Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Kutembea Kupatana na Roho, Kunamaanisha Uzima na Amani
    Munara wa Mulinzi—2011 | Mwezi wa 11 15
    • 8 Sheria hiyo, pamoja na amri zake nyingi, iliwahukumu watenda zambi. Zaidi ya hilo, makuhani wakuu wa Israeli waliotumika chini ya Sheria hawakuwa wakamilifu, kwa hiyo hawangeweza kutoa zabihu ambayo ingeondoa zambi kabisa. Katika maana hiyo Sheria ilikuwa ‘zaifu kupitia mwili.’ Lakini ‘kwa kumutuma Mwana wake mwenyewe akiwa katika mufano wa mwili wenye zambi’ na kumutoa awe zabihu ya ukombozi, Mungu ‘aliihukumu zambi katika mwili,’ na hivyo kupitia zabihu hiyo ushindi juu ya ‘sheria isiyo na uwezo’ ulipatikana. Kwa hiyo, kwa kuwa Wakristo watiwa-mafuta wana imani katika zabihu ya ukombozi ya Yesu, Yehova anawaona kuwa wenye haki. Paulo anawatia moyo ‘kutembea, si kupatana na mwili, bali kupatana na roho.’ (Soma Waroma 8:3, 4.) Wanapaswa kufanya hivyo kwa uaminifu mupaka mwisho wa maisha yao duniani ili wapewe “taji la uzima.”—Ufu. 2:10.

  • Kutembea Kupatana na Roho, Kunamaanisha Uzima na Amani
    Munara wa Mulinzi—2011 | Mwezi wa 11 15
    • 10. Namna gani sheria ya zambi na kifo inatutawala?

      10 Mutume Paulo aliandika hivi: ‘Kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi.’ (Rom. 5:12) Kwa kuwa sisi wote ni watoto wa Adamu, tunatawaliwa na sheria ya zambi na kifo. Mwili wetu wenye zambi unatuchochea kila mara kufanya mambo yanayomuchukiza Mungu, mambo hayo yanatuongoza kwenye kifo. Katika barua yake kwa Wagalatia, Paulo alitaja matendo hayo na tabia hizo kuwa “matendo ya mwili.” Kisha akaongeza: ‘Wale walio na mazoea ya kufanya mambo ya namna hiyo hawatauriti ufalme wa Mungu.’ (Gal. 5:19-21) Watu hao si tofauti na wale wanaotembea kupatana na mwili. (Rom. 8:4) ‘Kanuni iliyo ndani yao inayowachochea kutenda’ na ‘kanuni za maisha ambazo wamejichagulia’ ni za tamaa ya kimwili kabisa. Lakini je, wale wanaofanya uasherati, wanaoabudu sanamu, wanaopashana habari na roho waovu, ao wanaofanya zambi zingine nzito ndiyo tu wanaotembea kupatana na mwili? Hapana, kwa kuwa matendo ya mwili yanatia ndani pia mambo ambayo watu fulani wanawazia kuwa tu uzaifu wa mutu, kama vile wivu, hasira, na magomvi. Ni nani anayeweza kusema kwamba yeye amekwisha kujikomboa kabisa na hatembei tena kupatana na mwili?

  • Kutembea Kupatana na Roho, Kunamaanisha Uzima na Amani
    Munara wa Mulinzi—2011 | Mwezi wa 11 15
    • 12 Hali yetu ni kama mutu anayetunzwa ugonjwa mukali. Ikiwa tunataka kupona kabisa, tunapaswa kufanya yale muganga anatuambia tufanye. Hata ikiwa kuamini zabihu ya ukombozi kunaweza kutukomboa kutoka katika sheria ya zambi na kifo, tungali watu wasiokamilika na wenye zambi. Ili kuendelea kuwa na uhusiano wa karibu pamoja na Mungu, kukubaliwa naye, na kupata baraka zake, bado kuna jambo lingine tunalopaswa kufanya. Mutume Paulo alizungumuzia pia jambo la kutembea kupatana na roho ili kutimiza “takwa la uadilifu la Sheria.”

      Kutembea Kupatana na Roho

      13. Kutembea kupatana na roho kunamaanisha nini?

      13 Tunapotembea, tunaelekea hatua kwa hatua mahali fulani. Kwa hiyo, ili kutembea kupatana na roho ni lazima tuendelee kufanya maendeleo ya kiroho, lakini hilo halimaanishi kwamba hatutafanya tena makosa. (1 Tim. 4:15) Siku baada ya siku na kulingana na uwezo wetu, tunapaswa kujikaza kutembea, ao kuishi, kupatana na uongozi wa roho. “Kutembea kwa roho” kutafanya tukubaliwe na Mungu.—Gal. 5:16.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine