Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Mufano wa Mitume wa Yesu wa Kuendelea Kukesha Unatufundisha Nini?
    Munara wa Mulinzi—2012 | Mwezi wa 1 15
    • 4, 5. Namna gani mutume Paulo na wenzake walijionea mwongozo wa roho takatifu?

      4 Kwanza, mitume walikesha kwa kufuata muongozo kuhusu mahali pa kuhubiri. Katika habari moja, tunajifunza jinsi Yesu alivyotumia roho takatifu, ambayo Yehova alimutolea, ili kuongoza mutume Paulo na wenzake katika safari zao zisizo rahisi. (Mdo. 2:33) Acheni tuzungumuzie safari hizo.​—Soma Matendo 16:6-10.

  • Mufano wa Mitume wa Yesu wa Kuendelea Kukesha Unatufundisha Nini?
    Munara wa Mulinzi—2012 | Mwezi wa 1 15
    • 7 Wakati huo, wanaume hao wakachukua uamuzi ambao yaelekea haukutazamiwa. Mustari wa 8 unasema hivi: “Kwa hiyo wakapita Misia na kushuka mupaka Troa.” Wakaenda sehemu ya mangaribi na kutembea kilomita 550, wakipitia muji baada ya muji mupaka walipofika kwenye bandari ya Troa, njia iliyofaa ili kuingia Makedonia. Walipofika huko, kwa mara ya tatu, Paulo na wenzake walijaribu kugonga mulango, mara hiyo mulango ulifunguliwa wazi kabisa. Mustari wa 9 unaeleza jambo lililotokea: “Na usiku maono yakamutokea Paulo: mwanamume fulani Mumakedonia alikuwa amesimama akimusihi na kusema: ‘Vuka uingie Makedonia utusaidie.’” Mwishowe, Paulo akajua ni wapi atahubiri. Bila kuchelewa, wakachukua mashua kwenda Makedonia.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine