Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ‘Mulie Pamoja na Watu Wanaolia’
    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo)—2017 | Mwezi wa 7
    • 14. Tunaweza kusema nini ili kufariji watu wenye wamefiwa?

      14 Kwa kweli, inaweza kuwa vigumu kujua ni mambo gani yenye unaweza kumuambia mutu mwenye kuwa na huzuni nyingi. Hata hivyo, Biblia inasema kama ‘ulimi wa mwenye hekima unaponya.’ (Met. 12:18) Wengi wamepata maneno yenye kufariji katika broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa,c yenye wanaweza kuambia mutu mwenye amefiwa. Hata hivyo, mara nyingi jambo la maana zaidi lenye unaweza kufanya ni ‘kulia pamoja na watu wanaolia.’ (Rom. 12:15) Gaby, mwenye bwana yake alikufa, anasema hivi: “Machozi yamekuwa njia ya kuonyesha namna ninajisikia katika moyo wangu. Ndiyo sababu ninafarijiwa wakati marafiki wanalia pamoja na mimi. Wakati huo, sijisikie kuwa niko peke yangu katika huzuni yangu.”

  • ‘Mulie Pamoja na Watu Wanaolia’
    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo)—2017 | Mwezi wa 7
    • 20. Sababu gani ahadi za Yehova zinatutolea faraja kubwa?

      20 Ni jambo lenye kufariji sana kujua kuwa Yehova, Mungu wa faraja yote atamaliza huzuni yote na kutoa faraja ya milele wakati “wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake [Yesu] na kutoka”! (Yoh. 5:28, 29) Mungu anaahidi kuwa “atameza kifo milele, na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova hakika atafuta machozi katika nyuso zote.” (Isa. 25:8) Kwa hiyo, kuliko ‘kulia pamoja na watu wanaolia,’ wakaaji wote wa dunia ‘watashangilia pamoja na watu wanaoshangilia.’​—Rom. 12:15.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine