-
Anakomalia Katika NazaretiYesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Wakati iko pengine na miaka mbili, Yosefu na Maria wanamutosha Yesu Misri na kuenda naye Nazareti. Inaonekana kuwa wakati huo ni Yesu tu ndiye mutoto wao. Lakini kisha, ndugu-nusu za Yesu wanazaliwa pia: Yakobo, Yosefu, Simoni, na Yuda. Yosefu na Maria wanazaa pia watoto wanamuke, dada-nusu wa Yesu. Ndiyo, Yesu iko na wadogo yake sita hivi, wanaume na wanamuke.
-
-
Anakomalia Katika NazaretiYesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Yosefu anapaswa kutumika sana ili kutegemeza familia yake yenye inaongezeka. Anafanya kazi ya useremala. Yosefu anamulea Yesu kama mutoto wake mwenyewe, ndiyo sababu anaitwa “mwana wa ule seremala.” (Matayo 13:55) Yosefu anafundisha pia Yesu kazi ya useremala, na Yesu anaijua muzuri. Ndiyo sababu, watu wanafikia kusema juu ya Yesu: “Huyu ni ule seremala.”—Marko 6:3.
-