Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Mutoto Mwenye Aliahidiwa
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
    • Kumepita zaidi ya mwezi moja, na Yesu iko sasa na siku 40 tangu kuzaliwa kwake. Sasa, wazazi wake wanamupeleka wapi? Wanamupeleka kwenye hekalu katika Yerusalemu, kwenye kilometre kidogo na mahali kwenye wanaishi. Sheria inasema kama siku 40 kisha kuzala mutoto mwanaume, mama aliombwa kutoa toleo la utakaso kwenye hekalu.—Mambo ya Walawi 12:4-8.

      Maria anafanya hivyo. Toleo lake, ni ndege wawili wadogo. Hilo linatusaidia kuelewa hali ya maisha yenye Yosefu na Maria walikuwa nayo. Kulingana na Sheria, iliomba kutoa mwana-kondoo dume na ndege. Lakini kama mama hana uwezo wa kupata kondoo dume, angetoa njiwa (pigeon) ao njiwa-tetere (tourterelle) mbili. Maria alijikuta katika hali hiyo na alitoa kulingana na hali yake.

      “WAKATI MUDA ULIFIKA WA KUWATAKASA”

      Yosefu na Maria wanapeleka mutoto Yesu kwenye hekalu ili kutoa zabihu ya utakaso

      Wakati wanamuke wa Israeli walikuwa wanazaa, walionwa kuwa hawako safi kwa wakati fulani kulingana na desturi. Mwisho wa wakati huo, toleo la kuteketezwa lilipaswa kutolewa kama zabihu ya utakaso. Hilo liliwakumbusha wote kwamba wanamupatia mutoto uzima wenye haukamilike na wenye zambi. Mutoto Yesu alikuwa mukamilifu na mutakatifu. (Luka 1:35) Lakini Maria na Yosefu ‘walimupeleka’ kwenye hekalu ‘ili kujitakasa’ kulingana na Sheria.—Luka 2:22.

  • Mutoto Mwenye Aliahidiwa
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine