-
Mapambano kwa Ajili ya Habari Njema Huko ThesalonikeMunara wa Mulinzi—2012 | Mwezi wa 6 1
-
-
Kila mara, Paulo alipofika katika muji fulani, kwa kawaida alikuwa akizungumuza kwanza na Wayahudi kwa sababu wao walifahamu Maandiko. Kufanya hivyo kulimuwezesha kuanzisha mazungumuzo na kuwasaidia waelewe habari njema. Mutu fulani mwenye elimu anasema kama Paulo alizoea kufanya hivyo kwa sababu aliwahangaikia sana watu wa taifa lake ao alipenda kutumia Wayahudi na watu wengine wenye kumuogopa Mungu ili kuchochea Watu wa Mataifa wakubali habari njema.—Matendo 17:2-4.
Ndiyo sababu, wakati Paulo alifika huko Thesalonike, aliingia kwanza katika sinagogi, na ‘[kufikiri na Wayahudi] kwa kutumia Maandiko, akieleza na [kuonyesha kabisa kwa kutaja maandiko] kwamba ilikuwa lazima Kristo ateseke na kufufuliwa kutoka kwa wafu, akisema: Huyu ndiye Kristo, Yesu huyu ninayewatangazia ninyi.’—Matendo 17:2, 3, 10.
Ujumbe wa Paulo ulitokeza ubishi kwa sababu alipenda kusaidia Wayahudi wamutambue Masiya na daraka lake. Wayahudi walitumaini kama Masiya atakuja kuwapigania ili kuwakomboa kutoka utawala wa Waroma. Kwa hiyo, wazo la kusema kama Masiya angeteseka na kufa halikupatana na tumaini lao. Ili kuwasaidia Wayahudi wakubali wazo hilo, Paulo “[alifikiri nao],” ‘akieleza,’ na ‘[kuonyesha kabisa kwa kutaja Maandiko]’—huo ndio ufundi ambao mwalimu muzuri anatumia.a Lakini, je, wale waliomusikiliza Paulo walikubali mafundisho hayo mazuri?
-
-
Mapambano kwa Ajili ya Habari Njema Huko ThesalonikeMunara wa Mulinzi—2012 | Mwezi wa 6 1
-
-
a Labda Paulo alitaja maandiko ambayo leo ni Zaburi 22:7; 69:21; Isaya 50:6; 53:2-7; na Danieli 9:26.
-