Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ‘Kusema Bila Woga kwa Mamlaka ya Yehova’
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
    • 8. Juu ya nini Paulo na Barnaba waliondoka Ikoniamu, na mufano wao unatufundisha nini?

      8 Kisha wakati fulani, wapinzani wa Ikoniamu wakakamata mupango wa kupiga Paulo na Barnaba majiwe. Wakati wale wamisionere wawili walipata ile habari, wakaamua kuenda kuhubiri mu eneo ingine. (Mdo. 14:5-7) Leo, wahubiri wa habari njema wanatumia pia busara ya vile. Wakati watu wanatupinga kwa maneno, tunasema bila woga. (Flp. 1:7; 1 Pe. 3:13-15) Lakini wakati wanataka kututendea mubaya, tunaepuka kufanya jambo yoyote yenye inaweza kutia maisha yetu ao maisha ya ndugu zetu mu hatari.​—Mez. 22:3.

  • ‘Kusema Bila Woga kwa Mamlaka ya Yehova’
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
    • Ikoniamu ilikuwa ku mupaka wa maeneo ya Galatia, ni kusema eneo ya Likaonia na Frigia. Waandikaji fulani wa zamani kutia ndani Sisero na Strabo, waliita Ikoniamu muji wa Likaonia, na kulingana na karte, ni kweli ule muji ulikuwa mu ile eneo. Lakini kitabu ya Matendo inatofautisha Ikoniamu na Likaonia, kwenye “luga ya Kilikaonia” ilizungumuzwa. (Mdo. 14:1-6, 11) Njo maana watu fulani wanasema kama kitabu ya Matendo iko na makosa. Lakini, mu 1910 watu wenye kuvumbula vitu vya zamani walipata maandishi yenye ilionyesha kama luga ya Kifrigia njo luga yenye ilitumiwa Ikoniamu miaka mia mbili kisha Paulo na Barnaba kutembelea ile eneo. Kwa hiyo, mwenye aliandika kitabu ya Matendo hakukosea kwa kutofautisha Ikoniamu na miji ya Likaonia.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine