Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • “Kutoa Ushahidi Kamili”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
    • ‘Kuhubiri Ufalme wa Mungu’ (Mdo. 28:30, 31)

      19. Paulo alifanya nini wakati alikuwa mufungwa?

      19 Luka anamalizia habari yake kwa kusema hii maneno yenye kugusa moyo: “[Paulo] akakaa kule kwa miaka mbili ya kuenea katika nyumba yake ya kupanga, na alikuwa anapokea kwa fazili wale wote wenye walikuwa wanakuja kwake, na alikuwa anawahubiria Ufalme wa Mungu na kuwafundisha juu ya Bwana Yesu Kristo kwa uhuru mwingi wa kusema, bila kizuizi.” (Mdo. 28:30, 31) Paulo alikuwa mukaribishaji-wageni, alikuwa na imani, na alikuwa na bidii. Bila shaka alikuwa mufano muzuri!

      20, 21. Zungumuzia mifano ya watu wenye utumishi wa Paulo katika Roma uliletea faida.

      20 Kati ya watu wenye Paulo alipokea kwa upendo, kulikuwa mwanaume mwenye kuitwa Onesimo; alikuwa mutumwa mwenye alikimbia kutoka Kolosai. Paulo alisaidia Onesimo kuwa Mukristo na Onesimo akakuwa ‘ndugu muaminifu na mupendwa’ kwa Paulo. Na hata Paulo alimuita, “mutoto wangu . . . mwenye nimekuwa baba yake.” (Kol. 4:9; Flm. 10-12) Bila shaka alimutia Paulo moyo sana!a

      21 Watu wengine pia walifaidika na mufano muzuri wa Paulo. Aliandikia hivi Wafilipi: “Hali yangu kwa kweli imesaidia kuendeleza habari njema, hivi kwamba vifungo vyangu vya gereza kwa ajili ya Kristo vimejulikana waziwazi kati ya Walinzi wote wa Mufalme na wengine wote. Sasa ndugu wengi katika Bwana wamekuwa na uhakika kwa sababu ya vifungo vyangu vya gereza, na wanaonyesha uhodari mwingi wa kusema neno la Mungu bila woga.”​—Flp. 1:12-14.

  • “Kutoa Ushahidi Kamili”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
    • 25, 26. Paulo aliona utimizo wa unabii gani mbele hata miaka 30 ienee kisha ule unabii kutolewa, na ule unabii uko natimia namna gani leo?

      25 Kitabu ya Matendo inamalizia na habari yenye kuchochea ya mutume wa Kristo mwenye amefungwa mu nyumba, lakini mwenye ‘alikuwa anahubiri Ufalme wa Mungu’ kwa wote wenye walikuwa nakuya kumutembelea. Mu sura ya kwanza tulisoma kuhusu mugao wenye Yesu alipatia wafuasi wake wakati alisema: “Mutapokea nguvu wakati roho takatifu itakuja juu yenu, na mutakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika Yudea yote na Samaria, na mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia.” (Mdo. 1:8) Miaka 30 ilikuwa haiyaenea, lakini ujumbe wa Ufalme ulikuwa ‘umehubiriwa katika uumbaji wote chini ya mbingu.’d (Kol. 1:23) Ile ilionyesha kama roho ya Mungu iko na nguvu kabisa!​—Zek. 4:6.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine