Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Alifikiri na Kuamua Katika Moyo Wake
    Tuige Imani Yao
    • 10 Maria na Yosefu wanapofika, wanakuta kijiji hicho kinajaa watu. Watu wengine walifika mbele yao ili kujiandikisha, kwa hiyo, hawapate nafasi katika chumba cha kulala cha wageni.b Basi wanalazimika kupitisha usiku mahali wanyama wanapolalishwa. Katika akili tunaweza kuona namna Yosefu anavyohangaika anapomuona bibi yake katika uchungu mukali wa kuzaa unaozidi kuongezeka. Ni mahali hapo pasipofaa kabisa ambapo Maria anaanza kusikia uchungu wa kuzaa.

      11. (a) Sababu gani wanawake duniani pote wanaweza kuelewa jinsi Maria alivyojisikia? (b) Yesu ni ‘muzaliwa wa kwanza’ katika maana gani?

      11 Wanawake duniani pote wanaweza kuelewa jinsi Maria alivyojisikia. Miaka 4 000 hivi iliyokuwa imepita, Yehova alikuwa amesema kwamba, kwa sababu ya kuriti zambi, wanawake wangezaa watoto kwa uchungu. (Mwa. 3:16) Hakuna jambo linaloonyesha kwamba Maria hakupatwa na uchungu huo. Luka hakuzungumuzia uchungu ambao Maria alisikia, lakini anaandika tu hivi: ‘Akamuzaa mwana wake, muzaliwa wa kwanza.’ (Lu. 2:7) Ndiyo, ‘muzaliwa wake wa kwanza,’ kwa sababu baadaye Maria alizaa watoto wengine 7. (Mk. 6:3) Lakini, mwana huyu atakuwa tofauti kabisa na wengine. Ni kweli kwamba alikuwa muzaliwa wa kwanza wa Maria, lakini pia ‘muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote’ vya Yehova, Mwana muzaliwa​-pekee wa Mungu!​—Kol. 1:15.

      12. Maria alimulalisha mutoto mahali gani, na hilo linatofautiana namna gani na michezo, michoro na mambo mbalimbali yanayoonyesha kuzaliwa kwa Yesu?

      12 Sasa ni hapa ndipo habari hiyo inataja jambo fulani linalojulikana sana: ‘Akamufunga vitambaa na kumulaza katika hori [ao sanduku la kulishia wanyama].’ (Lu. 2:7) Michezo, michoro na mambo mbalimbali yanayofanywa mahali pote ili kuonyesha kuzaliwa kwa Yesu yanakazia sana tukio hilo kwa kupitisha kiasi na kwa njia isiyo ya kweli. Ukweli ni huu: Yesu alilazwa katika sanduku la kulishia wanyama. Usisahau kwamba familia hiyo ilienda kupitisha usiku mahali wanyama wanalalishwa, kwa kawaida hapo ni mahali penye harufu mbaya na pasipo na hewa safi. Kwa kweli, ni muzazi gani ambaye anaweza kuchagua kumuzaa mutoto wake mahali kama hapo ikiwa ana mahali pazuri zaidi? Kwa kawaida, wazazi wanataka kuwapatia watoto wao kilicho kizuri zaidi, sivyo? Bila shaka, Maria na Yosefu wangetaka pia Mwana wa Mungu azaliwe mahali pazuri zaidi!

      13. (a) Namna gani Maria na Yosefu wanafanya yale yanayolingana na uwezo wao? (b) Namna gani leo wazazi wenye hekima wanaweza kuiga mufano wa Yosefu na Maria?

      13 Hata hivyo, hawaruhusu hali hiyo mbaya iwakoseshe furaha; wanafanya tu yale yanayolingana na uwezo wao. Kwa mufano, ona kwamba Maria yeye mwenyewe anahangaikia kitoto chake, anakifunga nguo za kitoto ili kiwe na joto, kisha anakilalisha kwa uangalifu katika sanduku ili kilale vizuri, na anahakikisha kwamba kiko salama. Maria haruhusu hali hiyo imuvunje moyo na kumukengeusha kiasi cha kutofanya kile anaweza kufanya juu ya kitoto chake. Kwa upande mwengine, wao wawili wanajua kwamba jambo nzuri zaidi ambalo wanaweza kufanya juu ya mutoto huyo ni kumusaidia akomae vizuri kiroho. (Soma Kumbukumbu la Torati 6:6-8.) Leo, wazazi wenye hekima wanatia mambo ya kiroho pa nafasi ya kwanza wanapowalea watoto wao katika dunia hii isiyoona faida za kumutumikia Mungu.

  • Alifikiri na Kuamua Katika Moyo Wake
    Tuige Imani Yao
    • b Siku hizo ilikuwa kawaida katika muji kutayarisha chumba kimoja cha kulala kwa ajili ya watu wanaosafiri pamoja.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine