Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • “Watu Wenye Hawana Elimu na Watu wa Kawaida”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
    • 18. Ndugu na dada wa kutaniko ya Yerusalemu walisaidiana namna gani?

      18 Ndugu na dada wa ile kutaniko ya mupya yenye ilikuwa Yerusalemu waliongezeka na kuwa zaidi ya 5000.d Hata kama walikuwa watu wa kutokea fasi tofauti-tofauti, wanafunzi walikuwa na “moyo mumoja na nafsi moja.” Walikuwa wameunganishwa katika akili ileile na katika njia ileile ya kufikiri. (Mdo. 4:32; 1 Ko. 1:10) Kisha wale wanafunzi kumuomba Yehova abariki bidii yao hawakufunga mikono. Walitegemezana kiroho na hata kimwili pia, wakati ilikuwa lazima. (1 Yo. 3:16-18) Kwa mufano, mwanafunzi Yosefu, mwenye mitume walikuwa wanaita Barnaba, aliuzisha shamba yake. Na kwa moyo wote akapatia mitume makuta yote. Mitume walitumia ile makuta juu ya kusaidia wale wenye walitoka mbali ili wakae Yerusalemu kwa muda murefu zaidi kusudi wajifunze mambo mingi zaidi kuhusu imani yao ya mupya.

  • “Watu Wenye Hawana Elimu na Watu wa Kawaida”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
    • d Mu mwaka wa 33 K.K.Y., pengine kulikuwa Wafarisayo karibu 6000 na hesabu kidogo ya Wasadukayo mu muji wa Yerusalemu. Vile vikundi mbili vilipenda kulinda mamlaka yao. Pengine ile ni sababu ingine yenye ilifanya wajaribu kuzuia wanafunzi kufundisha juu ya Yesu.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine