Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • bt sura 4 uku. 28-35
  • “Watu Wenye Hawana Elimu na Watu wa Kawaida”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Watu Wenye Hawana Elimu na Watu wa Kawaida”
  • “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Haiko “Kupitia Nguvu Zetu” (Mdo. 3:11-26)
  • “Hatuwezi Kuacha Kusema” (Mdo. 4:1-22)
  • “Wakapandisha Sauti Zao kwa Mungu” (Mdo. 4:23-31)
  • Hawakutoa Hesabu ‘kwa Wanadamu, Lakini kwa Mungu’ (Mdo. 4:32–5:11)
  • Bwana Wake Alimufundisha Kusamehe
    Tuige Imani Yao
  • Alishinda Woga na Mashaka
    Tuige Imani Yao
  • Alibaki Mushikamanifu Ijapokuwa Majaribu
    Tuige Imani Yao
  • Kama Petro Usichoke, Endelea
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
“Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
bt sura 4 uku. 28-35

SURA YA 4

“Watu Wenye Hawana Elimu na Watu wa Kawaida”

Mitume wanatenda kwa uhodari na Yehova anawabariki

Inategemea Matendo 3:1–5:11

1, 2. Petro na Yohana walifanya muujiza gani karibu na mulango wa hekalu?

JUA ya kisha midi inaangaza, kuko mukutano mukubwa wa watu wengi. Wayahudi wengi wenye kumuogopa Mungu na wanafunzi wa Yesu wanaingia mu uwanja wa hekalu. “Saa ya sala” inakaribia.a (Mdo. 2:46; 3:1) Petro na Yohana wanajikaza kupita kati ya wale watu na kuingia mu hekalu kupitia mulango wenye kuitwa Muzuri. Kuko makelele mingi juu watu wengi wako natembea na kuongea wakati uleule. Kuko pia mwanaume wa kukomala mwenye alizaliwa kilema, mwenye alikuwa anaomba-omba. Ule mwanaume anaomba zawadi za rehema.​—Mdo. 3:2; 4:22.

2 Wakati Petro na Yohana wanakaribia, ule mutu wa kuomba-omba anawaomba makuta vile alikuwa anazoea kufanya. Wale mitume wanasimama, ile inafanya ule mutu akuwe na tumaini. Petro anamuambia: “Sina feza wala zahabu, lakini kile niko nacho ni kile ninakupatia. Katika jina la Yesu Kristo Munazareti, tembea!” Wazia namna watu wanashangala sana wakati Petro anamukamata mukono, na kwa mara ya kwanza mu maisha yake, anasimama! (Mdo. 3:6, 7) Wazia namna ule mutu iko naangalia miguu yake na kupima kutembea kwa mara ya kwanza mu maisha yake! Ile inafanya aanze kuruka-ruka na kumusifu Mungu kwa sauti kubwa!

3. Ni zawadi gani ya muzuri zaidi yenye wale watu wengi na ule mutu mwenye aliponyeshwa wangeweza kupata?

3 Wale watu wengi wanakimbilia kwenye Petro na Yohana wako mu eneo yenye mistari za nguzo za Sulemani. Wakati wako pale kwenye, wakati fulani Yesu alisimamaka na kufundisha, Petro anawaambia maana ya mambo yenye wamejionea. (Yoh. 10:23) Anasema kama wale watu wengi, kutia ndani ule mutu mwenye aliponyeshwa, wanaweza kupata zawadi ya bei sana kupita feza na zahabu. Ile zawadi haiko tu afya ya muzuri, inatia ndani mambo mingi zaidi. Inawapatia nafasi ya kutubu juu zambi zao zisamehewe na wakuwe wafuasi wa Yesu Kristo, “Kiongozi Mukubwa wa uzima,” mwenye alichaguliwa na Yehova.​—Mdo. 3:15.

4. (a) Muujiza wa kuponyesha ulileta fujo gani? (b) Tutazungumuzia maulizo gani mbili?

4 Ni siku ya pekee kabisa! Mutu mumoja ameponyeshwa kimwili na sasa anaweza kutembea. Maelfu ya watu wamepewa nafasi ya kuponyeshwa kiroho, juu waweze kumufurahisha Mungu. (Kol. 1:9, 10) Tena, mambo yenye ilitokea ile siku ilileta fujo kati ya wafuasi waaminifu wa Kristo na watu wenye mamlaka wenye walipenda kuwazuia wasitimize amri ya Yesu ya kuhubiri ujumbe wa Ufalme. (Mdo. 1:8) Namna Petro na Yohana, “watu wenye hawana elimu na watu wa kawaida” walitenda, na njia yenye walitumia wakati walikuwa wanahubiria wale watu wengi, inaweza kutufundisha nini?b (Mdo. 4:13) Na namna gani tunaweza kuwaiga wao na wanafunzi wengine wakati tunapambana na upinzani?

Haiko “Kupitia Nguvu Zetu” (Mdo. 3:11-26)

5. Namna Petro alihubiria watu wengi, inatufundisha nini?

5 Petro na Yohana walisimama mbele ya watu wengi. Walijua kama pengine wamoja kati yao walikuwa kati ya watu wenye waliomba Yesu auawe. (Mk. 15:8-15; Mdo. 3:13-15) Wazia uhodari wa Petro wakati alitangaza kama ule mutu mwenye alikuwa kilema ameponyeshwa katika jina ya Yesu. Petro hakujaribu kuficha ukweli. Aliwalaumu waziwazi na kuonyesha kama walichangia kumuua Kristo. Hata vile, Petro hakuwawekea kinyongo hata kidogo, juu ‘walitenda bila kujua.’ (Mdo. 3:17) Aliwaita “ndugu,” na kukazia mambo yenye kupendeza juu ya ujumbe wa Ufalme. Kama wangetubu na kumuamini Kristo, wangepata “vipindi vya kutuliza” kutoka kwa Yehova. (Mdo. 3:19) Na siye tunapaswa kuwa na uhodari na kusema mambo waziwazi wakati tunatangaza hukumu ya Mungu yenye inakaribia. Lakini, hatupaswe kuwa wakali, tunapaswa kuhangaikia hali ya wengine na kuepuka kuwahukumu. Tunaona watu wenye tunahubiria kuwa ndugu zetu wa kesho ao kesho yake, na vile Petro alifanya, tunakazia zaidi sana mambo yenye kufurahisha ya ujumbe wa Ufalme.

6. Namna gani Petro na Yohana walionyesha unyenyekevu na kiasi?

6 Wale mitume walikuwa na kiasi. Hawakusema kama walifanya ule muujiza kwa uwezo wao. Petro aliuliza wale watu hivi: “Sababu gani munashangazwa sana na jambo hili, na sababu gani munatuangalia kama vile ni kupitia nguvu zetu ao ni kupitia ushikamanifu wetu kwa Mungu?” (Mdo. 3:12) Petro na wale mitume wengine walijua kama kazi yao ilikuwa na matokeo ya muzuri, haiko juu ya nguvu zao wenyewe, lakini juu ya nguvu za Mungu. Walionyesha kiasi kwa kupatia Yehova na Yesu sifa kwa sababu ya matokeo ya muzuri yenye walipata.

7, 8. (a) Ni zawadi gani yenye tunaweza kutolea watu? (b) Ahadi ya “kurudishwa kwa mambo yote” inatimizwa namna gani leo?

7 Na siye tunapaswa kuonyesha kiasi wakati tunatangaza Ufalme. Ni kweli kama leo roho ya Mungu haipatie Wakristo nguvu ya kuponyesha watu kwa njia ya muujiza. Hata vile, tunaweza kusaidia watu waamini Mungu na Kristo na kupokea zawadi ileile yenye Petro aliahidi, ni kusema, kusamehewa zambi na kutulizwa na Yehova. Kila mwaka, mamia ya maelfu wanapokea ile zawadi, na kuwa wanafunzi wenye kubatizwa wa Kristo.

8 Kwa kweli tunaishi wakati wenye Petro aliita “wakati wa kurudishwa kwa mambo yote.” Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mbinguni mu mwaka wa 1914. Ile ilitimiza mambo yenye “Mungu alisema kupitia kinywa cha manabii wake watakatifu wa zamani.” (Mdo. 3:21; Zb. 110:1-3; Da. 4:16, 17) Wakati kidogo kisha pale, Yesu alianza kuongoza kazi ya kurudisha ao kuponyesha watu kiroho ku dunia. Mamilioni ya watu wameingizwa mu paradiso ya kiroho, na ile inafanya wakuwe raia wa Ufalme wa Mungu. Wamevua utu wa zamani na “kuvaa utu mupya wenye uliumbwa kupatana na mapenzi ya Mungu.” (Efe. 4:22-24) Vile tu ilikuwa kuhusu kuponyeshwa kwa ule kilema, ile kazi imetimizwa kwa nguvu ya roho ya Mungu, hapana nguvu za wanadamu. Sawa Petro, tunapaswa kutumia Neno ya Mungu kwa uhodari na mu njia yenye kufaa wakati tunafundisha wengine. Matokeo yenye tunapata wakati tunasaidia watu wakuwe wanafunzi wa Kristo inatokana na nguvu ya Mungu, hapana nguvu zetu wenyewe.

“Hatuwezi Kuacha Kusema” (Mdo. 4:1-22)

9-11. (a) Viongozi wa Wayahudi walitenda namna gani wakati walisikia ujumbe wa Petro na Yohana? (b) Mitume waliazimia kufanya nini?

9 Hotuba ya Petro, na ile makelele ya kuruka-ruka ya ule mutu mwenye aliponyeshwa, ilitokeza fujo. Kapiteni wa hekalu mwenye alikuwa na kazi ya kuhakikisha usalama ku hekalu pamoya na wakubwa wa makuhani, wakakuya mbio juu ya kuona jambo yenye ilitokea. Inawezekana walikuwa Wasadukayo. Wasadukayo walikuwa kikundi ya matajiri wenye walikuwa na uvutano mu mambo ya politike; walijikaza kulinda uhusiano muzuri na Waroma, walikatala desturi zenye zilipendwa sana na Wafarisayo, na walipinga fundisho ya ufufuo.c Walikasirika kabisa wakati walikuta Petro na Yohana mu hekalu na wako wanafundisha bila woga kama Yesu alifufuliwa!

10 Wale wapinzani wenye kasirani walitupa Petro na Yohana mu gereza. Kisha siku yenye ilifuata wakawapeleka mbele ya tribinali kubwa ya Wayahudi. Wale watawala wenye kutafuta utukufu, waliona Petro na Yohana kuwa “watu wenye hawana elimu na watu wa kawaida” wenye hawakukuwa na haki ya kufundisha mu hekalu. Hawakusomea ku masomo ya kidini yenye kujulikana sana. Hata vile, maneno yao yenye kuwa wazi na yenye kusadikisha, ilishangaza sana watu. Nini njo ilisaidia Petro na Yohana? Jambo moya ni juu ‘walikuwaka pamoja na Yesu.’ (Mdo. 4:13) Tofauti kabisa na waandishi, Bwana wao alikuwa anafundisha kama mutu mwenye mamlaka.​—Mt. 7:28, 29.

11 Ile tribinali ililazimisha wale mitume waache kuhubiri. Ile wakati, amri za ile tribinali ziliheshimiwa sana. Majuma fulani tu mbele ya pale, wakati Yesu alisamba mbele ya ileile tribinali, wenye kuifanyiza walisema hivi: “Anastahili kufa.” (Mt. 26:59-66) Hata vile, Petro na Yohana hawaogope. Wakiwa wenye kusimama mbele ya wale wanaume matajiri, wenye elimu, na wenye uvutano mukubwa, Petro na Yohana wanajibia hivi kwa heshima lakini bila woga: “Kama ni jambo lenye kuwa sawa mbele ya macho ya Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko kumusikiliza Mungu, muamue ninyi wenyewe. Lakini sisi hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo yenye tumeona na kusikia.”​—Mdo. 4:19, 20.

KUHANI MUKUBWA NA WAKUBWA WA MAKUHANI

Kuhani mukubwa aliwakilisha Waisraeli mbele ya Mungu. Mu Karne ya kwanza K.K.Y., alikuwa pia anasimamia Sanhedrini. Viongozi wengine wa Wayahudi walikuwa wakubwa wa makuhani. Kati yao kulikuwa makuhani wakubwa wa zamani, sawa vile Anasi, na pia wanaume wengine wenye kukomala wa mu familia zenye makuhani wakubwa walitoka ndani. Mutu mwenye elimu mwenye kuitwa Emil Schürer aliandika kama kuhani mwenye alitoka mu zile familia “aliheshimiwa zaidi” kati ya makuhani wengine.

Maandiko inaonyesha kama mutu alikuwa kuhani mukubwa maisha yake yote. (Hes. 35:25) Lakini, mu kipindi yenye kitabu ya Matendo inazungumuzia, magavana na wafalme wenye waliwekwa na Waroma, waliweka na kutosha makuhani wakubwa vile walipenda. Lakini, inaonekana kuwa wale viongozi wapagani walichagua makuhani kutoka mu uzao wa Haruni.

Usiache kitu yoyote ikuzuie kuzungumuzia mambo ya muzuri ya kiroho yenye umeona na kusikia

12. Nini inaweza kutusaidia tukuwe hodari na tuzungumuze kwa usadikisho zaidi?

12 Na weye unaweza kuonyesha uhodari wa vile? Unajisikiaka namna gani wakati unapata nafasi ya kuhubiria matajiri, watu wenye walisomaka sana, ao wenye kujulikana sana? Unafanyaka nini kama watu wa familia yako, wanafunzi wenzako, ao wafanyakazi wenzako wanakuchekelea juu ya imani yako? Unaogopaka? Kama ni vile, usivunjike moyo. Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alifundisha mitume wake namna ya kutetea imani yao bila woga na kwa heshima. (Mt. 10:11-18) Kisha kufufuliwa, Yesu aliahidi wanafunzi wake kama angeendelea kuwa pamoya nao “mupaka umalizio wa mupangilio wa mambo.” (Mt. 28:20) Chini ya uongozi wa Yesu, “mutumwa muaminifu na mwenye busara” anatufundisha namna ya kutetea imani yetu. (Mt. 24:45-47; 1 Pe. 3:15) Anafanya vile kupitia mikutano, kama vile Utumishi na Maisha ya Mukristo, na kupitia vichapo vyenye kutegemea Biblia, sawa vile habari zenye kuwa ku sehemu “Majibu ya Maulizo juu ya Biblia,” yenye inapatikana ku jw.org. Uko unatumia muzuri vile vifaa? Ukifanya vile, utakuwa hodari na utazungumuza kwa usadikisho zaidi. Na sawa vile mitume walifanya, hautaacha kitu yoyote ikuzuie kuzungumuzia mambo ya muzuri ya kiroho yenye umeona na kusikia.

Dada moya iko anahubiria mufanyakazi mwenzake wakati wa wanapumuzika kidogo.

Usiache kitu yoyote ikuzuie kuzungumuzia mambo ya muzuri ya kiroho yenye umejifunza

“Wakapandisha Sauti Zao kwa Mungu” (Mdo. 4:23-31)

13, 14. Tukipata upinzani, tunapaswa kufanya nini, na juu ya nini?

13 Kisha tu kuachiliwa, Petro na Yohana walikutana na wengine mu kutaniko. Wote pamoja, “wakapandisha sauti zao kwa Mungu” na kumuomba awapatie uhodari wa kuendelea kuhubiri. (Mdo. 4:24) Petro alijua muzuri kama ni kukosa akili kujaribu kufanya mapenzi ya Mungu kwa kutegemea nguvu yake mwenyewe. Majuma fulani yenye ilikuwa imepita, Petro alijitumainia kupita kiasi na kuambia hivi Yesu: “Hata kama wengine wote wanakwazika kwa sababu ya mambo yenye yatakupata, mimi sitakwazika hata kidogo!” Lakini vile tu Yesu alitabiri, Petro aliogopa wanadamu na kumukana rafiki na mwalimu wake. Lakini, Petro aliacha makosa yake imufundishe.​—Mt. 26:33, 34, 69-75.

14 Kama unapenda kuendelea kutoa ushahidi juu ya Kristo, haitoshe tu kuazimia kuhubiri. Wakati wapinzani wanajaribu kuvunja imani yako, ao kukuzuia usihubiri, fuata mufano wa Petro na Yohana. Umuombe Yehova akupatie nguvu. Tafuta musaada wa kutaniko. Ambia wazee na ndugu na dada wengine wenye kukomala kiroho magumu yenye uko nayo. Sala za wengine zinaweza kabisa kukutia nguvu.​—Efe. 6:18; Yak. 5:16.

15. Kama uliacha kuhubiri kwa muda fulani, ni mufano gani unaweza kukutia moyo?

15 Kama wakati fulani uliacha kuhubiri juu ya upinzani, usivunjike moyo. Kumbuka kama, wakati Yesu alikufa, mitume wote waliacha kuhubiri kwa muda, lakini bila kukawia walianza tena kutenda. (Mt. 26:56; 28:10, 16-20) Kuliko kuendelea kujihukumu kwa sababu ya makosa yako ya zamani, uache ikufundishe. Na utumie mambo yenye umejifunza ili kutia wengine nguvu.

16, 17. Sala yenye wanafunzi wa Kristo walitoa kule Yerusalemu inaweza kutufundisha nini?

16 Wakati wenye mamlaka wanatutesa, tunapaswa kusali kuhusu nini? Kumbuka kama wanafunzi hawakuomba waepushwe na majaribu. Walikumbuka muzuri hii maneno ya Yesu: “Kama wamenitesa mimi, watawatesa ninyi pia.” (Yoh. 15:20) Lakini wale wanafunzi washikamanifu waliomba Yehova ‘asikilize’ namna wapinzani wao waliwaogopesha. (Mdo. 4:29) Ni wazi kama wale wanafunzi walijua kama mapenzi ya Mungu njo jambo ya maana zaidi. Walitambua kama mateso yenye walikuwa wanapata ilikuwa utimizo wa unabii. Walijua kama, sawa vile Yesu aliwafundisha kusali, mapenzi ya Mungu ‘yangefanyika duniani,’ hata watawala wanadamu waseme nini.​—Mt. 6:9, 10.

17 Juu ya kufanya mapenzi ya Mungu, wanafunzi waliomba Yehova hivi: ‘Uwawezeshe watumwa wako waendelee kutangaza neno lako bila woga wowote.’ Namna gani Yehova alijibia sala yao? “Mahali walikuwa wamekusanyika pamoja pakatetemeshwa, na wote wakajazwa roho takatifu na walikuwa wanasema neno la Mungu bila woga.” (Mdo. 4:29-31) Hakuna kitu yenye inaweza kuzuia mapenzi ya Mungu kufanyika. (Isa. 55:11) Hata hali zikuwe nguvu namna gani, ao adui akuwe nguvu namna gani, tukisali kwa Mungu, tunaweza kuwa hakika kama atatupatia nguvu ya kuendelea kusema neno yake bila woga.

Hawakutoa Hesabu ‘kwa Wanadamu, Lakini kwa Mungu’ (Mdo. 4:32–5:11)

18. Ndugu na dada wa kutaniko ya Yerusalemu walisaidiana namna gani?

18 Ndugu na dada wa ile kutaniko ya mupya yenye ilikuwa Yerusalemu waliongezeka na kuwa zaidi ya 5000.d Hata kama walikuwa watu wa kutokea fasi tofauti-tofauti, wanafunzi walikuwa na “moyo mumoja na nafsi moja.” Walikuwa wameunganishwa katika akili ileile na katika njia ileile ya kufikiri. (Mdo. 4:32; 1 Ko. 1:10) Kisha wale wanafunzi kumuomba Yehova abariki bidii yao hawakufunga mikono. Walitegemezana kiroho na hata kimwili pia, wakati ilikuwa lazima. (1 Yo. 3:16-18) Kwa mufano, mwanafunzi Yosefu, mwenye mitume walikuwa wanaita Barnaba, aliuzisha shamba yake. Na kwa moyo wote akapatia mitume makuta yote. Mitume walitumia ile makuta juu ya kusaidia wale wenye walitoka mbali ili wakae Yerusalemu kwa muda murefu zaidi kusudi wajifunze mambo mingi zaidi kuhusu imani yao ya mupya.

19. Juu ya nini Yehova aliua Anania na Safira?

19 Anania na Safira pia waliuzisha mali yao na kutoa muchango. Walipenda kuonyesha kama wametoa makuta yote, kumbe walikuwa ‘wameficha kiasi fulani cha feza.’ (Mdo. 5:2) Yehova aliwaua, haiko juu muchango yenye walitoa ilikuwa kidogo, lakini ni juu nia yao ya kutoa ilikuwa mubaya na tena walidanganya. ‘Hawakudanganya wanadamu, lakini walimudanganya Mungu.’ (Mdo. 5:4) Sawa tu wanafiki wenye Yesu alilaumu, Anania na Safira walitaka sana kusifiwa na wanadamu kuliko kutafuta kukubaliwa na Mungu.​—Mt. 6:1-3.

20. Tunajifunza nini kuhusu michango yenye tunatoa?

20 Kama vile wanafunzi waaminifu wa karne ya kwanza walifanyaka kule Yerusalemu, leo, mamilioni ya Mashahidi wa Yehova wanaonyesha roho ya ukarimu kwa kutegemeza kazi ya kuhubiri mu dunia yote kupitia michango yao ya kujipendea. Hakuna mwenye anawalazimisha watumie wakati wao ao makuta yao juu ya kutegemeza kazi ya Ufalme. Kwa kweli, Yehova hapendi tumutumikie “kwa kutokupenda wala kwa kulazimishwa.” (2 Ko. 9:7) Wakati tunatoa michango yetu, Yehova haangaliake wingi wa makuta yenye tunatoa, lakini nia yetu. (Mk. 12:41-44) Hatupendi kuwa kama Anania na Safira hata kidogo kwa kumutumikia Mungu ili kujitafutia faida na kujitafutia sifa. Lakini, kama Petro, Yohana, na Barnaba, upendo wa kweli kwa Mungu na kwa wanadamu wenzetu njo utuchochee kumutumikia Yehova.​—Mt. 22:37-40.

PETRO​—MUVUAJI WA SAMAKI ANAKUWA MUTUME MWENYE BIDII

Mu Maandiko Petro anaitwa kwa majina tano. Anaitwa Simioni mu Kiebrania na Simoni mu Kigiriki. Anaitwa pia Petro na pia Kefa wakati inatafsiriwa mu Kiaramu. Anaitwa pia kwa majina yake mbili yenye kutiwa pamoya, Simoni Petro.​—Mt. 10:2; Yoh. 1:42; Mdo. 15:14.

Mutume Petro anabeba kikapu ya samaki.

Petro alikuwa na bibi na alikuwa anaishi fasi moya na ndugu yake na pia mama yake mukwe. (Mk. 1:29-31) Alikuwa muvuvi wa samaki wa Betsaida, muji wenye ulikuwa kaskazini mwa Bahari ya Galilaya. (Yoh. 1:44) Kisha alianza kuishi mu muji wa Kapernaumu wenye haukukuwa mbali na Betsaida. (Lu. 4:31, 38) Ni mu mashua ya Petro njo Yesu aliikala wakati alizungumuza na watu wengi wenye walikuwa wamekusanyika pembeni ya Bahari ya Galilaya. Kisha tu pale Yesu alimusaidia kuvua samaki wengi sana kwa njia ya muujiza. Ile ilifanya Petro aogope sana. Lakini Yesu alimuambia hivi: “Acha kuogopa. Kuanzia sasa utakuwa unavua watu wakiwa wazima.” (Lu. 5:1-11) Petro alikuwa anavua samaki pamoja na ndugu yake Andrea, na pamoya na Yohana, na Yakobo. Wote waine waliacha kazi yao ya kuvua samaki na wakakubali kuwa wafuasi wa Yesu. (Mt. 4:18-22; Mk. 1:16-18) Kisha mwaka moya hivi, Petro alifikia kuwa kati ya watu 12 wenye Yesu alichagua ili wakuwe “mitume” wake, ni kusema “wenye kutumwa.”​—Mk. 3:13-16.

Yesu alichagua Petro, Yakobo, na Yohana ili wakuwe naye wakati wa matukio ya pekee. Waliona wakati Yesu aligeuzwa sura, wakati alifufua binti ya Yairo, na walikuwa pamoja naye wakati alikuwa na huzuni mu bustani ya Getsemane. (Mt. 17:1, 2; 26:36-46; Mk. 5:22-24, 35-42; Lu. 22:39-46) Wale mitume tatu pamoya na Andrea, walimuuliza Yesu kuhusu alama ya kuwapo kwake.​—Mk. 13:1-4.

Petro alikuwa mutu wa moto-moto na wakati fulani alisema mawazo yake bila kufikiri. Inaonekana kama mara mingi yeye njo alikuwa wa kwanza kusema. Mu vitabu vya Injili, kama maneno ya mitume 11 inatiwa pamoya, maneno ya Petro njo ya mingi zaidi. Petro aliuliza maulizo wakati wengine walibakia kimya. (Mt. 15:15; 18:21; 19:27-29; Lu. 12:41; Yoh. 13:36-38) Ni yeye njo alikatala Yesu amunawishe miguu, na wakati Yesu alimurekebisha, Petro alimuambia amunawishe pia mikono na kichwa!​—Yoh. 13:5-10.

Juu Petro alimupenda Yesu sana, alijaribu kumushawishi kama haikukuwa lazima ateseke na kufa. Mara moya Yesu alimurekebisha juu alikuwa na mawazo yenye haifae. (Mt. 16:21-23) Usiku wa mwisho wa Yesu ku dunia, Petro alisema kama hata mitume wengine wamuache Yesu, yeye hatamuacha hata kidogo. Wakati maadui walimukamata Yesu, kwa uhodari Petro alimupigania kwa upanga, na kisha alimufuata mupaka mu uwanja wa kuhani mukubwa. Lakini, uleule usiku Petro alimukana Bwana wake mara tatu, na wakati alitambua jambo yenye alikuwa amefanya, alilia kwa uchungu sana.​—Mt. 26:31-35, 51, 52, 69-75.

Wakati kidogo kisha Yesu kufufuliwa na mbele atokee mitume wake katika Galilaya, Petro aliambia wenzake kama anaenda kuvua samaki, na mitume fulani walienda pamoya naye. Wakati Petro alitambua kama Yesu iko pembeni ya bahari, bila kufikiri alijitupa ndani ya maji na kuogelea mupaka ku inchi kavu. Yesu alipika samaki kwa ajili ya mitume wake na wakati walikuwa wanakula, aliuliza Petro ikiwa anamupenda kuliko “hawa,” ni kusema wale samaki wenye walikuwa mbele yake. Yesu alikuwa natia Petro moyo achague kumufuata wakati wote kuliko kutia kazi ingine pa nafasi ya kwanza, sawa vile kazi ya kuvua samaki.​—Yoh. 21:1-22.

Mu mwaka wa 62-64 hivi K.K.Y., Petro alihubiri habari njema katika Babiloni, yenye ilipatikana mu Iraq ya leo, kwenye kulikuwa Wayahudi wengi. (1 Pe. 5:13) Ni wakati Petro alikuwa Babiloni njo aliandika kitabu ya 1 Petro na pengine aliandika pia 2 Petro wakati alikuwa kule. Yesu “alimutia Petro nguvu,” na kumupatia “utume kwa wale wenye kutahiriwa.” (Gal. 2:8, 9) Kwa upendo na kwa bidii Petro alitimiza kazi yenye Yesu alimupatia.

YOHANA​—MWANAFUNZI MWENYE YESU ALIPENDA

Mutume Yohana alikuwa mwana wa Zebedayo na ndugu ya mutume Yakobo. Inaonekana jina ya mama yake ilikuwa Salome, mwenye pengine alikuwa dada ya Maria, mama ya Yesu. (Mt. 10:2; 27:55, 56; Mk. 15:40; Lu. 5:9, 10) Kwa hiyo, alikuwa binamu ya Yesu. Inaonekana familia ya Yohana ilikuwa tajiri. Kazi ya Zebedayo ya kuvua samaki ilikuwa kubwa mupaka alikuwa anatumikisha watu wengine. (Mk. 1:20) Salome alimusindikiza Yesu, alimutumikia wakati alikuwa Galilaya, na wakati Yesu alikufa alileta manukato ili kutayarisha mwili wa Yesu kwa ajili ya maziko. (Mk. 16:1; Yoh. 19:40) Inawezekana Yohana alikuwa na nyumba yake.​—Yoh. 19:26, 27.

Mutume Yohana iko na kitabu ya kukunjwa mu mikono.

Inawezekana Yohana alikuwaka mwanafunzi wa Yohana Mubatizaji mwenye alikuwa nasimama pamoya na Andrea, wakati Yohana Mubatizaji alimuangalia Yesu na kusema: “Ona, Mwana-Kondoo wa Mungu!” (Yoh. 1:35, 36, 40) Kisha pale, ni wazi kama Yohana mwana wa Zebedayo alimusindikiza Yesu katika Kana na alijionea muujiza wake wa kwanza. (Yoh. 2:1-11) Namna Yohana anafasiria waziwazi mambo yenye Yesu alisema na kufanya Yerusalemu, Samaria, na Galilaya inaweza kuonyesha kama alijionea ile mambo yote. Tunajua kama Yohana alikuwa na imani kabisa juu, kama Yakobo, Petro, na Andrea, aliacha mara moya nyavu zake, mashua yake, na kazi yake ili kumufuata Yesu.​—Mt. 4:18-22.

Yohana hazungumuziwe sana mu vitabu vya Injili sawa Petro. Lakini yeye pia alikuwa moto-moto. Jina yenye Yesu alimupatia yeye na ndugu yake Yakobo inaonyesha vile. Aliwaita Boanerge, ni kusema “Wana wa Ngurumo.” (Mk. 3:17) Ku mwanzo, Yohana alipenda mambo makubwa mupaka yeye na ndugu yake wakaambia mama yao aombe Yesu awapatie cheo ya maana zaidi mu Ufalme wake. Hata kama ile ombi haikukuwa ya muzuri, ilionyesha kuwa waliamini kama Ufalme ulikuwa jambo ya kweli kabisa. Na ile ombi yao ilitolea Yesu nafasi ya kushauria mitume wake kama walipaswa kuwa wanyenyekevu.​—Mt. 20:20-28.

Yohana alionyesha kama alikuwa na bidii sana wakati alijaribu kukataza mwanaume fulani mwenye hakukuwa namufuata Yesu kufukuza pepo wachafu mu jina ya Yesu. Wakati mwingine, Yohana alikuwa tayari kuomba moto ushuke kutoka mbinguni na kuharibu wakaaji wa kijiji fulani ya Samaria wenye walikatala kuonyesha Yesu na wanafunzi wake ukarimu. Ile mambo ilifanya Yesu amurekebishe Yohana. Ni wazi kama kisha wakati, Yohana alifikia kuwa na usawaziko zaidi na huruma zaidi. (Lu. 9:49-56) Hata kama alikosea mara kwa mara, Yohana alikuwa “mwanafunzi mwenye Yesu alipenda.” Kwa hiyo, wakati Yesu alikuwa karibu kufa, alimuomba Yohana amuhangaikie mama yake Maria.​—Yoh. 19:26, 27; 21:7, 20, 24.

Yohana aliishi muda murefu kuliko mitume wengine wote, sawa tu vile Yesu alitabiri. (Yoh. 21:20-22) Yohana alimutumikia Yehova kwa uaminifu kwa miaka 70 hivi. Ku mwisho-mwisho wa maisha yake, wakati Domitian alikuwa mutawala wa Roma, Yohana alipelekwa katika uhamisho mu kisiwa ya Patmo “kwa sababu ya kusema juu ya Mungu na kutoa ushahidi juu ya Yesu.” Kule, mu mwaka wa 96 hivi K.K.Y., Yohana alipewa maono yenye aliandika mu kitabu ya Ufunuo. (Ufu. 1:1, 2, 9) Watu fulani wanaamini kama kisha kuachiliwa, Yohana alienda Efeso, kwenye aliandika kitabu ya Injili yenye kuwa na jina yake na barua ya 1, 2, na 3 ya Yohana, na kisha akakufa katika Efeso mu mwaka wa 100 hivi K.K.Y.

a Mu hekalu, sala zilikuwa zinatolewa wakati wa zabihu ya asubui na ya mangaribi. Zabihu ya mangaribi ilikuwa inatolewa “saa ya kenda (15h00 hivi).”

b Ona kisanduku “Petro​—Muvuaji wa Samaki Anakuwa Mutume Mwenye Bidii,” na pia “Yohana​—Mwanafunzi Mwenye Yesu Alipenda.”

c Ona kisanduku yenye kichwa “Kuhani Mukubwa na Wakubwa wa Makuhani.”

d Mu mwaka wa 33 K.K.Y., pengine kulikuwa Wafarisayo karibu 6000 na hesabu kidogo ya Wasadukayo mu muji wa Yerusalemu. Vile vikundi mbili vilipenda kulinda mamlaka yao. Pengine ile ni sababu ingine yenye ilifanya wajaribu kuzuia wanafunzi kufundisha juu ya Yesu.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine