Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • bt sura 15 uku. 117-123
  • ‘Kutia Makutaniko Nguvu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • ‘Kutia Makutaniko Nguvu
  • “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Turudie Sasa na Tutembelee Ndugu” (Mdo. 15:36)
  • “Mulipuko Mukali wa Kasirani” (Mdo. 15:37-41)
  • “Walikuwa Wanatoa Ushahidi Muzuri Juu Yake” (Mdo. 16:1-3)
  • “Kuwa Nguvu Katika Imani” (Mdo. 16:4, 5)
  • ‘Mutoto Wangu Mupendwa na Muaminifu Katika Bwana’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • ‘Kusema Bila Woga kwa Mamlaka ya Yehova’
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Ndugu Vijana​—⁠Muige Marko na Timoteo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • “Kujaa na Furaha na Roho Takatifu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
Ona Habari Zaidi
“Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
bt sura 15 uku. 117-123

SURA YA 15

‘Kutia Makutaniko Nguvu’

Watumishi wenye kusafiri wanasaidia makutaniko ikuwe na imani yenye nguvu

Inategemea Matendo 15:36–16:5

1-3. (a) Nani njo ameanza kusafiri pamoya na Paulo, na ni mutu wa namna gani? (b) Tutajifunza nini mu hii sura?

WAKATI wako nasafiri muji kisha muji, Paulo anaangalia kijana mwenye iko anatembea pembeni yake, kijana Timoteo. Ni kijana mwenye nguvu. Na inawezekana iko na miaka karibu 20. Wakati wako wanaendelea na safari, ni vile ule kijana iko anakuwa mbali zaidi na kwao. Kadiri masiku iko inapita, muji wa Listra na Ikoniamu inabakia mbali sana. Ni mambo gani itatokea mu safari yao? Paulo anajua mambo yenye inaweza kutokea, kwa sababu ni safari yake ya pili ya umisionere. Anajua kama kutakuwa hatari na magumu mingi. Ule kijana atatenda namna gani?

2 Paulo anamutumainia Timoteo, pengine kupita vile Timoteo anajitumainia mwenyewe. Mambo yenye ilipita mu masiku yenye ilitangulia, ilimuhakikishia Paulo kama iko na lazima ya mutu mwenye anastahili kabisa wa kusafiri naye. Paulo anajua kama kazi yenye watafanya, ni kusema kutembelea makutaniko na kuitia nguvu, itaomba wajitoe sana na wakuwe na umoja kati yao. Pengine juu ya nini Paulo anawaza vile? Inawezekana ni juu ya hali ya kukosa kuelewana yenye ilitokea mbele ya pale kati yake na Barnaba, yenye ilifanya waachane.

3 Mu hii sura, tutajifunza njia ya muzuri ya kumaliza hali ya kukosa kuelewana. Tutaona pia juu ya nini Paulo alimuchagua Timoteo ili asafiri pamoya naye, na tutaelewa muzuri kazi ya maana yenye waangalizi wa muzunguko wanafanya leo.

“Turudie Sasa na Tutembelee Ndugu” (Mdo. 15:36)

4. Paulo alikuwa na kusudi ya kufanya nini mu safari yake ya pili ya umisionere?

4 Mu sura yenye ilitangulia, tuliona vile ile kikundi ya watu ine, ni kusema, Paulo, Barnaba, Yuda, na Sila, walitia moyo kutaniko yenye ilikuwa Antiokia kwa kuwaambia uamuzi wa baraza yenye kuongoza kuhusu kutahiriwa. Paulo alifanya nini kisha pale? Alimuambia hivi Barnaba: “Turudie sasa na tutembelee ndugu katika kila muji kwenye tulitangaza neno la Yehova, tuone wako namna gani.” (Mdo. 15:36) Paulo hakukuwa anamaanisha kuenda tu kutembelea wale Wakristo wapya. Habari yenye kuwa mu kitabu ya Matendo inatusaidia kujua kusudi ya safari ya pili ya Paulo ya umisionere. Kwanza, angeendelea kuambia ndugu kuhusu uamuzi wa baraza yenye kuongoza. (Mdo. 16:4) Pili, juu alikuwa mwangalizi mwenye kusafiri, Paulo aliazimia kabisa kutia nguvu makutaniko na kusaidia ndugu na dada wakuwe na imani ya nguvu. (Ro. 1:11, 12) Namna gani tengenezo ya Mashahidi wa Yehova leo inafuata ule mufano wa mitume?

5. Leo Baraza Yenye Kuongoza inatumia njia gani ili kutia moyo makutaniko na kuitolea muongozo?

5 Leo, Kristo iko anatumia Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova ili kuongoza kutaniko yake. Wale wanaume waaminifu na wenye ni watiwa-mafuta, wanatumia barua, vichapo vyenye kuwa ku Enternete na vyenye kuchapishwa, mikutano, na njia zingine ili kutia moyo makutaniko ya mu dunia yote na kuipatia muongozo. Kila wakati, Baraza Yenye Kuongoza inajikaza kujua muzuri hali ya kila kutaniko. Njo maana, inatumaka waangalizi wenye kusafiri ili watembelee makutaniko. Baraza Yenye Kuongoza imeweka moja kwa moja maelfu ya wazee wenye kustahili mu dunia yote ili wakuwe waangalizi wa muzunguko.

6, 7. Waangalizi wa muzunguko wanafanya mambo gani mbalimbali?

6 Leo wakati waangalizi wa muzunguko wanatembelea makutaniko, wanahangaikiaka kila mutu mu kutaniko na kutia nguvu imani ya ndugu na dada. Namna gani? Kwa kufuata mufano muzuri wa Wakristo wa mu karne ya kwanza sawa vile Paulo. Paulo aliambia hivi Timoteo mwangalizi mwenzake: “Hubiri neno; fanya vile kwa bidii katika nyakati zenye kufaa na nyakati zenye kuwa ngumu; karipia, kemea, chochea, kwa uvumilivu wote na ufundi wa kufundisha. . . . Fanya kazi ya mweneza-injili.”​—2 Ti. 4:2, 5.

7 Sawa vile ile maneno inaonyesha, mwangalizi wa muzunguko na bibi yake, kama alishaoa, wanatumikaka pamoya na wahubiri wa mu kutaniko mu aina mbalimbali ya mahubiri. Kwa sababu ni walimu wazuri na wanapenda mahubiri, mufano wao unachochea ndugu na dada. (Ro. 12:11; 2 Ti. 2:15) Waangalizi wa muzunguko wanakuwaka na upendo na wanajitoaka sana kwa ajili ya wengine. Wanafurahiaka kutoa wakati wao na nguvu yao juu ya kutumikia wengine, na wanakuwaka tayari kusafiri kwenye hali ya hewa haiko muzuri na hata mu maeneo hatari. (Flp. 2:3, 4) Pia, waangalizi wa muzunguko wanatia moyo, wanafundisha, na kuchochea kila mutu mu kutaniko kupitia hotuba zao zenye kutegemea Biblia. Ni muzuri watu wote mu kutaniko wafikirie mufano wao na wajikaze kuiga imani yao.​—Ebr. 13:7.

“Mulipuko Mukali wa Kasirani” (Mdo. 15:37-41)

8. Barnaba alitenda namna gani wakati Paulo alimuambia watembelee ndugu pamoya?

8 Barnaba anakubali kuenda pamoya na Paulo ili ‘kutembelea ndugu.’ (Mdo. 15:36) Paulo na Barnaba walishatumika pamoya na wanajua muzuri ndugu na dada wa mu makutaniko yenye watatembelea. (Mdo. 13:2–14:28) Ilionekana kama ilikuwa wazo ya muzuri watumike tena pamoya. Lakini tatizo moya inatokea. Andiko ya Matendo 15:37 inasema hivi: “Barnaba alikuwa ameamua kabisa waende pamoja na Yohana, mwenye aliitwa Marko.” Barnaba hakukuwa anatoa tu pendekezo. Lakini “alikuwa ameamua kabisa” kuenda na binamu yake Marko mu hii safari ya umisionere.

9. Juu ya nini Paulo hakukubali wazo ya Barnaba?

9 Paulo hakukubali ile wazo. Juu ya nini? Habari inaendelea hivi: “Lakini Paulo hakutaka waende pamoja [na Marko], kwa sababu aliwaacha kule Pamfilia na hakuenda pamoja nao kwenye kazi.” (Mdo. 15:38) Marko alikuwa pamoya na Paulo na Barnaba mu safari yao ya kwanza ya umisionere. Lakini hakufika mupaka mwisho wa safari. (Mdo. 12:25; 13:13) Ku mwanzo-mwanzo wa safari, wakati walikuwa wangali Pamfilia, Marko aliacha mugao wake na kurudia Yerusalemu. Biblia haiseme juu ya nini alirudia. Lakini Paulo aliona kama Marko hakukuwa na sababu ya muzuri ya kurudia Yerusalemu, na ile ilifanya Paulo ajiulize ikiwa anaweza tena kumutumainia.

10. Ni nini ilitokea kisha Paulo na Barnaba kukosa kuelewana?

10 Lakini Barnaba aliazimia kabisa waende pamoya na Marko. Paulo naye alikatala kabisa waende naye. Matendo 15:39 inasema hivi: “Halafu kukatokea mulipuko mukali wa kasirani, na hivyo wakaachana.” Barnaba akachukua mashua na kurudia kwao, ku kisiwa wa Kipro. Akaenda pamoya na Marko. Paulo akaendelea na safari yake ya umisionere. Habari inaendelea hivi: “Paulo akamuchagua Sila na kuondoka kisha ndugu kumuweka katika fazili zenye hazistahiliwe za Yehova.” (Mdo. 15:40) Alisafiri pamoya naye na ‘wakapitia Siria na Kilikia, wakitia makutaniko nguvu.’​—Mdo. 15:41.

11. Ni sifa gani zitatusaidia tuendelee kuwa marafiki na mutu mwenye ametukosea?

11 Hii habari inatukumbusha kama siye pia tuko watu wenye hawakamilike. Paulo na Barnaba walikuwa wajumbe wa pekee wa baraza yenye kuongoza. Na inawezekana kisha wakati, Paulo alifikia kuwa kati ya ndugu wa baraza yenye kuongoza. Paulo na Barnaba walikuwa watu wazuri, lakini mu hii hali walishindwa kujizuia kwa sababu ya kutokamilika. Waliacha ile hali iharibu urafiki wao? Hata kama Paulo na Barnaba hawakukuwa wakamilifu, walikuwa wanyenyekevu na walijikaza kumuiga Yesu. Kisha wakati, walisameheana na walirudisha urafiki kati yao. (Efe. 4:1-3) Paulo na Marko walifikia kutumika pamoya mu migao ingine.a​—Kol. 4:10.

12. Kama Paulo na Barnaba, wazee leo wanapaswa kuwa na sifa gani?

12 Hata kama Paulo na Barnaba walikasirika mu hii hali, hawakukuwa watu wa kasirani. Barnaba alijulikana kuwa mutu muchangamufu na mukarimu. Njo maana, kuliko kumuita ku jina yake Yosefu, mitume walimupatia jina Barnaba, yenye inamaanisha “Mwana wa Faraja.” (Mdo. 4:36) Paulo pia alijulikana kuwa mutu mupole na mwenye kuhangaikia watu. (1 Te. 2:7, 8) Leo pia wazee wote, kutia ndani waangalizi wa muzunguko, wanapaswa kumuiga Paulo na Barnaba. Wanapaswa kuwa wanyenyekevu na wanapaswa kutendea ndugu na dada na wazee wenzao kwa upole na kuwahangaikia kwa upendo.​—1 Pe. 5:2, 3.

“Walikuwa Wanatoa Ushahidi Muzuri Juu Yake” (Mdo. 16:1-3)

13, 14. (a) Timoteo alikuwa nani, na inawezekana Paulo alikutana naye namna gani? (b) Juu ya nini Paulo alishangazwa na Timoteo? (c) Timoteo alipewa mugao gani?

13 Mu safari yake ya pili ya umisionere, Paulo alifika Galatia, jimbo ya Waroma, kwenye makutaniko fulani ilikuwa imeanzishwa. “Alifika Derbe na pia Listra.” Habari yenye kuwa mu Matendo inaendelea hivi: “Na mwanafunzi mumoja mwenye kuitwa Timoteo alikuwa kule, alikuwa mwana wa mwanamuke Muyahudi mwenye alikuwa muamini, lakini baba yake alikuwa Mugiriki.”​—Mdo. 16:1.b

14 Inaonekana Paulo alikuwa amekutana na familia ya Timoteo wakati alitembelea ile eneo kwa mara ya kwanza mu mwaka wa 47 K.K.Y. Sasa wakati anarudia kule kwa mara ya pili, miaka mbili ao tatu kisha, Paulo anashangazwa sana na kijana Timoteo. Juu ya nini? Kwa sababu ndugu “walikuwa wanatoa ushahidi muzuri juu yake.” Sifa za muzuri za Timoteo hazikujulikana tu mu kutaniko yake lakini pia mu makutaniko ya pembeni-pembeni. Habari yenye iko mu kitabu ya Matendo inaonyesha kama, ndugu wa Listra na ndugu wa Ikoniamu, yenye ilikuwa ku kilometre 30 hivi, walikuwa wanasema mambo ya muzuri juu yake. (Mdo. 16:2) Kwa muongozo wa roho ya Mungu, wazee walimupatia Timoteo mugao wa maana sana: Kusindikiza Paulo na Sila mu safari yao ya kuhubiri.​—Mdo. 16:3.

15, 16. Juu ya nini ndugu walisema mambo ya muzuri juu ya Timoteo?

15 Ni nini ilifanya ndugu waseme mambo ya muzuri juu ya Timoteo hata kama alikuwa angali kijana? Ni juu ya akili yake? Sura yake? Ao vipawa vyake? Mara mingi, watu wanaona ile mambo kuwa ya maana. Na hata nabii Samweli alichochewa siku moya na namna mutu anaonekana kwa inje. Lakini, Yehova alimukumbusha hivi: “Kwa maana Mungu haone kama vile mwanadamu anaona, kwa sababu mwanadamu bure anaona kile chenye kinaonekana kwa macho, lakini Yehova anaona ndani ya moyo.” (1 Sa. 16:7) Ndugu walipenda Timoteo, haiko kwa sababu ya vipawa vyake, lakini kwa sababu ya sifa zake.

16 Miaka mingi kisha, Paulo alizungumuzia sifa fulani za kiroho za Timoteo. Paulo alionyesha kama Timoteo alikuwa na muelekeo muzuri, alipenda watu na alikuwa tayari kujitoa kwa ajili yao, na kama alikuwa anatumika kwa bidii kwa ajili ya kutaniko. (Flp. 2:20-22) Pia Timoteo alijulikana kuwa ndugu mwenye “imani yenye haina unafiki.”​—2 Ti. 1:5.

17. Leo vijana wanaweza kuiga namna gani Timoteo?

17 Leo, vijana wengi wanaiga Timoteo kwa kukomalisha sifa za muzuri. Kwa hiyo, wanajifanyia jina ya muzuri mbele ya Yehova na watu wake, hata kama wangali vijana sana. (Mez. 22:1; 1 Ti. 4:15) Hawatende kwa namna fulani wakati wako na ndugu na kutenda kwa namna ingine wakati wako na marafiki wao. Kwa hiyo, wanaonyesha imani yenye haina unafiki. (Zb. 26:4) Sawa vile Timoteo, vijana wengi wanaweza kufanya mambo mingi mu kutaniko. Ndugu na dada mu kutaniko wanafurahi sana wakati vijana wanakuwa wahubiri wa habari njema, na wakati wanajitoa kwa Yehova na kubatizwa!

“Kuwa Nguvu Katika Imani” (Mdo. 16:4, 5)

18. (a) Paulo na Timoteo walikuwa wanafanya nini wakati walikuwa wanasafiri? (b) Makutaniko ilipata faida gani?

18 Paulo na Timoteo walitumika pamoya kwa miaka mingi. Juu walikuwa wahubiri wenye kusafiri, baraza yenye kuongoza iliwapatia kazi mbalimbali. Habari yenye kuwa mu kitabu ya Matendo inasema: “Wakati walikuwa wanapita katika miji, walikuwa wanawapatia maagizo yenye yalikuwa yameamuliwa na mitume na wazee wenye walikuwa Yerusalemu ili wayashike.” (Mdo. 16:4) Makutaniko ilifuata muongozo wenye walipata kutoka kwa mitume na wazee wa Yerusalemu. Matokeo yenye ule utii ulileta ilikuwa kwamba, “makutaniko yakaendelea kuwa nguvu katika imani na hesabu ya waamini iliendelea kuongezeka siku kwa siku.”​—Mdo. 16:5.

19, 20. Juu ya nini Wakristo wanapaswa kutii “wale wenye wanaongoza”?

19 Leo pia, kwa sababu Mashahidi wa Yehova wanatii muongozo wenye wanapata kutoka kwa “wale wenye wanaongoza” kati yao, wanapata faida mingi. (Ebr. 13:17) Kwa sababu mambo inaendelea kubadilika mu hii ulimwengu, ni jambo ya maana sana tuendelea kusikiliza kwa uangalifu na kutumikisha muongozo wenye tunapata kutoka kwa “mutumwa muaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:45; 1 Ko. 7:29-31) Kufanya vile, kutatusaidia tuendelee kuwa na imani yenye nguvu, na kutatusaidia kuendelea kubakia bila doa kutokana na ulimwengu.​—Yak. 1:27.

20 Paulo, Barnaba, na wazee wengine watiwa-mafuta wa wakati wa mitume hawakukuwa wakamilifu. Ni vile pia wazee leo, kutia ndani ndugu wa Baraza Yenye Kuongoza, hawako wakamilifu. (Ro. 5:12; Yak. 3:2) Lakini Baraza Yenye Kuongoza ni yenye kutumainika kwa sababu inafuata kwa ukaribu Neno ya Mungu na mufano wa mitume. (2 Ti. 1:13, 14) Ile inafanya makutaniko iendelee kutiwa nguvu katika imani.

TIMOTEO ANATUMIKA “ILI KUENDELEZA HABARI NJEMA”

Paulo alisamini sana kazi ya bidii ya Timoteo. Kisha wale wanaume wawili kutumika pamoya kwa miaka 11 hivi, Paulo aliandika hivi kuhusu Timoteo: “Sina mutu mwingine mwenye kuwa na muelekeo kama wake mwenye atajali kabisa mahangaiko yenu. . . . Munajua uhakikisho wenye alitoa juu yake mwenyewe, kwamba kama mutoto na baba yake alitumika pamoja na mimi ili kuendeleza habari njema.” (Flp. 2:20, 22) Timoteo alikuwa tayari kujitoa ili kuendeleza kazi ya kuhubiri. Njo maana, mutume Paulo alimupenda sana na alituachia mufano muzuri.

Timoteo.

Baba ya Timoteo alikuwa Mugiriki na mama yake alikuwa Muyahudi. Inaonekana Timoteo alikomalia Listra. Tangu wakati alikuwa mutoto, mama yake Eunike na tate yake Loisi walimufundisha Maandiko. (Mdo. 16:1, 3; 2 Ti. 1:5; 3:14, 15) Inawezekana wote watatu walifikia kuwa Wakristo wakati Paulo alitembelea Listra kwa mara ya kwanza.

Wakati Paulo alirudia tena Listra kisha miaka fulani, ndugu wa “kule Listra na Ikoniamu walikuwa wanatoa ushahidi muzuri” juu ya Timoteo mwenye inawezekana alikuwa na miaka 20 hivi. (Mdo. 16:2) Roho ya Mungu ilikuwa imetoa “unabii mbalimbali” kuhusu ule kijana mwanaume, na kupatana na ile Paulo na wazee waliamua kupatia Timoteo mugao wa pekee. (1 Ti. 1:18; 4:14; 2 Ti. 1:6) Alipaswa kusindikiza Paulo mu kazi ya umisionere. Timoteo alipaswa kuacha familia yake, na ili Wayahudi wenye angetembelea wasikuwe na sababu yoyote ya kukwazika, alipaswa kutahiriwa.​—Mdo. 16:3.

Timoteo alisafiri mu maeneo mingi. Alihubiri pamoya na Paulo na Sila katika Filipi, alihubiri na Sila katika Beroya, na alihubiri yeye peke katika Tesalonike. Wakati Timoteo alikutana tena na Paulo katika Korinto, alimupatia habari ya muzuri kuhusu upendo na uaminifu wenye ndugu wa Tesalonike walionyesha hata kama walikuwa katika taabu. (Mdo. 16:6–17:14; 1 Te. 3:2-6) Wakati Paulo alikuwa Efeso alipata habari ya mubaya kuhusu Wakorinto, kwa hiyo aliamua kumutuma Timoteo arudie Korinto. (1 Ko. 4:17) Kisha wakati fulani, wakati Paulo alikuwa angali Efeso, alituma Timoteo na Erasto waende Makedonia. Lakini wakati Paulo aliandikia Waroma, Timoteo alikuwa alisharudia Korinto na alikuwa na Paulo. (Mdo. 19:22; Ro. 16:21) Ile ni mifano kidogo tu ya safari zenye Timoteo alifanya kwa ajili ya habari njema.

Maneno yenye kutia moyo yenye Paulo aliandikia Timoteo inaweza kuonyesha kama Timoteo aliona kuwa hakustahili mugao wenye alikuwa anatumikia. Paulo alimuandikia hivi: “Usiruhusu hata kidogo mutu yeyote azarau ujana wako.” (1 Ti. 4:12) Paulo alimutumainia sana Timoteo, njo maana alimutuma mu kutaniko yenye ilikuwa na matatizo mingi na alimupatia hii maagizo: “Uamuru watu fulani wasifundishe fundisho tofauti.” (1 Ti. 1:3) Pia, Paulo alimuambia Timoteo kama anaweza kuweka waangalizi na watumishi wa huduma mu kutaniko.​—1 Ti. 5:22.

Paulo alimupenda sana Timoteo juu alikuwa na sifa za muzuri. Maandiko inaonyesha kama ule kijana mwanaume alitumika kwa ukaribu sana, kwa uaminifu, na kwa upendo pamoya na Paulo. Alikuwa sawa vile mwana wake. Njo maana Paulo aliandika kama anakumbuka machozi ya Timoteo, anatamani sana kumuona, na anasali kwa ajili yake. Sawa vile baba anahangaikiaka mutoto wake, Paulo alipatia Timoteo mashauri kuhusu ‘ugonjwa wake wa mara kwa mara.’ Inaonekana alikuwa nagonjwa tumbo.​—1 Ti. 5:23; 2 Ti. 1:3, 4.

Wakati Paulo alifungwa kwa mara ya kwanza kule Roma, Timoteo alikuwa pamoya naye. Inawezekana kwa wakati fulani, Timoteo naye alifungwa mu gereza. (Flm. 1; Ebr. 13:23) Tunajua kama wale wanaume wawili walikuwa na uhusiano wa karibu sana, juu wakati Paulo aliona kama anakaribia kufa, aliandikia hivi Timoteo: “Fanya nguvu yako yote ili ukuje kwangu bila kuchelewa.” (2 Ti. 4:6-9) Biblia haionyeshe wazi ikiwa Timoteo alifika mbele ya wakati na kuonana tena na Paulo, mupendwa wake na mwalimu wake, mbele akufe.

MARKO ALIKUWA NA MAPENDELEO MINGI

Injili ya Marko inaeleza kama wale wenye walimukamata Yesu walijaribu pia kukamata “kijana mumoja” mwenye aliponyoka na “akakimbia akiwa uchi.” (Mk. 14:51, 52) Kwa sababu ni Marko, mwenye anaitwa pia Yohana Marko, njo tu aliandika ile habari mu Injili, inawezekana ule kijana alikuwa yeye. Kama ni vile, inawezekana Marko alionanaka na Yesu wakati fulani.

Marko iko nasikiliza na iko naandika wakati mwanaume mwenye komaa iko nazungumuza.

Kisha miaka 11 hivi, wakati Herode Agripa alikuwa anatesa Wakristo, “watu fulani” wa mu kutaniko ya Yerusalemu walikutana mu nyumba ya Maria, mama ya Marko, ili kusali. Ni kwao njo Petro aliendaka kisha kufunguliwa kimuujiza kutoka mu gereza. (Mdo. 12:12) Kwa hiyo, inawezekana Marko alikomalia mu nyumba yenye ilifikia kutumiwa ili kufanya mikutano ya Kikristo. Bila shaka alijua muzuri wanafunzi wa kwanza-kwanza wa Yesu, na alichochewa kuwaiga.

Marko alitumika kwa ukaribu na waangalizi wengi wa makutaniko ya kwanza-kwanza ya Kikristo. Inaonekana kuwa, mugao wake wa kwanza ulikuwa kutumika pamoya na binamu yake Barnaba na mutume Paulo kule Antiokia ya Siria. (Mdo. 12:25) Wakati Barnaba na Paulo walienda mu safari yao ya kwanza ya umisionere, Marko alisafiri pamoya nao. Walienda kwanza Kipro na kisha Asia Ndogo. Wakati walikuwa kule, Marko alirudia Yerusalemu kwa sababu zenye hazijulikane. (Mdo. 13:4, 13) Sawa vile sura ya 15 ya kitabu ya Matendo inaonyesha, kisha Paulo na Barnaba kukosa kuelewana kwa sababu ya Marko, Marko na Barnaba waliendelea na utumishi wa umisionere katika Kipro.​—Mdo. 15:36-39.

Inaonekana kuwa, wote walikuwa walishamaliza ile tatizo ya kukosa kuelewana juu, kufikia mwaka wa 60 ao 61 K.K.Y., Marko alikuwa anatumika tena pamoya na Paulo katika Roma. Paulo, mwenye alikuwa mufungwa mu ule muji, aliandikia hivi kutaniko ya Kolosai: “Aristarko mwenzangu wa utekwa anawatumia salamu zake, na pia Marko, binamu ya Barnaba (mwenye mulipokea maagizo ya kumukaribisha ikiwa atakuja kwenu).” (Kol. 4:10) Kwa hiyo, Paulo alikuwa anafikiria kutuma Yohana Marko kutoka Roma ili aende Kolosai juu asaidie ile kutaniko.

Wakati fulani kati ya mwaka wa 62 na 64 K.K.Y., Marko alitumika pamoya na mutume Petro katika Babiloni. Sawa vile tuliona mu Sura ya 10 ya hii kitabu, walifikia kuwa marafiki sana juu Petro alimuita ule kijana mwanaume, “Marko, mwana wangu.”​—1 Pe. 5:13.

Mwishowe, mu mwaka wa 65 hivi K.K.Y. wakati mutume Paulo alikuwa mu gereza kwa mara ya pili katika Roma, aliandikia hivi Timoteo mwenye alikuwa Efeso: “Chukua Marko ukuje pamoja naye, kwa maana ni mwenye faida kwangu katika utumishi.” (2 Ti. 4:11) Bila shaka, Marko alikubali mara moya na akatoka Efeso ili kurudia Roma. Tunaelewa juu ya nini Barnaba, Paulo, na Petro walimupenda sana!

Pendeleo kubwa zaidi yenye Marko alipata ni kuongozwa na roho ya Yehova ili aandike kitabu moya kati ya vitabu ine vya Injili. Watu fulani wamesema kama habari mingi zenye Marko aliandika alizitosha kwa mutume Petro. Inaonekana kuwa ushuhuda mbalimbali unaunga mukono ile wazo, juu Marko aliandika mambo mingi yenye, mutu tu mwenye alikuwa pale sawa vile Petro, njo angeweza kujua. Lakini, inawezekana Marko aliandika Injili yake wakati alikuwa Roma, hapana wakati alikuwa Babiloni pamoya na Petro. Marko alitumia maneno mingi ya Kilatini na alitafsiri maneno ya Kiebrania yenye ingekuwa nguvu kwa watu wenye hawako Wayahudi kuelewa. Kwa hiyo, inaonekana kuwa aliandika ile Injili zaidi sana kwa ajili ya Watu wa Mataifa.

a Ona kisanduku “Marko Alikuwa na Mapendeleo Mingi.”

b Ona kisanduku “Timoteo Anatumika ‘ili Kuendeleza Habari Njema.’”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine