-
Mutoto Mwenye AliahidiwaYesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Kumepita zaidi ya mwezi moja, na Yesu iko sasa na siku 40 tangu kuzaliwa kwake. Sasa, wazazi wake wanamupeleka wapi? Wanamupeleka kwenye hekalu katika Yerusalemu, kwenye kilometre kidogo na mahali kwenye wanaishi. Sheria inasema kama siku 40 kisha kuzala mutoto mwanaume, mama aliombwa kutoa toleo la utakaso kwenye hekalu.—Mambo ya Walawi 12:4-8.
Maria anafanya hivyo. Toleo lake, ni ndege wawili wadogo. Hilo linatusaidia kuelewa hali ya maisha yenye Yosefu na Maria walikuwa nayo. Kulingana na Sheria, iliomba kutoa mwana-kondoo dume na ndege. Lakini kama mama hana uwezo wa kupata kondoo dume, angetoa njiwa (pigeon) ao njiwa-tetere (tourterelle) mbili. Maria alijikuta katika hali hiyo na alitoa kulingana na hali yake.
-