mengi zaidi katika kazi za Ufalme. Yesu anawatia moyo hivi wasikilizaji wake: “Kila mutu mwenye anaweza kukubali neno hilo [la kuwa bila kuoa ao kuolewa], alikubali.”—Matayo 19:12.

Sasa, watu wanaanza kumuletea Yesu watoto wadogo. Lakini wanafunzi wanafokea watu, pengine, hawapendi wamusumbue Yesu. Wakati Yesu anaona jambo hilo, anakasirika na kuwaambia hivi: “Muache watoto wadogo wakuje kwangu; musijaribu kuwazuia, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa wale wenye kuwa kama wao. Kwa kweli ninawaambia ninyi, kila mutu mwenye hapokee Ufalme wa Mungu kama mutoto mudogo hataingia hata kidogo ndani yake.”—Marko 10:14, 15; Luka 18:15.

Hilo ni somo la muzuri kabisa! Ili kupokea Ufalme wa Mungu, tunapaswa kuwa wapole na kujiacha kufundishwa, kama watoto wadogo. Sasa, Yesu anaonyesha upendo kwa watoto wadogo kwa kuwabeba katika mikono yake na kuwabariki. Na iko na upendo kama huo kwa wote wenye ‘kupokea Ufalme wa Mungu kama mutoto mudogo.’—Luka 18:17.

  • Namna gani Wafarisayo wanajaribu Yesu kuhusu mambo ya kuvunja ndoa?

  • Kulingana na Yesu, kanuni ya Mungu ni nini kuhusu kuvunja ndoa?

  • Pengine ni sababu gani inafanya wanafunzi fulani wachague kubakia bila kuoa ao kuolewa?

  • Yesu anafundisha somo gani kupitia namna yake ya kutendea watoto wadogo?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine