Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • bt sura 17 uku. 133-139
  • “Akafikiri Nao kwa Kutumia Maandiko”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Akafikiri Nao kwa Kutumia Maandiko”
  • “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Akafikiri . . . kwa Kutumia Maandiko” (Mdo. 17:1-3)
  • “Wamoja . . . Wakakuwa Waamini” (Mdo. 17:4-9)
  • Walikuwa “Wasikivu” Zaidi” (Mdo. 17:10-15)
  • Mapambano kwa Ajili ya Habari Njema Huko Thesalonike
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Paulo, Sila, na Timoteo
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • “Vuka Uingie Makedonia”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
“Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
bt sura 17 uku. 133-139

SURA YA 17

“Akafikiri Nao kwa Kutumia Maandiko”

Juu ya kufundisha muzuri tunapaswa kutumia Maandiko; mufano muzuri wa Waberoya

Inategemea Matendo 17:1-15

1, 2. Ni nani wako nasafiri kutoka Filipi kuenda Tesalonike, na inawezekana wako najiuliza nini?

BARABARA yenye kutumiwa sana, yenye ilijengwa na mafundi Waroma, ilikatwa katika milima. Muko makelele mingi mu ile barabara: makelele ya punda, ya gari za kukokotwa, na ya watu wenye kusafiri kutia ndani maaskari, wafanyabiashara, na mafundi. Paulo, Sila, na Timoteo wako wanasafiri zaidi ya kilometre 130 mu ile barabara, kutoka Filipi kuenda Tesalonike. Ile safari haiko mwepesi zaidi sana kwa Paulo na Sila. Wakati walikuwa Filipi walipigwa sana, na vidonda vyao haviyapona.​—Mdo. 16:22, 23.

2 Wanapaswa kutembea safari murefu sana, na ile inaweza kuwavunja moyo. Lakini kuzungumuza mu njia kunafanya wafurahie safari. Wangali wanakumbuka mambo yenye ilitokea Filipi, namna ule mulinzi na familia yake walifikia kuwa waamini. Ile jambo imefanya wale wanaume watatu waazimie kabisa kuendelea kutangaza neno ya Mungu. Lakini, wakati wanakaribia muji wa Tesalonike, pengine wanajiuliza ikiwa Wayahudi wenye kuwa mu ule muji watawatendea namna gani. Watawashambulia ao hata kuwapiga, sawa vile katika Filipi?

3. Namna gani mufano wa Paulo wa kuonyesha uhodari mu kazi ya kuhubiri unaweza kutusaidia leo?

3 Mu barua yenye Paulo alifikia kuandikia Watesalonike, alifasiria namna alikuwa najisikia. Alisema hivi: “Hata kama tuliteseka kwanza na kutendewa kwa zarau kule Filipi, kama vile munajua, Mungu wetu alitufanya tusikuwe na woga ili tuwatangazie ninyi habari njema ya Mungu katika upinzani mwingi.” (1 Te. 2:2) Kwa hiyo, inaonekana Paulo alikuwa na mashaka kuhusu kuenda Tesalonike, zaidi sana kisha mambo yenye ilimufikia katika Filipi. Unaelewa namna Paulo alikuwa najisikia? Na weye unaona kama ni nguvu kutangaza habari njema? Paulo alimutegemea Yehova juu amupatie nguvu na amusaidie akuwe na uhodari wenye alikuwa nao lazima. Kujifunza mufano wa Paulo kunaweza kukusaidia na weye ufanye vile.​—1 Ko. 4:16.

“Akafikiri . . . kwa Kutumia Maandiko” (Mdo. 17:1-3)

4. Juu ya nini inawezekana Paulo hakufanya tu juma tatu mu Tesalonike?

4 Kitabu ya Matendo inasema kama, wakati walikuwa Tesalonike, Paulo alihubiri katika sinagogi muda wa Sabato tatu. Ni kusema Paulo alifanya kule juma tatu tu? Hatuwezi kuhakikisha vile. Zaidi ya ile, barua za Paulo zinaonyesha kama wakati walikuwa Tesalonike, yeye na wenzake walifanya kazi ya kimwili ili kutimiza mahitaji yao. (1 Te. 2:9; 2 Te. 3:7, 8) Tena, wakati walikuwa kule, Paulo alipokea musaada mara mbili kutoka kwa ndugu wa Filipi. (Flp. 4:16) Kwa hiyo inawezekana hakufanya mu Tesalonike juma tatu tu, lakini alifanya wakati murefu.

5. Paulo alifanya nini ili watu waamini mambo yenye alikuwa anafundisha?

5 Juu alikuwa na uhodari wa kuhubiri, Paulo alizungumuza na wale wenye walikusanyika katika sinagogi. Kulingana na desturi yake, “[alifikiri] nao kwa kutumia Maandiko, alikuwa anafasiria na kuhakikisha kwa kutumia mambo yenye kuandikwa kwamba ilikuwa lazima Kristo ateseke na afufuliwe kutoka kwa wafu, akisema: ‘Huyu ndiye Kristo, Yesu huyu mwenye ninawatangazia ninyi.’” (Mdo. 17:2, 3) Kumbuka kama Paulo hakupenda tu kuchangamusha wasikilizaji wake; lakini alipenda wafikiri juu ya mambo yenye walikuwa nasikia. Alijua kama wale wenye walikuwa naenda ku sinagogi, walijua Maandiko na waliiheshimia. Lakini hawakuelewa Maandiko muzuri. Kwa hiyo Paulo alifikiri nao, akawafasiria, na kuonyesha kwa kutumia Maandiko kama Yesu wa Nazareti alikuwa Masiya ao Kristo mwenye aliahidiwa.

6. Namna gani Yesu alifikiri na watu kwa kutumia Maandiko, na matokeo ilikuwa nini?

6 Paulo aliiga mufano wa Yesu, mwenye mafundisho yake ilitoka mu Maandiko. Kwa mufano wakati alikuwa nahubiri, aliambia wanafunzi wake kama kulingana na Maandiko, mwana wa binadamu alipaswa kuteswa, kufa, na kufufuliwa. (Mt. 16:21) Kisha kufufuliwa, Yesu alitokea wanafunzi wake. Bila shaka kufanya vile kulionyesha kama alisemaka kweli. Lakini, Yesu hakuachia pale. Kuhusu mambo yenye aliambia wanafunzi fulani, Maandiko inasema hivi: “Akianza na Musa na Manabii wote, akawafasiria mambo yenye kumuhusu yeye mwenyewe katika Maandiko yote.” Matokeo ilikuwa nini? Mitume walishangala na kusema hivi: “Je, mioyo yetu haikukuwa inawaka wakati alikuwa anazungumuza na sisi katika barabara, na wakati alikuwa anatufasiria Maandiko waziwazi?”​—Lu. 24:13, 27, 32.

7. Juu ya nini ni jambo ya maana mafundisho yetu itegemee Maandiko?

7 Habari yenye kuwa mu Neno ya Mungu iko na nguvu. (Ebr. 4:12) Kwa hiyo, leo Wakristo wanatosha mambo yote yenye wanafundisha mu Neno ya Mungu, sawa vile Yesu. Paulo na mitume wengine walifanya pia vile. Siye pia tunafikiri na watu, tunawafasiria maana ya maandiko, na tunawafungulia Biblia ili waone kama mambo yenye tunasema inatoka mu Biblia. Tunafanya vile juu habari yenye tunafundisha haiko yetu. Kwa kutumia Biblia tunasaidia watu waone kama mambo yenye tunafundisha haiko mawazo yetu lakini ni mafundisho ya Mungu. Zaidi ya ile, ni muzuri tuendelee kukumbuka kama ujumbe wenye tunahubiri unategemea kabisa Neno ya Mungu. Ile inafanya watu watumainie ile ujumbe. Kujua ile, kunafanya ukuwe na uhodari wa kuhubiri sawa vile Paulo?

“Wamoja . . . Wakakuwa Waamini” (Mdo. 17:4-9)

8-10. (a) Watu wa Tesalonike walitenda namna gani wakati walisikia habari njema? (b) Juu ya nini Wayahudi fulani walimusikilia Paulo wivu? (c) Wale Wayahudi wapinzani walitenda namna gani?

8 Paulo alikuwa amejionea kama Yesu alisema kweli wakati alisema hivi: “Mutumwa haiko mukubwa kuliko bwana wake. Kama wamenitesa mimi, watawatesa ninyi pia; kama wameshika neno langu, watashika lenu pia.” (Yoh. 15:20) Ni vile mambo ilikuwa katika Tesalonike. Kisha Paulo kuhubiri, watu fulani walikuwa tayari kukubali ile neno, lakini wengine walikatala. Kuhusu wale wenye walikubali, Luka aliandika hivi: “Wamoja kati yao [Wayahudi] wakakuwa waamini [Wakristo] na wakajiunga na Paulo na Sila, na ni vile Wagiriki wengi sana wenye kumuabudu Mungu walifanya, pamoja na wanamuke fulani wenye vyeo.” (Mdo. 17:4) Ni wazi kama wale wanafunzi wapya walifurahi kuelewa muzuri Maandiko.

9 Hata kama watu fulani walifurahia mafundisho ya Paulo, wengine walimukasirikia sana. Wayahudi fulani katika Tesalonike walimusikilia Paulo wivu juu “Wagiriki wengi sana” walikubali ujumbe wake. Wale Wayahudi walifundisha Wagiriki maandiko ya Kiebrania juu wakuwe wageuzwa-imani, na kisha waliwaona kuwa wanafunzi wao. Lakini bila kutazamia, waliona kama Paulo iko naiba wale Wagiriki, tena mbele ya macho yao mulemule mu sinagogi! Wayahudi walikasirika sana.

Paulo na Sila wako nakimbilia fasi fulani ili watu wenye kasirani wasiwatendee mubaya. Mwanaume fulani iko nazungumuza na wale watu ku mulango.

“Walikuwa wanamutafuta Paulo na Sila waletwe inje kwenye kile kikundi.”​—Matendo 17:5

10 Luka anatuelezea mambo yenye ilitokea kisha pale: “Wayahudi wakakuwa na wivu, wakakusanya wanaume fulani waovu wenye walikuwa wanawayawaya katika soko, na wakafanyiza kikundi na kutokeza fujo katika muji. Wakashambulia nyumba ya Yasoni na walikuwa wanamutafuta Paulo na Sila waletwe inje kwenye kile kikundi. Wakati waliwakosa, wakamukokota Yasoni na wamoja kati ya ndugu mupaka kwa watawala wa muji, wakisema kwa sauti kubwa: ‘Watu hawa wenye wamepindua dunia yenye kuikaliwa na watu wako hapa pia, na Yasoni amewakaribisha kama wageni wake. Watu hao wote wanatenda kinyume na maagizo ya Kaisari, wakisema kuko mufalme mwingine, Yesu.’” (Mdo. 17:5-7) Kushambuliwa na ile kikundi yenye kasirani kungekuwa na matokeo gani juu ya Paulo na wenzake?

11. Paulo na wenzake walishitakiwa nini, na pengine Wayahudi wenye waliwashitaki walitumia sheria gani ili kuwashitaki? (Ona maelezo ya chini.)

11 Watu wenye kasirani wakikusanyika pamoya, wanatendaka mubaya sana. Wanaweza kutenda kwa jeuri na bila kujizuia, sawa vile mutoni yenye inayala mupaka maji inakosa kwa kuenda. Wayahudi walitumia kikundi ya vile yenye kasirani juu ya kufukuza Paulo na Sila. Kisha wale Wayahudi kutokeza “fujo katika muji,” walijaribu kusadikisha watawala kama mambo yenye wale wanaume wanashitakiwa inastahili kabisa malipizi. Jambo ya kwanza yenye Paulo na wenzake walishitakiwa ni kama “wamepindua dunia yenye kuikaliwa na watu.” Lakini haiko Paulo na wenzake njo walichochea watu wafanye fujo mu Tesalonike! Jambo ya pili yenye waliwashitaki ilikuwa ya nguvu sana. Wale Wayahudi walisema kama wale wamisionere walikuwa natangaza mufalme mwingine, Yesu, na kwa kufanya vile walikuwa navunja sheria za mutawala wa Roma.a

12. Nini njo inaonyesha kama mashitaka yenye Wakristo wa Tesalonike walishitakiwa ingekuwa na matokeo ya mubaya sana?

12 Kumbuka kama viongozi wa dini walishitaki Yesu mambo ya kufanana na ile. Waliambiaka hivi Pilato: “Tulimukuta mutu huyu akileta muvurugo katika taifa . . . na kusema kwamba yeye mwenyewe ndiye Kristo mufalme.” (Lu. 23:2) Juu pengine Pilato aliwaza kama mutawala wa Roma atawaza kuwa iko naunga mukono mufalme mwingine, alihukumu Yesu kifo. Vilevile, mashitaka yenye Wakristo Watesalonike walishitakiwa, ingewatia mu hatari kubwa. Kitabu fulani inasema hivi: “Ni nguvu kupata maneno ya kufasiria hatari yenye ile ingewaletea, ‘wazo tu ya kusaliti mutawala wa Roma, ingefanya mutu auawe.’” Ile mupango ya mubaya ya Wayahudi wenye chuki ingefanikiwa?

13, 14. (a) Juu ya nini ile kikundi ya watu wenye kasirani ilishindwa kuzuia kazi ya kuhubiri? (b) Namna gani Paulo alitii shauri ya Yesu ya kuwa muangalifu, na namna gani tunaweza kuiga mufano wake?

13 Wale watu wengi wenye kasirani hawakuzuia kazi ya mahubiri iendelee katita Tesalonike. Juu ya nini? Sababu moya ni kwamba, Paulo na Sila hawakupatikana. Zaidi ya ile, watawala wa muji hawakuamini kabisa kama ile mashitaka ilikuwa ya kweli. Kisha kuomba “feza za kutosha,” waliachilia Yasoni na ndugu wengine wenye walikuwa wameletwa mbele yao. (Mdo. 17:8, 9) Paulo alifuata shauri ya Yesu ya kuwa “waangalifu kama nyoka na bila kosa kama njiwa.” Kwa hiyo alijiepusha na hatari ili aendelee kuhubiri fasi ingine. (Mt. 10:16) Bila shaka, hata kama Paulo alikuwa na uhodari ile haikumaanisha kama angejiingiza mu hatari hivihivi tu. Namna gani Wakristo leo wanaweza kuiga mufano wake?

14 Leo pia, viongozi wa dini wamechochea watu wenye jeuri washambulie Mashahidi wa Yehova. Wanashitaki Mashahidi wa Yehova kuwa wanapinga serikali na kusaliti inchi yao, na wanatumia ile mashitaka ili kuchochea wakubwa wa serikali wawatese. Sawa vile wapinzani wa karne ya kwanza, leo pia wapinzani wanafanya vile juu wanatusikilia wivu. Lakini siye Wakristo wa kweli, hatujiingizake mu hatari hivihivi tu. Kama inawezekana tunaepuka kubishana na wale watu wenye kasirani na wenye kukosa usawaziko. Tunapendelea kuendelea na kazi yetu kwa amani, pengine hata kuondoka na kurudia wakati hali itakuwa ilishatulia.

MAMBO YENYE KITABU YA MATENDO INASEMA KUHUSU KAISARI

Matukio yote yenye kitabu ya Matendo na vitabu vingine vya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo vinazungumuzia, ilipitikana mu maeneo yenye ilikuwa chini ya Utawala wa Roma. Kwa hiyo, mutu mwenye mamlaka makubwa zaidi alikuwa mutawala wa Roma. Ni yeye njo Wayahudi wa Tesalonike walimaanisha wakati walizungumuzia “maagizo ya Kaisari.” (Mdo. 17:7) Watawala ine njo walitawala Roma mu kipindi yenye kitabu ya Matendo inazungumuzia, ni kusema Tiberio, Gayo, Klaudio wa Kwanza, na Nero.

  • Tiberio (14-37 K.K.Y.) alikuwa mutawala wakati wa utumishi wa Yesu ku dunia na mu miaka ya kwanza-kwanza ya kuanzishwa kwa kutaniko ya Kikristo. Wakati Yesu alikuwa anahukumiwa, Wayahudi walimaanisha Tiberio wakati walilalamika hivi: “Kama [Pilato] unamufungua mutu huyu, wewe hauko rafiki ya Kaisari. . . . Sisi hatuna mufalme isipokuwa Kaisari.”​—Yoh. 19:12, 15.

  • Gayo mwenye anajulikana pia kwa jina ya Caligula (37-41 K.K.Y.), hazungumuziwe mu Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.

  • Klaudio wa Kwanza (41-54 K.K.Y.) anatajwa mara mbili mu kitabu ya Matendo. Sawa vile nabii Mukristo Agabo alitabiri, “njaa kali” yenye ilitokea kuanzia mwaka wa 46 hivi K.K.Y, ilikuja “juu ya dunia yote yenye kuikaliwa na watu . . . wakati wa Klaudio.” Zaidi ya ile, mu mwaka wa 49 ao ku mwanzo wa mwaka wa 50 K.K.Y., Klaudio ‘aliagiza Wayahudi wote watoke Roma.’ Ile agizo njo ilifanya Akila na Prisila watoke Roma na wahamie Korinto kwenye walikutana na mutume Paulo.​—Mdo. 11:28; 18:1, 2.

  • Nero (54-68 K.K.Y.) njo Kaisari mwenye Paulo aliomba asikilize kesi yake. (Mdo. 25:11) Inasemekana kama ule mutawala alifikia kulaumu Wakristo juu ya moto wenye uliharibu sehemu kubwa ya Roma mu mwaka wa 64 hivi K.K.Y. Muda mufupi kisha pale mu mwaka wa 65 hivi K.K.Y., mutume Paulo alifungwa kwa mara ya pili katika Roma na akauawa.

Walikuwa “Wasikivu” Zaidi” (Mdo. 17:10-15)

15. Waberoya walitenda namna gani wakati walisikia habari njema?

15 Ili kulinda usalama wao, ndugu walituma Paulo na Sila katika Beroya, kwenye umbali wa kilometre 65 hivi. Wakati tu alifika, Paulo alienda ku sinagogi na akazungumuza na watu wenye walikuwa nakusanyika kule. Bila shaka Paulo alifurahi sana kukutana na watu wenye walipenda kusikia habari njema! Luka aliandika hivi kuhusu Wayahudi wenye walikuwa Beroya “walikuwa wasikivu kuliko wale wa Tesalonike, kwa maana walikubali neno kwa hamu kubwa ya akili, na walikuwa wanachunguza Maandiko kwa uangalifu kila siku ili kuona kama mambo hayo yalikuwa vile.” (Mdo. 17:10, 11) Ile haimaanishe kama wale wenye walikubali habari njema katika Tesalonike hawakukuwa na mutazamo muzuri. Paulo alifikia kuandika hivi kuwahusu: “Sisi pia tunamushukuru Mungu bila kuacha, kwa sababu wakati mulipokea neno la Mungu, lenye mulisikia kutoka kwetu, hamukulikubali kama neno la wanadamu, lakini mulilikubali kama vile liko kwa kweli, kama neno la Mungu, lenye pia linafanya kazi ndani yenu ninyi waamini.” (1 Te. 2:13) Sasa, nini njo ilifanya Wayahudi wenye walikuwa Beroya wakuwe wasikivu sana?

16. Juu ya nini Biblia inasema kama Waberoya walikuwa “wasikivu”?

16 Hata kama ilikuwa mara ya kwanza kwa Waberoya kusikia habari njema, hawakuichambua-chambua ao kuipinga; hata vile hawakukuwa watu wa kuamini-amini tu mambo bila sababu. Kwanza, walisikiliza kwa uangalifu mambo yenye Paulo alikuwa nasema. Kisha, walitafuta kujua ikiwa mambo yenye walikuwa wamefundishwa ni ya kweli kwa kuchunguza Maandiko, yenye Paulo aliwasaidia kuelewa. Zaidi ya ile, walijifunza kwa bidii Neno ya Mungu, hapana tu siku ya Sabato, lakini kila siku. Na walifanya vile kwa “hamu kubwa ya akili.” Walikamata wakati ili kuelewa namna mambo ya mupya yenye walitoka kujifunza inapatana na Maandiko. Kisha, wakaonyesha kama ni wanyenyekevu kabisa kwa kufanya mabadiliko. Kwa hiyo “wengi wao wakakuwa waamini.” (Mdo. 17:12) Tunaelewa juu ya nini Luka alisema kama walikuwa “wasikivu”!

17. Juu ya nini Waberoya ni mufano muzuri, na namna gani tunaweza kuendelea kuiga mufano wao hata kisha kuwa waamini?

17 Wale Waberoya hawangewazia kama mufano wao muzuri kuelekea habari njema ungeandikwa mu Neno ya Mungu na ungekuwa mufano muzuri kwetu. Walifanya tu jambo yenye Paulo alitazamia kuwa watafanya na jambo yenye Yehova alipenda wafanye. Siye pia tunatia watu moyo wafanye vile, ni kusema wachunguze Maandiko kwa uangalifu ili imani yao itegemee kabisa Neno ya Mungu. Lakini je, kisha kuwa waamini ni kusema hatuna tena lazima ya kuwa wasikivu? Hapana, tofauti na ile, wakati tunakuwa waamini ni jambo ya maana tupende hata zaidi kujifunza juu ya Yehova na kutumikisha bila kukawia mafundisho yake. Wakati tunafanya vile, tunaacha Yehova atufinyange na atuzoeze kulingana na mapenzi yake. (Isa. 64:8) Ile inafanya Baba yetu wa mbinguni aendelee kututumikisha, na tunamufurahisha.

18, 19. (a) Juu ya nini Paulo alitoka Beroya, lakini aliendelea kufanya nini na tunaweza kumuiga namna gani? (b) Paulo atahubiria nani sasa, na atahubiria wapi?

18 Paulo hakubakia Beroya kwa wakati murefu. Kitabu ya Matendo inasema hivi: “Wakati Wayahudi wa Tesalonike walisikia kwamba Paulo alikuwa anatangaza pia neno la Mungu kule Beroya, wakaenda kule ili kuchochea na kutia watu wengi katika musukosuko. Mara moja ndugu wakamusindikiza Paulo mupaka kwenye bahari, lakini Sila na Timoteo wakabakia kule. Hata hivyo, wale wenye walimusindikiza Paulo wakaenda naye mupaka Atene, na wakarudia kisha kupokea maagizo kwamba Sila na Timoteo wamufuate Paulo mbio kadiri inawezekana.” (Mdo. 17:13-15) Kusema kweli, wale maadui wa habari njema hawakukuwa na haya kabisa! Kwanza walifukuza Paulo Tesalonike; kisha wanafunga safari mupaka Beroya na kujaribu kuchochea ileile fujo yenye walichocheaka Tesalonike. Lakini walichokea bure. Paulo alijua kama eneo ilikuwa kubwa; kwa hiyo alihama na kuenda kuhubiri fasi ingine. Leo pia haturuhusu mutu yeyote atuzuie kuhubiri!

19 Kisha kutoa ushahidi kwa ukamili kwa Wayahudi katika Tesalonike na Beroya, bila shaka Paulo alikuwa ameelewa kama ni jambo ya maana kutoa ushahidi kwa uhodari na kufikiri na watu kupitia Maandiko. Na siye tumeelewa vile. Sasa, Paulo anajikuta mu hali tofauti. Anapaswa kuhubiria Watu wa Mataifa katika Atene. Watu watatenda namna gani mu ule muji wakati watasikia mahubiri yake? Sura yenye kufuata, itajibia ile ulizo.

a Kulingana na mutu fulani mwenye elimu, ile wakati kulikuwa sheria ya kaisari yenye ilikataza kutangaza “kuja kwa mufalme ao ufalme mupya wenye ungekamata nafasi, ao kuhukumu mutawala mwenye alikuwa anatawala.” Pengine maadui wa Paulo walifasiria mubaya ujumbe wake ili kuonyesha kama alivunja ile sheria. Ona kisanduku “Mambo Yenye Kitabu ya Matendo Inasema Kuhusu Kaisari.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine