Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • bt sura 9 uku. 69-76
  • “Mungu Hana Ubaguzi”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Mungu Hana Ubaguzi”
  • “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Anasali kwa “Kumulilia Mungu Sikuzote” (Mdo. 10:1-8)
  • “Petro Alikuwa . . . Anashangaa” (Mdo. 10:9-23a)
  • Petro “Akawaamuru Wabatizwe” (Mdo. 10:23b-48)
  • “Wakaacha Kupinga, na Wakamutukuza Mungu” (Mdo. 11:1-18)
  • “Wengi Wakakuwa Waamini” (Mdo. 11:19-26a)
  • Kutuma “Misaada” (Mdo. 11:26b-30)
  • Kornelio Anapokea Roho Takatifu
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • “Kisha . . . Kukosa Kupatana”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Yehova “Hana Ubaguzi”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kama Petro Usichoke, Endelea
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
“Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
bt sura 9 uku. 69-76

SURA YA 9

“Mungu Hana Ubaguzi”

Wakristo wanaanza kuhubiria Watu wa Mataifa wenye hawatahiriwe

Inategemea Matendo 10:1–11:30

1-3. Petro anapewa maono gani, na juu ya nini ni jambo ya maana tuelewe maana ya ile maono?

TUKO mu mwaka wa 36 K.K.Y. Petro iko nasali ku sehemu ya juu ya nyumba yenye kuwa pembeni ya bahari mu muji wa Yopa. Amekuwa mugeni mu ile nyumba kwa siku fulani. Juu alikuwa tayari kubakia mu ile nyumba, ile inaonyesha kama kwa kiasi fulani hakukuwa na ubaguzi. Mwenye ile nyumba ni Simoni mutengenezaji wa ngozi, na haiko kila Muyahudi njo angekubali kubakia na mutu mwenye anafanyaka ile kazi.a Petro alikuwa karibu kujifunza hii somo ya maana: Yehova hana ubaguzi.

2 Wakati Petro alikuwa anasali akaanza kuona maono. Mambo yenye aliona inaweza kusumbua kila Muyahudi. Aliona kitu fulani yenye kuwa sawa vile chombo yenye kutengenezwa na kitambaa iko nashuka kutoka mbinguni, na ndani yake mulikuwa wanyama wenye hawakukuwa safi kulingana na Sheria. Wakati aliambiwa achinje na akule nyama yao Petro alijibia hivi: “Hapana Bwana, kwa sababu sijakula hata siku moja kitu kichafu na chenye hakiko safi.” Anaambiwa hivi mara tatu: “Acha kuita vitu vyenye Mungu ametakasa kuwa ni vichafu.” (Mdo. 10:14-16) Ile maono inafanya Petro avurugike, lakini karibuni ataelewa maana ya ile maono.

3 Maono yenye Petro aliona ilikuwa na maana gani? Ni jambo ya maana sana kujua maana ya ile maono juu itatusaidia kuelewa kweli ya maana sana kuhusu namna Yehova anaonaka watu. Juu tuko Wakristo wa kweli, hatuwezi kabisa kutoa ushahidi kwa ukamili kuhusu Ufalme wa Mungu kama hatujikaze kuona watu vile Mungu anawaona. Ili tuelewe maana ya maono yenye Petro aliona tuchunguze mambo yenye ilitokea mbele apewe ile maono.

Anasali kwa “Kumulilia Mungu Sikuzote” (Mdo. 10:1-8)

4, 5. Kornelio alikuwa nani, na nini ilitokea wakati alikuwa anasali?

4 Petro hakujua kama siku yenye ilitangulia katika Kaisaria, yenye ilikuwa ku kilometre 50 hivi kaskazini, mwanaume mwenye kuitwa Kornelio alikuwa pia amepata maono kutoka kwa Mungu. Kornelio, ofisa katika jeshi la Roma, “alikuwa muabudu wa Mungu.”b Alikuwa pia anahangaikia familia yake muzuri juu alikuwa “anamuogopa Mungu, yeye pamoja na watu wote wa nyumba yake.” Kornelio hakukuwa Muyahudi mugeuzwa-imani, lakini alikuwa mutu wa mataifa mwenye hatahiriwe. Hata vile alionea huruma Wayahudi wenye walikuwa mu uhitaji na aliwapatia vitu vyenye walikuwa navyo lazima. Ule mwanaume mwenye moyo muzuri “alikuwa anasali kwa kumulilia Mungu sikuzote.”​—Mdo. 10:2.

5 Saa kenda hivi ya muchana (15h00), Kornelio alikuwa anasali wakati aliona maono, na mu ile maono malaika alimuambia hivi: “Sala zako na zawadi zako za rehema zimepanda kwa Mungu na anaendelea kuzikumbuka.” (Mdo. 10:4) Sawa vile malaika amemuamuru, Kornelio anatuma wanaume waende kumuita mutume Petro. Kornelio mutu wa mataifa mwenye hatahiriwe, alikuwa karibu kufunguliwa mulango wenye kufikia sasa ulikuwa umefungwa, ni kusema alikuwa karibu kusikia ujumbe wa wokovu.

6, 7. (a) Toa mufano wenye unaonyesha kama Yehova anajibiaka sala za watu wenye mioyo mizuri wenye wako natafuta kweli kumuhusu. (b) Ile mifano ya vile inaonyesha nini?

6 Je, leo Mungu anasikilizaka sala za watu wenye mioyo mizuri wenye wako natafuta kujua ukweli kumuhusu? Tuone mufano fulani. Mwanamuke fulani mu inchi ya Albania alikubali Munara wa Mulinzi wenye ulikuwa na habari fulani yenye kuzungumuzia namna ya kukomalisha watoto.c Aliambia hivi Shahidi mwenye alimutembelea: “Unaweza kuamini kama nilikuwa nasali Mungu anisaidie kukomalisha watoto wangu wanamuke? Amekutuma! Umenipatia jambo yenye nilikuwa nayo lazima kabisa!” Ule mwanamuke na watoto wake walianza kujifunza Biblia kisha bwana yake naye akaanza kujifunza Biblia.

7 Ni ile mufano moya tu? Hapana, mambo ya vile inatokeaka mara kwa mara mu dunia yote. Njo maana hatuwezi kusema kama ni mambo yenye inajitokezaka tu hivihivi! Sasa ile inaonyesha nini? Kwanza, Yehova anajibiaka sala za watu wenye mioyo mizuri wenye wako namutafuta. (1 Fa. 8:41-43; Zb. 65:2) Pili, malaika wanatuongozaka mu kazi ya kuhubiri.​—Ufu. 14:6, 7.

“Petro Alikuwa . . . Anashangaa” (Mdo. 10:9-23a)

8, 9. Mungu alifunulia Petro nini kupitia roho yake takatifu, na Petro alitenda namna gani?

8 Petro alikuwa angali ku sehemu ya juu ya nyumba na “alikuwa . . . anashagaa” juu ya maana ya ile maono, wakati wanaume wenye Kornelio alituma walikaribia nyumba kwenye alikuwa. (Mdo. 10:17) Petro, mwenye alikatala mara tatu kula vyakula vyenye vilionwa kuwa haviko safi kulingana na Sheria, angekubali kuenda na wale wanaume na kuingia mu nyumba ya Mutu wa Mataifa? Kwa njia fulani, kupitia roho yake takatifu, Mungu alimufunulia mapenzi yake kuhusu ile jambo. Petro aliambiwa: “Angalia! Wanaume watatu (3) wanakutafuta. Basi simama, ushuke na uende pamoja nao, usikuwe na mashaka hata kidogo, kwa sababu nimewatuma.” (Mdo. 10:19, 20) Maono yenye Petro aliona ya kitu fulani yenye kuwa sawa chombo yenye kutengenezwa na kitambaa, bila shaka ilimutayarisha.

9 Wakati alijua kama Mungu njo alikuwa ameamuru Kornelio atume watu wamuite, Petro alikaribisha wale Watu wa Mataifa mu nyumba “na kukaa nao wakiwa wageni wake.” (Mdo. 10:23a) Ule mutume mutiifu alikuwa tayari ameanza kubadilisha mawazo yake na kuipatanisha na mapenzi ya Mungu.

10. Yehova anaongoza watu wake namna gani na tunaweza kujiuliza maulizo gani?

10 Leo pia, Yehova anaongoza watu wake hatua kwa hatua. (Mez. 4:18) Kupitia roho yake takatifu, iko naongoza “mutumwa muaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:45) Wakati fulani, tunaweza kupata mafasirio mapya juu ya namna yetu ya kuelewa Neno ya Mungu, ao mabadiliko juu ya namna mambo inapangwa mu tengenezo. Ni muzuri tujiulize hivi: ‘Ninatenda namna gani wakati kunakuwa mafasirio mapya ao mabadiliko fulani? Niko tayari kutii muongozo wa roho takatifu ya Mungu mu ile mambo?’

Petro “Akawaamuru Wabatizwe” (Mdo. 10:23b-48)

11, 12. Petro alifanya nini wakati alifika Kaisaria, na alijifunza nini?

11 Kisha Petro kupata ile maono, siku yenye ilifuata, yeye na watu wengine kenda, ni kusema wanaume tatu wenye Kornelio alituma na “ndugu sita (6) [Wayahudi]” kutoka Yopa wakaeda Kaisaria. (Mdo. 11:12) Wakati Kornelio alikuwa anamuchunga Petro, alikusanya “watu wa jamaa yake na marafiki wake wa karibu;” inaonekana wote walikuwa Watu wa Mataifa. (Mdo. 10:24) Wakati Petro alifika, alifanya jambo yenye hakuwaziaka hata siku moya kama atafanya: Aliingia mu nyumba ya Mutu wa Mataifa mwenye hatahiriwe! Petro alisema hivi: “Munajua muzuri kwamba Muyahudi haruhusiwe kushirikiana ao kukaribia mutu wa jamii ingine, lakini Mungu amenionyesha kwamba sipaswe kuita mutu yeyote kuwa muchafu ao haiko safi.” (Mdo. 10:28) Kufikia sasa Petro ameelewa kama maono yenye ameona ilikuwa na kusudi ya kumufundisha somo fulani ya maana, haikukuwa tu nahusu chakula. Hakupaswa “kuita mutu yeyote [hata Mutu wa Mataifa] kuwa muchafu.”

Petro na wenzake wanaingia mu nyumba ya Kornelio.

“Kornelio alikuwa anawangojea na alikuwa amekusanya watu wa jamaa yake na marafiki wake wa karibu.”​—Matendo 10:24

12 Watu wote wenye walikuwa pale walikuwa na hamu ya kusikia mambo yenye Petro atasema. Kisha Kornelio akasema hivi: “Sisi wote tuko mbele ya Mungu ili kusikia mambo yote yenye Yehova amekuamuru useme.” (Mdo. 10:33) Wazia namna unaweza kujisikia kama mutu mwenye kupendezwa anasema maneno ya vile! Petro anaanza na hii maneno yenye kugusa moyo sana: “Sasa ninaelewa kabisa kwamba Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa mutu mwenye anamuogopa na kufanya mambo yenye kuwa sawa anakubaliwa naye.” (Mdo. 10:34, 35) Petro alikuwa ameelewa kama haiko rangi ya ngozi, inchi ao jambo ingine yenye inaonekana kwa inje njo inaweza kufanya Mungu akubali mutu ao hapana. Kisha Petro akaanza kutoa ushahidi kuhusu utumishi wa Yesu, kifo yake, na ufufuo wake.

13, 14. (a) Kuingia kwa Watu wa Mataifa mu kutaniko ya Kikristo mu 36 K.K.Y. kungekuwa na matokeo gani? (b) Juu ya nini hatupaswe kuhukumu watu kulingana na namna wanaonekana kwa inje?

13 Sasa kunatokea jambo yenye ilikuwa haiyatokeaka: “Wakati Petro alikuwa angali anasema,” roho takatifu ilimwangwa juu ya wale “watu wa mataifa.” (Mdo. 10:44, 45) Ni hii mara tu njo Biblia inazungumuzia watu wenye walipokea roho takatifu mbele ya kubatizwa. Juu Petro alitambua kama ile ni alama ya kukubaliwa na Mungu ‘aliawaamuru [wale Watu wa Mataifa] wabatizwe.’ (Mdo. 10:48) Wakati Watu wa Mataifa waliingia mu kutaniko ya Kikristo mu mwaka wa 36 K.K.Y., Yehova hakutendea tena Wayahudi kwa njia ya pekee. (Da. 9:24-27) Juu Petro njo alitolea ushahidi Watu wa Mataifa, alitumia ‘funguo ya Ufalme’ ya tatu, ni kusema funguo ya mwisho. (Mt. 16:19) Ile funguo ilitolea Watu wa Mataifa wenye hawatahiriwe nafasi ya kuwa Wakristo watiwa-mafuta.

14 Leo, siye wahubiri wa Ufalme tunajua pia kama “hakuna ubaguzi kwa Mungu.” (Ro. 2:11) Mapenzi yake ni kwamba “watu wa namna zote waokolewe.” (1 Ti. 2:4) Kwa hiyo hatupaswe kuhukumu watu kulingana na vile wanaonekana kwa inje. Kazi yetu ni kutoa ushahidi kamili kuhusu Ufalme wa Mungu, ni kusema tunapaswa kuhubiria watu wote bila kuangalia rangi yao ya ngozi, inchi yao, namna wanaonekana kwa inje, ao dini yao.

“Wakaacha Kupinga, na Wakamutukuza Mungu” (Mdo. 11:1-18)

15, 16. Juu ya nini Wakristo fulani Wayahudi walibishana na Petro, na alijieleza namna gani?

15 Bila shaka Petro alikuwa na hamu sana ya kuenda Yerusalemu na kueleza mambo yote yenye ilitokea. Alipenda kueleza namna Watu wa Mataifa wenye hawatahiriwe walikuwa “wamekubali neno la Mungu.” Lakini inaonekana kama ile habari ilikuwa ilishamutangulia. Kisha tu Petro kufika, “wale wenye waliunga mukono kutahiriwa wakaanza kubishana naye.” Walikwazika kwa sababu alikuwa ameingia mu ‘nyumba ya watu wenye hawatahiriwe na kula pamoja nao.’ (Mdo. 11:1-3) Shida haikukuwa Watu wa Mataifa kuwa wanafunzi wa Kristo. Wale wanafunzi Wayahudi walikuwa njo nakazia kama Watu wa Mataifa walipaswa kufuata Sheria ya Musa kutia ndani kutahiriwa ili Yehova akubali ibada yao. Ni wazi kwamba, ilikuwa nguvu kwa wanafunzi fulani Wayahudi kuachana na Sheria ya Musa.

16 Petro alijieleza namna gani? Kulingana na Matendo 11:4-16, alifasiria mambo ine yenye ilionyesha waziwazi kama alikuwa anafuata muongozo wa Mungu: (1) maono yenye Mungu alimupatia (Mustari wa 4-10); (2) maagizo yenye roho takatifu ilimupatia (Mustari wa 11, 12); (3) namna malaika alimutembelea Kornelio (Mustari wa 13, 14); na (4) namna Watu wa Mataifa walipokea roho takatifu (Mustari wa 15, 16). Kisha Petro alimalizia na ulizo yenye iliwachochea wafikiri sana. Aliwauliza hivi: “Kwa hiyo, kama Mungu alipatia hao [Watu wa Mataifa wenye waliamini] zawadi ileile ya bure [ya roho takatifu] kama vile alitupatia sisi [Wayahudi] wenye tumemuamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani ili niweze hata kumuzuia Mungu?”​—Mdo. 11:17.

17, 18. (a) Kisha kusikiliza ushuhuda wa Petro, wale Wakristo Wayahudi walipaswa kufanya nini? (b) Juu ya nini inaweza kuwa nguvu kulinda umoja wa kutaniko, na ni muzuri tujiulize maulizo gani?

17 Kisha kusikiliza ushuhuda wa Petro wale Wakristo Wayahudi walipaswa kuamua. Wangeachana kabisa na ubaguzi na kukubali wale Watu wa Mataifa wenye walitoka kubatizwa kuwa Wakristo wenzao? Biblia inasema hivi: “Wakati walisikia mambo hayo, [ni kusema, mitume na Wakristo wengine Wayahudi] wakaacha kupinga, na wakamutukuza Mungu, na kusema: ‘Kwa hiyo basi, Mungu amepatia watu wa mataifa pia musamaha wenye unaongoza kwenye uzima.’” (Mdo. 11:18) Ile namna yao ya kutenda ililinda umoja wa kutaniko.

18 Leo kulinda umoja inaweza kuwa nguvu juu Wakristo wa kweli wanatoka mu “mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na luga.” (Ufu. 7:9) Kwa hiyo mu makutaniko mingi muko watu wa rangi tofauti ya ngozi, wa desturi mbalimbali, na wenye walikomala mu njia mbalimbali. Kwa hiyo, ni muzuri tujiulize hivi: ‘Nimetosha kabisa ubaguzi wa namna yoyote mu moyo wangu? Nimeazimia kutoruhusu mambo yenye kugawanya watu mu dunia, sawa vile mutu kupenda sana inchi yake, kabila yake, desturi yake ao rangi yake ya ngozi ichochee namna yangu ya kutendea ndugu na dada zangu Wakristo?’ Kumbuka mambo yenye ilimufikia Petro (Kefa) miaka fulani kisha Watu wa Mataifa wa kwanza-kwanza kuwa Wakristo. Juu alichochewa na ubaguzi wa wengine, alianza ‘kujitenga’ na Wakristo wa mataifa na Paulo alimukaripia juu ya ile. (Gal. 2:11-14) Tunapaswa kuendelea kuwa waangalifu juu tusiangukie mu mutego wa kubagua watu.

“Wengi Wakakuwa Waamini” (Mdo. 11:19-26a)

19. Wakristo Wayahudi wenye walikuwa Antiokia walianza kuhubiria nani, na matokeo ilikuwa nini?

19 Wanafunzi wa Yesu walianza sasa kuhubiria Watu wa Mataifa wenye hawatahiriwe? Fikiria mambo yenye ilitokea katika Antiokia ya Siria.d Wayahudi wengi waliishi mu ile muji, lakini hakukukuwa uadui kati ya Wayahudi na Watu wa Mataifa. Kwa hiyo Antiokia ilikuwa fasi ya muzuri sana ya kuhubiria Watu wa Mataifa. Ni mu ile muji njo wanafunzi Wayahudi walianza kutangazia habari njema “watu wenye kusema Kigiriki.” (Mdo. 11:20) Hawakuhubiria tu Wayahudi wenye kusema kigiriki lakini pia Watu wa Mataifa wenye hawatahiriwe. Yehova alibariki ile kazi ya kuhubiri na “wengi wakakuwa waamini.”​—Mdo. 11:21.

ANTIOKIA YA SIRIA

Antiokia ya Siria ilikuwa mu eneo ya muto Orontes, ku kilometre 30 hivi kutoka ku bandari ya Seleukia yenye kuwa pembeni ya Bahari ya Mediterania na ilikuwa ku kilometre 550 hivi kaskazini mwa Yerusalemu. (Mdo. 13:4) Niketa Seleuko wa Kwanza, mutawala wa kwanza wa Utawala wa Seleukia alianzisha Antiokia mu mwaka wa 300 M.K.Y. Juu Antiokia ilikuwa muji mukubwa wa ule utawala, bila kukawia ulifikia kuwa muji wa maana sana. Mu 64 M.K.Y., jenerali Muroma Pompey alifanya Siria kuwa jimbo la Roma, na Antiokia ikakuwa muji mukubwa wa ile jimbo. Kufikia karne ya kwanza kisha kuzaliwa kwa Yesu, ule muji wenye kuendelea sana ulifikia kuwa muji wa tatu wenye kuwa mukubwa na tajiri kati ya miji ya Utawala wa Roma; ilikuwa ya tatu kisha Roma na Aleksandria.

Antiokia ilikuwa muji wa kibiashara na wa politike. Biashara kutoka Siria yote ilipitia Antiokia mbele ya kupelekwa mu maeneo ingine yenye kuzunguka Bahari ya Mediterania. Mutu moya mwenye elimu anasema hivi: “Juu ilikuwa katikati ya mipaka ya eneo ya Wagiriki na Waroma na majimbo ya mashariki, ilikuwa na watu wa kutoka fasi mbalimbali kuliko miji mingi ya Wagiriki.” Mu muji wa Antiokia mulikuwa Wayahudi wengi na kulingana na mwanahistoria Muyahudi Flavius Josèph, wale “Wayahudi walifanya Wagirikiri wengi” wenye kuishi pale “kuwa wageuzwa-imani.”

20, 21. Namna gani Barnaba alionyesha kama alikuwa mwenye kiasi, na namna gani siye pia tunaweza kuonyesha sifa ya kiasi mu mahubiri?

20 Ili kushugulikia ile shamba yenye ilikuwa tayari kuvunwa, kutaniko katika Yerusalemu ilituma Barnaba katika Antiokia. Juu watu wengi sana walikuwa nakubali habari njema, Barnaba hangeweza kushugulikia wale watu yeye peke. Sauli mwenye angefikia kuwa mutume kwa mataifa njo alifaa kabisa kumusaidia. (Mdo. 9:15; Ro. 1:5) Barnaba aliwaza kama ikiwa anaomba Sauli amusaidie, ni kusema Sauli atakuwa wa maana kumupita? Hapana. Barnaba alikuwa mwenye kiasi. Yeye mwenyewe aliamua kuenda Tarso kumutafuta Sauli na kumuleta ili asaidie. Wote wawili walifanya mwaka moya na wako natia wanafunzi moyo katika kutaniko kule Antiokia.​—Mdo. 11:22-26a.

21 Namna gani tunaweza kuwa na kiasi wakati tuko tunafanya kazi yetu ya kuhubiri? Tunapaswa kujua mipaka yetu. Siye wote tuko na uwezo mbalimbali. Kwa mufano, wamoja wanaweza kuwa na ufundi wa kuhubiria watu wakati wowote ao nyumba kwa nyumba, lakini wako na magumu ya kurudilia watu na kuanzisha mafunzo ya Biblia. Kama ungependa kukomalisha ufundi wako mu sehemu fulani ya mahubiri, juu ya nini usiombe musaada? Kama unafanya vile, utakuwa muhubiri muzuri zaidi na utapata furaha mu kazi ya kuhubiri.​—1 Ko. 9:26.

Kutuma “Misaada” (Mdo. 11:26b-30)

22, 23. Ndugu katika Antiokia walionyesha namna gani kama wanapenda ndugu zao, na watu wa Mungu wanafanya vile namna gani leo?

22 Katika Antiokia njo kwa mara ya kwanza “wanafunzi waliitwa Wakristo kupitia muongozo wa Mungu.” (Mdo. 11:26b) Ile jina yenye ilikubaliwa na Mungu njo ilistahili kabisa kuita wale wenye walifuata mufano wa Kristo. Wakati Watu wa Mataifa waliendelea kuwa Wakristo, je, Wayahudi na Watu wa Mataifa walifikia kuishi kama vile ndugu? Ona mambo yenye ilifanyika mu mwaka wa 46 K.K.Y.e wakati njaa kubwa ilitokea. Zamani wakati njaa kubwa ilitokea, maskini njo waliteseka sana juu hawakukuwa na chakula ao makuta pembeni. Wakati ile njaa ilitokea Wakristo Wayahudi wenye kuishi Yudea walikuwa na lazima ya chakula juu inaonekana wengi wao walikuwa maskini. Wakati ndugu wa Antiokia walipata ile habari, kutia ndani Watu wa Mataifa wenye walikuwa Wakristo, walituma “misaada kwa ndugu wenye kuishi Yudea.” (Mdo. 11:29) Bila shaka walionyesha ndugu zao upendo wa kweli!

23 Leo pia watu wa Mungu wako nafanya vile. Wakati tunapata habari kuwa ndugu zetu mu inchi ingine ao mu eneo yetu wako na lazima ya musaada, tunakuwaka tayari kuwasaidia. Bila kukawia Halmashauri za Tawi zinakamataka mipango juu ya kuweka Halmashauri za Kutoa Misaada juu zishugulikie ndugu wenye wanapatwa na misiba ya asili sawa vile upepo mukali, matetemeko ya inchi, na tsunami. Ile kazi ya kutoa misaada inaonyesha kama tunapenda kabisa ndugu zetu.​—Yoh. 13:34, 35; 1 Yo. 3:17.

24. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunakamata kwa uzito maana ya maono yenye Petro aliona?

24 Juu tuko Wakristo wa kweli, tunakamata kwa uzito maono yenye Petro aliona wakati alikuwa ku sehemu ya juu ya nyumba kule Yopa. Tunaabudu Mungu mwenye hana ubaguzi. Mapenzi yake ni tutoe ushahidi kwa ukamili kuhusu Ufalme wake. Ile inatia ndani kuhubiria wengine bila kuangalia rangi yao ya ngozi, inchi yao, ao hali yao ya maisha. Kwa hiyo, tuazimie basi kupatia watu wote wenye wako tayari kusikiliza nafasi ya kukubali habari njema.​—Ro. 10:11-13.

Ndugu na dada wako natengeneza sehemu ya juu ya nyumba.

Wakati ndugu zetu wako na lazima ya musaada, tunakuwaka tayari kuwasaidia

KORNELIO NA JESHI YA ROMA

Makao makubwa ya serikali na ya jeshi kwa ajili ya jimbo la Waroma la Yudea ilikuwa Kaisaria. Chini ya uongozi wa gavana, kulikuwa wapanda-farasi kati ya 500 na 1000 na vikundi tano vya maaskari wa kutembea kwa miguu. Mu kila kikundi ya maaskari wa kutembea kwa miguu mulikuwa maaskari 600 hivi. Kwa kawaida wale maaskari walichaguliwa kati ya watu wenye waliishi mu maeneo yenye kutawaliwa na Roma lakini hapana kati ya raia wa Roma. Wengi wao walitumikia Kaisaria, lakini vikundi vidogo-vidogo vilitawanywa katika Yudea yote. Kikundi moya ya maaskari ilikuwa inabakia kwenye Munara wa Antonia katika Yerusalemu ili kulinda Mulima wa Hekalu na muji. Wakati wa sikukuu za Wayahudi maaskari walikuwa wanaongezwa mu ile muji juu washugulikie mambo ikiwa kunatokea muvurugo.

Ofisa wa jeshi alikuwa anasimamia maaskari karibu 100. Maandiko ya Kigiriki mu Matendo 10:1 inasema kama Kornelio alikuwa ofisa wa jeshi katika kikundi chenye kiliitwa Kikundi cha Maaskari wa Italia, na kilikuwa Kaisaria. Pengine ile ilikuwa kikundi ya pili ya maaskari wa Italia wenye walikuwa raia wa Roma wenye kujitolea.f Maofisa walikuwa na mamlaka makubwa juu ya watu na jeshi, na walikuwa na mali. Inawezekana feza yenye walikuwa wanalipwa ilikuwa mara 16 feza yenye askari wa kawaida alikuwa analipwa.

f Mu Kilatini, Cohors II Italica voluntariorum civium Romanorum. Kuko ushuhuda wenye kuonyesha kama ile kikundi ilikuwa Siria mu mwaka wa 69 K.K.Y.

a Wayahudi fulani walizarau watengenezaji wa ngozi juu ile kazi ilifanya waguse ngozi na maiti za wanyama, na pia vitu vingine vyenye kuchukiza vyenye walikuwa navyo lazima ili kufanya ile kazi. Watengenezaji wa ngozi walionwa kuwa hawastahili kufika ku hekalu. Nafasi yao ya kutumikia ilipaswa kuwa ku umbali wa metre 22 hivi kutoka mu muji. Ile inaweza kuwa sababu yenye ilifanya nyumba ya Simoni ikuwe “pembeni ya bahari.”​—Mdo. 10:6.

b Ona kisanduku “Kornelio na Jeshi ya Roma.”

c Habari yenye kichwa “Mashauri Yenye Kutegemeka Kuhusu Kulea Watoto,” ilitolewa mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 11, 2006, ukurasa wa 4-7.

d Ona kisanduku “Antiokia ya Siria.”

e Mwanahistoria Muyahudi Josèph anasema kama ile “njaa kubwa” ilitokea wakati wa utawala wa Klaudio (41-54 K.K.Y.).

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine