Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 10/07 uku. 8
  • Sisi Wote Tunatiana Moyo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sisi Wote Tunatiana Moyo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Paulo Akamushukuru Mungu na Akajipatia Uhodari”
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2019
  • Wanajitoaka Sana ili Kututumikia
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
  • Waangalizi wa Kuchunga Kundi
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Waangalizi wa Muzunguko Wanatusaidia Namna Gani?
    Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2007
km 10/07 uku. 8

Sisi Wote Tunatiana Moyo

1 Mtume Paulo aliandikia kutaniko la Roma hivi: “Ninatamani kuwaona ninyi, ili niwape sehemu ya zawadi ya kiroho kusudi mfanywe imara; au, badala ya hivyo, kwamba kuwe na ubadilishanaji wa kitia-moyo kati yenu, kila mmoja kupitia imani ya mwingine, yenu na yangu pia.” (Rom. 1:11, 12) Waangalizi wasafiri wanapotembelea makutaniko katika siku za leo, hilo linatoa pia nafasi za kutiana moyo.

2 Kutaniko: Kwa kawaida, kutaniko linatangaziwa kuja kwa mwangalizi wa mzunguko karibu miezi mitatu mbele afike. Hilo linatusaidia kupata wakati wa kufanya mipango mbele ya wakati ili kufaidika kabisa. (Efe. 5:15, 16) Ikiwa wewe ni mfanyakazi, labda utaweza kuomba ruhusa ya kutoenda kazini ili kutegemeza kazi ya kuhubiri muda wa juma hilo. Wengine wanafanya mpango ili kufanya kazi ya upainia msaidizi mwezi ambao mwangalizi atatembelea kutaniko. Ikiwa umepanga kusafiri, je, unaweza kubadili mipango yako ili uwe katika kutaniko lenu juma hilo?

3 Kusudi kubwa la mwangalizi wa mzunguko kutembelea kutaniko ni kutia watu moyo na kuwazoeza katika kazi ya kuhubiri. Je, unaweza kuomba kuhubiri pamoja naye ao pamoja na mke wake ikiwa yeye ni mwenye kuoa? Mwangalizi wa mzunguko anafurahia kutumika na wahubiri mbalimbali, kutia ndani wale wasio na uzoefu mwingi ao wasio na ufundi katika kazi ya kuhubiri. Wote wanaweza kujifunza kupitia namna yake ya kuhubiri na wanaweza kutumia mapendekezo yote ambayo anaweza kutoa kwa wema. (1 Kor. 4:16, 17) Kumwalika ili kula chakula pamoja naye kutawatolea nafasi nyingine ili mutiane moyo. (Ebr. 13:2) Sikiliza kwa uangalifu hotuba zake, kwa kuwa zinapatana na mahitaji ya kutaniko.

4 Mwangalizi wa Mzunguko: Mtume Paulo hakuwa tofauti na ndugu ambao alitumikia, kwa kuwa naye alipatwa na matatizo na mahangaiko na alikuwa na lazima ya kutiwa moyo na wengine, na alionyesha shukrani kwa hilo. (2 Kor. 11:26-28) Washiriki wa kutaniko la Roma waliposikia kwamba Paulo, ambaye ni mfungwa, alikuwa akikuja kwao, wengine kati yao walisafiri mpaka kwenye soko la Apio, kilometa 74, ili kukutana naye. “Alipowaona, Paulo akamshukuru Mungu na kujipa moyo.” (Mdo. 28:15) Ninyi pia munaweza kumtia moyo mwangalizi wenu wa mzunguko. Mumwonyeshe heshima “mara mbili” kwa kumuunga mkono kwa shauku anapotembelea kutaniko lenu. (1 Tim. 5:17) Muzungumze naye na kumwonyesha shukrani yenu kwa kuwa yeye anajikaza ili kuwasaidia. Mwangalizi na mke wake watafurahi wanapoona imani yenu, upendo wenu, na uvumilivu wenu.—2 The. 1:3, 4.

5 Katika hizi “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo,” ni nani kati yetu asiyekuwa na lazima ya kutiwa moyo? (2 Tim. 3:1) Tuamue sasa kushiriki kabisa katika juma la pekee la utendaji pamoja na mwangalizi wa mzunguko. Sisi wote, waangalizi wasafiri na wahubiri pia, tunaweza kuungana mkono ili kutiana moyo kwa furaha. Kwa kufanya hivyo, sisi pia ‘tutaendelea kufarijiana na kujengana.’—1 The. 5:11.

[Maulizo ya Funzo]

1. Ni nafasi gani za pekee zinazopatikana wakati ambapo waangalizi wasafiri wanatembelea makutaniko?

2. Kwa nini kuja kwa mwangalizi wa mzunguko kunatangazwa mbele ya wakati?

3. Ili tutiwe moyo, tunaweza kufanya nini wakati ambapo mwangalizi anatutembelea?

4. Namna gani tunaweza kumtia moyo mwangalizi wetu wa mzunguko?

5. Kwa nini leo sisi wote tuna lazima ya kutiana moyo mmoja na mwingine?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine