Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w16 Mwezi wa 1 uku. 20-26
  • Tunapenda ‘Kuenda Pamoja’ na Wewe

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tunapenda ‘Kuenda Pamoja’ na Wewe
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • NI LAZIMA TUJUE MAJINA YA WATU WOTE WENYE WANATIWA MAFUTA LEO?
  • WATIWA-MAFUTA WANAPASWA KUJIONA NAMNA GANI?
  • UNAPASWA KUWATENDEA NAMNA GANI?
  • TUNAPASWA KUHANGAIKIA HESABU?
  • Tutaenda Pamoja na Ninyi
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Roho Inatoa Ushahidi Pamoja na Roho Yetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • “Roho Yenyewe Inatoa Ushahidi”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Juu ya Nini Tunahuzuriaka Ukumbusho?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
w16 Mwezi wa 1 uku. 20-26
Kondoo zinafuata muchungaji kwenye muteremuko wa mulima

Tunapenda ‘Kuenda Pamoja’ na Wewe

‘[Tunapenda] kuenda pamoja na [wewe], kwa maana tumesikia ya kuwa Mungu iko pamoja na ninyi.’—ZEKARIA 8:23.

NYIMBO: 65, 122

UNAWEZA KUELEZA?

  • Namna gani andiko la Zekaria 8:23 linaendelea kutimia?

  • Namna gani Wakristo watiwa-mafuta wanapaswa kujiona?—1 Wakorintho 4:6-8.

  • Sababu gani hatupaswe kuhangaikia hesabu ya wale wenye wanakula mukate na kunywa divai kwenye Ukumbusho?—Waroma 9:11, 16.

1, 2. (a) Yehova alisema nini juu ya wakati wetu? (b) Tutajibu maulizo gani katika habari hii? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

YEHOVA alisema kwamba katika siku zetu, “watu kumi kutoka katika luga zote za mataifa watashika [watakamata], ndiyo, watashika nguo ya Muyahudi, wakisema: ‘Tunapenda kuenda pamoja na [wewe], kwa maana tumesikia ya kuwa Mungu iko pamoja na ninyi.’” (Zekaria 8:23) ‘Muyahudi’ huyo anafananisha wale wenye Mungu ametia mafuta kwa roho takatifu. Wanaitwa pia “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16) “Watu kumi” hao wanafananisha wale wenye kuwa na tumaini la kuishi milele katika dunia. Wanajua kwamba Yehova amebariki kikundi hicho cha watiwa-mafuta na wanaona kuwa ni pendeleo kumuabudu Yehova pamoja nao.

2 Kama vile nabii Zekaria, Yesu pia alisema kwamba watu wa Mungu wangekuwa na umoja. Yesu aliita wale wenye wanangojea kuishi mbinguni ‘kundi ndogo,’ na wale wenye wanangojea kuishi duniani “kondoo wengine.” Lakini alisema kwamba wote wangekuwa “kundi moja” na wangemufuata, yeye ‘muchungaji mumoja’ wao. (Luka 12:32; Yohana 10:16) Kwa sababu kuko vikundi viwili, watu fulani wanaweza kujiuliza hivi: (1) Ni lazima kondoo wengine wajue majina ya watu wote wenye wanatiwa mafuta leo? (2) Wale wenye wametiwa mafuta, wanapaswa kujiona namna gani? (3) Ikiwa mutu fulani katika kutaniko langu anaanza kula mukate na kunywa divai kwenye Ukumbusho, ninapaswa kumutendea namna gani? (4) Ninapaswa kuhangaika wakati ninaona hesabu ya wale wenye wanakula mukate na kunywa divai kwenye Ukumbusho inaendelea kuongezeka? Tutajibu maulizo hayo katika habari hii.

NI LAZIMA TUJUE MAJINA YA WATU WOTE WENYE WANATIWA MAFUTA LEO?

3. Sababu gani hatuwezi kujua kabisa wale wenye watakuwa kati ya wale 144000?

3 Je, ni lazima kondoo wengine wajue majina ya watu wote wenye wanatiwa mafuta leo? Hapana. Sababu gani? Kwa sababu hakuna mutu mwenye anaweza kujua kwa uhakika kabisa ikiwa watiwa-mafuta hao watapokea zawadi yao.[1] (Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.) Hata kama Mungu amewaalika ili kuenda mbinguni, watapokea zawadi yao ikiwa tu wanabakia waaminifu. Shetani anajua jambo hilo; kwa hiyo, anatumia ‘manabii wa uongo’ ili kujaribu “kuwapotosha [kuwadanganya].” (Mathayo 24:24) Wakristo watiwa-mafuta wanaweza kuwa hakika kwamba watapokea zawadi yao wakati tu Yehova mwenyewe anawahakikishia kwamba amewaona kuwa waaminifu. Yehova anawahakikishia jambo hilo, ao kuwatia muhuri kwa mara ya mwisho, muda fulani mbele ya kifo chao, ao muda fulani mbele ‘ziki kubwa’ ianze. —Ufunuo 2:10; 7:3, 14.

Yesu ndiye Kiongozi wetu, na tunapaswa kumufuata yeye tu

4. Kwa sababu hatuwezi kujua majina ya watiwa-mafuta wote wenye kuwa katika dunia leo, namna gani tunaweza ‘kuenda pamoja’ nao?

4 Kwa sababu haiwezekane kujua majina ya watiwa-mafuta wote wenye kuwa katika dunia leo, namna gani kondoo wengine wanaweza ‘kuenda pamoja’ nao? Biblia inasema kwamba “watu kumi” “watashika nguo ya Muyahudi, wakisema: ‘[Tunapenda] kuenda pamoja na [wewe], kwa maana tumesikia ya kuwa Mungu iko pamoja na ninyi.’” Andiko hilo la Biblia linataja Muyahudi mumoja. Lakini maneno ‘wewe’ na ‘ninyi,’ inazungumuzia watu wengi. Hilo linamaanisha kwamba Muyahudi huyo haiko mutu moja tu lakini anafananisha kikundi cha watiwa-mafuta wote. Kondoo wengine wanajua jambo hilo; kwa hiyo, wanamutumikia Yehova pamoja na kikundi hicho. Hawana lazima ya kujua jina la kila mutiwa-mafuta wa kikundi hicho na kumufuata. Yesu ndiye Kiongozi wetu, na Biblia inatuambia kwamba tunapaswa kumufuata yeye tu.—Mathayo 23:10.

WATIWA-MAFUTA WANAPASWA KUJIONA NAMNA GANI?

5. Watiwa-mafuta wanapaswa kufikiria sana onyo gani, na sababu gani?

5 Watiwa-mafuta wanapaswa kufikiria sana onyo lenye kupatikana katika andiko la 1 Wakorintho 11:27-29. (Soma.) Namna gani mutiwa-mafuta anaweza kula mukate na kunywa divai “isivyofaa” kwenye Ukumbusho? Ikiwa haendelee kuwa na uhusiano muzuri pamoja na Yehova na habakie mwaminifu kwake, wakati anakula mukate na kunywa divai, anakosa heshima. (Waebrania 6:4-6; 10:26-29) Onyo hilo kali linakumbusha watiwa-mafuta kwamba wanapaswa kubakia waaminifu ikiwa wanapenda kupokea ‘tuzo [zawadi] la mwito wa Mungu wa kuenda juu kwa njia ya Kristo Yesu.’—Wafilipi 3:13-16.

6. Wakristo watiwa-mafuta wanapaswa kujiona namna gani?

6 Mutume Paulo aliambia Wakristo watiwa-mafuta hivi: ‘Mimi, niliye mufungwa katika Bwana, nawasihi [ninawaomba] ninyi mutembee kwa kuustahili mwito mulioitiwa.’ Namna gani walipaswa kufanya hivyo? Mutume Paulo alifasiria hivi: ‘Mukiwa na unyenyekevu kamili wa akili na upole, mukiwa na ustahimilivu, mukivumiliana katika upendo, mukijitahidi [mukijikaza] sana kuushika umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani.’ (Waefeso 4:1-3) Roho takatifu ya Yehova inasaidia watumishi wake wakuwe wanyenyekevu, na waepuke kuwa na kiburi. (Wakolosai 3:12) Kwa hiyo, watiwa-mafuta hawajione kuwa wao ni wazuri zaidi kuliko wengine. Hawafikiri kwamba Yehova anapaswa kuwapatia roho takatifu zaidi kuliko watumishi wake wengine. Pia, hawafikiri kwamba wao wanaweza kuelewa kweli za Biblia muzuri zaidi kuliko wengine wote. Tena, hawapaswe hata kidogo kuambia mutu fulani kwamba yeye pia ametiwa mafuta na anapaswa kuanza kula mukate na kunywa divai kwenye Ukumbusho. Lakini, ni wanyenyekevu na wanajua kwamba ni Yehova tu ndiye anaalika watu kuenda mbinguni.

7, 8. Wakristo watiwa-mafuta hawatazamie jambo gani, na sababu gani?

7 Hata kama watiwa-mafuta wanaona kuwa ni pendeleo kualikwa kuenda mbinguni, hawatazamie wengine wawatendee kwa njia ya pekee. (Waefeso 1:18, 19; soma Wafilipi 2:2, 3.) Wanajua pia kwamba wakati Yehova aliwatia mafuta, hakujulisha mutu mwengine yeyote. Ndiyo sababu mutiwa-mafuta hashangae ikiwa watu fulani hawakubali mara moja kwamba ametiwa mafuta. Anaelewa kwamba Biblia inatuomba tusiamini haraka-haraka mutu fulani mwenye anasema kwamba Mungu amemupatia daraka fulani la pekee. (Ufunuo 2:2) Kwa sababu mutiwa-mafuta hatazamie wengine wamutendee kwa njia fulani ya pekee, hataambia wale wenye anakutana nao kwa mara ya kwanza kwamba yeye ni mutiwa-mafuta. Kwa hiyo, hapaswe kuambia mutu yeyote kwamba yeye ni mutiwa-mafuta. Pia, hatajisifu juu ya mambo mazuri sana yenye atafanya huko mbinguni.—1 Wakorintho 1:28, 29; soma 1 Wakorintho 4:6-8.

8 Wakristo watiwa-mafuta hawaone kwamba wanafanyiza kikundi fulani cha pekee, na kwamba wanapaswa kupitisha wakati pamoja na watiwa-mafuta wenzao tu. Hawajaribu kutafuta watiwa-mafuta wengine ili kuzungumuzia habari zenye kuwahusu ao kukusanyika katika vikundi ili kujifunza Biblia. (Wagalatia 1:15-17) Kutaniko haliwezi kuendelea kuwa na umoja ikiwa watiwa-mafuta wanafanya hivyo. Wangekuwa hawatende kupatana na roho takatifu, yenye inasaidia watu wa Mungu wakuwe na amani na umoja.—Soma Waroma 16:17, 18.

UNAPASWA KUWATENDEA NAMNA GANI?

9. Sababu gani unapaswa kuwa muangalifu juu ya namna unawatendea wale wenye wanakula mukate na kunywa divai kwenye Ukumbusho? (Soma kisanduku “Upendo ‘Haujiendeshe Bila Adabu.’”)

9 Unapaswa kutendea namna gani ndugu na dada wenye wametiwa mafuta? Yesu aliambia wanafunzi wake hivi: “Ninyi nyote ni ndugu.” Aliongezea hivi: “Yeyote yule anayejiinua atanyenyekezwa, na yeyote yule anayejinyenyekeza atainuliwa.” (Mathayo 23:8-12) Kwa hiyo, hatupaswe hata kidogo kusifu-sifu mutu fulani, hata kama ni ndugu ya Kristo, ni kusema, mutiwa-mafuta. Wakati Biblia inazungumuzia wazee, inatutia moyo tuige imani yao, lakini haiseme kwamba tunaweza kufanya mwanadamu fulani akuwe kiongozi wetu. (Waebrania 13:7) Ni kweli Biblia inasema kwamba watu fulani ‘wanastahili heshima mara mbili.’ Wanastahili heshima hiyo kwa sababu ‘wanasimamia kwa njia nzuri’ na ‘wanafanya kazi kwa bidii katika kusema na kufundisha,’ si kwa sababu wao ni watiwa-mafuta. (1 Timotheo 5:17) Ikiwa tunawasifu-sifu sana watiwa-mafuta na kuwaheshimia kupita kiasi, hilo linaweza kuwafanya wajisikie mubaya. Na jambo la mubaya zaidi, hilo linaweza kuwafanya wakuwe na kiburi. (Waroma 12:3) Hakuna Mukristo mwenye anapenda kufanya jambo fulani lenye linaweza kuchochea mumoja wa ndugu watiwa-mafuta wa Kristo afanye zambi hiyo nzito!—Luka 17:2.

Shahidi wa Yehova anakula mukate kwenye Ukumbusho

Namna gani unapaswa kumutendea mutu mwenye anakula mukate na kunywa divai kwenye Ukumbusho? (Picha hii inapatana na fungu la 9-11)

10. Namna gani unaweza kuonyesha kwamba unaheshimia Wakristo watiwa-mafuta?

10 Namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunaheshimia wale wenye Yehova ametia mafuta? Tutaepuka kuwauliza namna gani walitiwa mafuta. Hilo ni jambo la kipekee lenye hatuna haki ya kujua. (1 Wathesalonike 4:11; 2 Wathesalonike 3:11) Tena, hatupaswe kufikiri kwamba bwana ao bibi, wazazi, ao watu wengine wa familia yao ni watiwa-mafuta pia. Mutu hariti tumaini hilo kutoka kwa familia yake. (1 Wathesalonike 2:12) Tunapaswa pia kuepuka kuuliza maulizo yenye inaweza kuwakwaza wengine. Kwa mufano, tunapaswa pia kuepuka kuuliza bibi ya ndugu mutiwa-mafuta ikiwa anajisikia namna gani juu ya kuishi milele katika dunia bila kuwa pamoja na bwana yake. Lakini, tunaweza kuwa hakika kabisa kwamba katika dunia mupya, Yehova ‘atatosheleza [atatimiza] tamaa ya kila kitu kilicho hai [chenye kuwa na uzima].’—Zaburi 145:16.

11. Namna gani tunajilinda sisi wenyewe wakati tunaepuka kuwasifu-sifu watu wenye kujulikana?

11 Tunajilinda sisi wenyewe, ikiwa hatuone watiwa-mafuta kuwa watu wa maana sana kuliko wengine. Namna gani? Biblia inatuambia kwamba katika kutaniko, kunaweza kuwa ‘ndugu wa uongo’ wenye wanaweza kusema kwamba ni watiwa-mafuta. (Wagalatia 2:4, 5; 1 Yohana 2:19) Pia, watiwa-mafuta fulani wanaweza kukosa kuendelea kuwa waaminifu. (Mathayo 25:10-12; 2 Petro 2:20, 21) Lakini ikiwa tunaepuka “kustaajabia watu mashuhuri [kuwasifu-sifu],” hatutakuwa hata kidogo wafuasi wa wengine, hata wale wenye wametiwa mafuta, ao wenye kujulikana, ao wale wenye wamemutumikia Yehova kwa miaka mingi. Kwa hiyo, ikiwa wanakosa uaminifu ao wanaacha kutaniko, hatutapoteza imani yetu katika Yehova ao kuacha kumutumikia.—Yuda 16

TUNAPASWA KUHANGAIKIA HESABU?

12, 13. Sababu gani hatupaswe kuhangaikia hesabu ya wale wenye wanakula mukate na kunywa divai kwenye Ukumbusho?

12 Kwa miaka mingi yenye imepita, hesabu ya wale wenye wanakula mukate na kunywa divai kwenye Ukumbusho iliendelea kupunguka. Lakini hivi karibuni, hesabu hiyo imekuwa ikiongezeka kila mwaka. Je, jambo hilo linapaswa kutuhangaisha? Hapana. Tuone basi sababu gani hatupaswe kuhangaika.

13 “Yehova anawajua walio wake.” (2 Timotheo 2:19) Yehova anajua kabisa ni nani kwa kweli mwenye ametiwa mafuta, lakini ndugu wenye kuhesabu wale wenye wanakula mukate na kunywa divai kwenye Ukumbusho hawajue jambo hilo. Kwa hiyo, katika hesabu hiyo, kuko wale wenye wanafikiri kwamba ni watiwa-mafuta lakini hawako watiwa-mafuta. Kwa mufano, watu fulani wenye walikuwa wanakula mukate na kunywa divai walifikia kuacha. Wengine, kwa sababu ya magonjwa ya akili, wanaweza kuamini kwamba watatawala pamoja na Kristo mbinguni. Kwa hiyo, ni wazi kwamba, hatujue kabisa hesabu ya watiwa-mafuta wenye wangali katika dunia.

14. Biblia inasema nini juu ya hesabu ya watiwa-mafuta wenye watakuwa wangali katika dunia wakati ziki kubwa itaanza?

14 Kutakuwa watiwa-mafuta katika sehemu mbalimbali za dunia wakati Yesu atakuja kuwachukua ili waende mbinguni. Biblia inasema kwamba Yesu ‘atawatuma malaika zake pamoja na muvumo mukubwa wa tarumbeta, nao watawakusanya pamoja watu wake waliochaguliwa kutoka kwenye zile pepo ine, kutoka mwisho mumoja wa mbingu mupaka mwisho wake mwingine.’ (Mathayo 24:31) Biblia inasema pia kwamba katika siku za mwisho, kutakuwa kungali hesabu kidogo ya watiwa-mafuta katika dunia. (Ufunuo 12:17) Lakini haiseme ni watiwa-mafuta wangapi wenye watakuwa wangali katika dunia wakati ziki kubwa itaanza.

15, 16. Tunapaswa kuelewa mambo gani juu ya wale 144000 wenye Yehova amechagua?

15 Yehova anaamua wakati wa kuchagua watiwa-mafuta. (Waroma 8:28-30) Yehova alianza kuchagua watiwa-mafuta kisha kufufuliwa kwa Yesu. Inawezekana, wakati wa mitume, Wakristo wote walikuwa watiwa-mafuta. Miaka mingi kisha hapo, wengi kati ya wale wenye walikuwa wanajiita kuwa ni Wakristo, hawakumufuata kabisa Kristo. Hata hivyo, Yehova alitia mafuta hesabu kidogo ya wale wenye walikuwa Wakristo wa kweli katika miaka hiyo. Walifananishwa na ngano zenye Yesu alisema kwamba zingekomaa katikati ya magugu. (Mathayo 13:24-30) Katika siku hizi za mwisho, Yehova ameendelea kuchagua watu wenye watakuwa kati ya wale 144000.[2] (Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.) Kwa hiyo, ikiwa Mungu anaamua kuchagua watu fulani kati ya hao mbele tu mwisho ufike, tutakuwa hakika kwamba anafanya jambo lenye kufaa. (Isaya 45:9; Danieli 4:35; soma Waroma 9:11, 16.)[3] (Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.) Tunapaswa kuwa waangalifu ili tusitende kama vile wafanya-kazi wenye walimunungunikia bwana wao kwa sababu ya namna alitendea wale wenye walianza kutumika saa ya mwisho.—Soma Mathayo 20:8-15.

16 Wakristo wote wenye kuwa na tumaini la kuishi mbinguni hawafanyize ‘mutumwa mwaminifu na mwenye busara.’ (Mathayo 24:45-47) Kama vile tu wakati wa mitume, Yehova na Yesu wanatumia hesabu kidogo ya watu ili kukulisha, ao kufundisha watu wengi. Wakati wa mitume, hesabu kidogo tu ya Wakristo watiwa-mafuta ndio walitumiwa ili kuandika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Leo pia, hesabu kidogo tu ya Wakristo watiwa-mafuta ndio wenye kuwa na daraka la kutolea watu wa Mungu ‘chakula kwa wakati unaofaa.’

17. Umejifunza nini katika habari hii?

17 Tumejifunza nini katika habari hii? Yehova ameamua kupatia watu wake wengi uzima wa milele katika dunia na kupatia wale wenye watatawala pamoja na Yesu uzima huko mbinguni. Yehova anapatia zawadi watumishi wake wote, “Muyahudi” na wale “watu kumi,” na anawaomba wote waheshimie amri zilezile na waendelee kuwa waaminifu. Wote wanapaswa kuendelea kuwa wanyenyekevu. Wote wanapaswa kutumika pamoja na kuwa na umoja. Na wote wanapaswa kutumika ili kuendeleza umoja katika kutaniko. Kwa sababu mwisho unakaribia sana, sisi wote tunapaswa kuendelea kumutumikia Yehova na kumufuata Kristo tukiwa kundi moja.

^ [1] (fungu la 3) Kupatana na Zaburi 87:5, 6, wakati unaokuja, pengine Mungu atafunua majina ya wale wote wenye watatawala pamoja na Yesu mbinguni.—Waroma 8:19.

^ [2] (fungu la 15) Andiko la Matendo 2:33 linaonyesha kwamba Yesu ana daraka fulani wakati mutu anatiwa mafuta, lakini Yehova ndiye anaalika mutu huyo.

^ [3] (fungu la 15) Ili kupata habari zaidi, soma “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 5, 2007, ukurasa wa 30-31.

Ndugu na bibi yake wanazungukwa na watu wenye kupenda kuwakamata picha

Upendo ‘Haujiendeshe Bila Adabu’

Mutume Paulo aliandika hivi: ‘Upendo ni wenye ustahimilivu na wenye fazili. Upendo hauna wivu. Haujigambe, haujivune, haujiendeshe bila adabu, hautafute faida zake wenyewe.’ (1 Wakorintho 13:4, 5) ‘Tunajiendesha bila adabu’ ikiwa tunakosa heshima, tunajiendesha mubaya, na hatuonyeshe kwamba tunaheshimia wengine. Lakini, ikiwa tunapenda ndugu na dada zetu, tutafikiria namna wanaweza kujisikia mbele ya kuwaambia ao kuwatendea jambo fulani.

Tunaweza kuonyesha kwamba tunapenda wale wenye kuongoza katika tengenezo la Yehova kupitia namna tunawatendea. Wakati fulani, ndugu wenye kujulikana wanaweza kutembelea kutaniko letu ao wanaweza kuhuzuria mukusanyiko fulani pamoja na sisi. Wanaweza kuwa waangalizi wa muzunguko, Wanabeteli, ndugu wa Halmashauri ya Tawi, ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza, ao wasaidizi kwenye Baraza Lenye Kuongoza. Kwa kawaida, tunapenda kuonyesha kwamba tunawaheshimia wao na bibi zao, na ni muzuri kufanya hivyo. Hatupende kuwa kama Diotrefe; kwa sababu ya kukosa heshima, alikataa kupokea ndugu wenye walikuwa wanatembelea kutaniko lake. (3 Yohana 9, 10) Lakini hata kama tunapokea ndugu hao, je, tunaweza kufanya jambo fulani lenye kuonyesha kwamba hatuwaheshimie? Namna gani tunaweza kufanya hivyo?

Ni kweli kwamba tunafurahia kukusanyika na kuzungumuza na ndugu na dada wenye wanatutembelea, lakini tunaweza kuonyesha kwamba hatuwaheshimie ikiwa tunawaona kama watu wenye kujulikana sana. Kwa mufano, je, tutaonyesha kwamba tunawaheshimia ikiwa tunawakamata picha bila ruhusa yao ao bila wao kujua, pengine wakati wanakula ao wakati wanafanya mambo mengine? Tutawaomba watie sinyatire zao katika Biblia ao vitabu vyetu? Tutasukumana-sukumana na wengine na kutafuta tu kukamata picha pamoja nao? Kufanya hivyo kunaweza kuwa na matokeo gani juu ya wale wenye wanahuzuria mikusanyiko yetu kwa mara ya kwanza? Kwa kweli, ikiwa tunapenda ndugu na dada zetu, tutaepuka kufanya mambo kama hayo. Lakini, tunaonyesha kwamba tunawaheshimia kwa sababu tunaelewa sababu gani wanatutembelea na kwamba wanatumika sana kwa ajili yetu.

Ni nini itatusaidia tujue namna ya kutendea ndugu na dada zetu? Kwanza, tukumbuke kwamba ni Yehova tu ndiye anapaswa kupewa utukufu. (Ufunuo 4:11) Pili, tuelewe kwamba hata kama tunapaswa kuheshimia ndugu hao na bibi zao, tunapaswa kuepuka kuwaona kama watu wenye kujulikana sana. Wanapenda tuwatendee kama ndugu na dada wengine. (Mathayo 23:8) Tatu, tukumbuke mambo yenye Yesu alifundisha. Alisema hivi: ‘Kwa hiyo, mambo yote munayotaka watu wawatendee ninyi, lazima muwatendee wao pia vivyo hivyo.’ (Mathayo 7:12) Ikiwa tunakumbuka mambo hayo, tutaonyesha upendo na ‘hatutajiendesha bila adabu.’

MAANA YA MANENO FULANI

  • Watu kumi “wanaenda pamoja” na Muyahudi: Kondoo wengine wanamutumikia Yehova pamoja na watiwa-mafuta lakini hawawaone kuwa viongozi wao ao kuwasifu-sifu na kuwaheshimia kupita kiasi. Lakini, wanawapenda na kuwaheshimu, na wanawatendea kama ndugu na dada zao

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine