Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • kr sura 20 uku. 209-219
  • Kazi ya Kutolea Ndugu Misaada Wakati wa Magumu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kazi ya Kutolea Ndugu Misaada Wakati wa Magumu
  • Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sababu Gani Kazi Hiyo Ni Utumishi Mutakatifu
  • Makusudi ya Kazi ya Kutolea Ndugu Misaada Wakati wa Magumu
  • Kazi ya Kutolea Ndugu Misaada Inaleta Faida Zenye Kudumu
  • Unaweza pia Kusaidia?
  • Tunaweza Kusaidia Namna Gani Kisha Musiba?
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
  • Mashahidi wa Yehova Wanasaidiaka Wale Wenye Wanafikiwa na Misiba?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
  • Kuunga Ufalme Mukono—Kazi ya Kujenga Mahali pa Ibada na Kutolea Ndugu Misaada Wakati wa Magumu
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Kutolea Musaada Wale Wenye Walipatwa na Musiba
    Namna Michango Yako Inatumiwa
Ona Habari Zaidi
Ufalme wa Mungu Unatawala!
kr sura 20 uku. 209-219

SURA YA 20

Kazi ya Kutolea Ndugu Misaada Wakati wa Magumu

WAZO KUBWA KATIKA SURA HII

Wakristo wanaonyesha upendo wao wakati wa magumu

1, 2. (a) Wakristo wa Yudea walipambana na magumu gani? (b) Ni tendo gani la upendo Wakristo Wayahudi walijionea?

NI MWAKA wa 46 hivi wakati wa mitume. Muji wa Yudea unashambuliwa na njaa kali sana. Kwa sababu hakuna chakula kingi katika muji, chakula kinapanda bei sana. Kwa hiyo, Wakristo Wayahudi hawana uwezo wa kujiuzia chakula. Wana njaa, wanakosewa kabisa chakula. Lakini, hivi karibuni watajionea ulinzi wa mukono wa Yehova. Kwa wakati wao, hakuna wanafunzi wengine wa Kristo ambao walikuwa wamekwisha kujionea ulinzi kama huo. Ni jambo gani litafanyika?

2 Wakristo Wayahudi na wa Mataifa ambao walikuwa wanaishi katika muji wa Antiokia na Siria, walifanya nini wakati walisikia kwamba ndugu zao Wayahudi wa Yerusalemu na Yudea wanateseka? Walikusanya feza na kuwatumia. Pia walichagua kati yao ndugu wawili wenye kutumainiwa, Barnaba na Sauli ili wapeleke musaada huo kwa wazee wa kutaniko la Yerusalemu. (Soma Matendo 11:27-30; 12:25.) Fikiria namna ndugu wa Yudea waliguswa moyo kwa sababu ya tendo hilo la upendo ambalo ndugu zao wa Antiokia waliwaonyesha!

3. (a) Namna gani watu wa Mungu leo, wanaendelea kufuata mufano wa Wakristo wa Antiokia? Toa mufano. (Soma pia kisanduku “Programu Yetu Kubwa Zaidi ya Kwanza ya Kutolea Ndugu Misaada Katika Siku Zetu.”) (b) Ni maulizo gani tutazungumuzia katika sura hii?

3 Jambo hilo ambalo lilifanyika siku za mitume, ndilo tukio la kwanza kuandikwa ambalo linaonyesha namna Wakristo ambao wanaishi katika sehemu fulani ya dunia wanatumia Wakristo wengine misaada wakati wa magumu. Leo, tunafuata mufano huo wa ndugu zetu wa Antiokia. Wakati tunajulishwa kwamba ndugu zetu katika inchi fulani wamepatwa na magumu ao musiba, tunawatolea musaada.a Ili kuelewa namna misaada ambayo tunajikaza kutoa wakati wa magumu ni sehemu ya utumishi wetu mwengine ambao tunamutolea Mungu, acha tuchunguze maulizo matatu kuhusu kazi ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu. Sababu gani tunaona kazi hiyo kuwa ni utumishi ambao tunamutolea Mungu? Kazi yetu ya kutoa misaada iko na makusudi gani? Inaleta faida gani?

Sababu Gani Kazi Hiyo Ni Utumishi Mutakatifu

4. Mutume Paulo aliwaambia Wakorintho nini juu ya huduma ya Kikristo?

4 Katika barua yake ya pili kwa Wakorintho, mutume Paulo alifasiria kwamba utumishi wa Wakristo uko na sehemu mbili za maana. Hata ikiwa ni Wakristo watiwa-mafuta ndio waliandikiwa barua hiyo, maneno ya mutume Paulo yanawahusu pia “kondoo wengine.” Yoh. 10:16) Sehemu moja ya kazi yetu ni “huduma [utumishi] ya upatanisho,” ( ni kusema, kazi yetu ya kuhubiri na kufundisha. (2 Kor. 5:18-20; 1 Tim. 2:3-6) Sehemu ingine ni kazi ambayo tunatimiza kwa faida ya ndugu zetu. Mutume Paulo anazungumuzia sehemu hiyo kuwa “huduma [kazi]” ya kutoa misaada. (2 Kor. 8:4) Katika Kigiriki neno “huduma” ambalo linapatikana katika maneno “huduma ya upatanisho” na ‘huduma ya kutoa misaada’, ni di·a·ko·niʹ. Sababu gani matumizi ya neno hilo ni ya maana?

5. Sababu gani ni jambo la maana kwamba mutume Paulo aliita kazi ya kutolea ndugu misaada kuwa ni huduma?

5 Kwa kutumia neno lilelile la Kigiriki kuhusu kazi hizo mbili, mutume Paulo anaonyesha kwamba kazi ya kutolea ndugu misaada inapatana na sehemu zingine za huduma ao kazi ambazo zilikuwa zinatimizwa na kutaniko la Kikristo. Mbele ya kuzungumuzia jambo hilo alikuwa amekwisha kusema hivi: “Kuna huduma za namna mbalimbali, na bado kuna Bwana yuleyule; na kuna utendaji wa namna mbalimbali; . . . Lakini ni roho ileile moja inayofanya utendaji huu wote.” (1 Kor. 12:4-6, 11) Kwa kweli, mutume Paulo alionyesha kwamba kuna upatano kati ya huduma mbalimbali ambao ulitimizwa katika kutaniko na ‘utumishi mutakatifu.’b (Rom. 12:1, 6-8) Kwa hiyo, haitushangaze ikiwa Paulo aliona kwamba ni jambo la maana kutumia sehemu ya wakati wake “ili kuwahudumia watakatifu”!—Rom. 15:25, 26.

6. (a) Kama vile mutume Paulo alifasiria, sababu gani kazi ya kutolea ndugu misaada ni sehemu ya ibada yetu? (b) Fasiria namna gani kazi yetu ya kutolea ndugu misaada inafanyika leo. (Soma kisanduku “Wakati Musiba Unatokea!” ukurasa wa 214.)

6 Mutume Paulo aliwasaidia Wakorintho waelewe kwamba kazi ya kutolea ndugu misaada ni sehemu ya ibada yao kwa Yehova na vilevile ni sehemu ya huduma yao kwa Yehova. Fikiria sababu ya mutume Paulo: Ikiwa Wakristo walitoa misaada ni kwa sababu walikuwa wenye ‘kujitiisha kwenye habari njema juu ya Kristo.’ (2 Kor. 9:13) Kwa hiyo, Wakristo wanasaidia ndugu zao kwa sababu wanataka kutumikisha mafundisho ya Kristo katika maisha yao. Mutume Paulo anasema kwamba matendo ya upendo ambayo Wakristo wanaonyesha ndugu zao, ni ‘fazili nyingi zaidi zisizostahiliwa za Mungu.’ (2 Cor. 9:14; 1 Pet. 4:10) Ndiyo sababu, gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 2, 1975, lilizungumuzia kazi ya kusaidia ndugu zetu wakati wa magumu; lilisema waziwazi hivi: “Tunapaswa kuwa na uhakika kwamba Yehova na Mwana wake Yesu Kristo wanaona kazi hiyo kuwa ya maana sana.” Bila shaka, kazi ya kusaidia ndugu wakati wa magumu ao misiba ni sehemu ya maana sana ya utumishi wetu mutakatifu.​—Rom. 12:1, 7; 2 Kor. 8:7; Ebr. 13:16.

Makusudi ya Kazi ya Kutolea Ndugu Misaada Wakati wa Magumu

7, 8. Kusudi letu la kwanza la kutolea ndugu misaada ni nini? Fasiria.

7 Kazi yetu ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu ina makusudi gani? Mutume Paulo alijibia ulizo hilo katika barua yake ya pili kwa Wakorintho. (Soma 2 Wakorintho 9:11-15.) Katika andiko hilo, mutume Paulo anakazia makusudi matatu ambayo yanatuchochea kuunga mukono ‘huduma ya utumishi wa [ao kwa ajili ya] watu wote,’ ni kusema, kazi ya kutoa misaada. Acha tuzungumuzie makusudi hayo.

8 Kusudi la Kwanza: Kazi yetu ya kutoa misaada inamuletea Yehova utukufu. Katika mistari tano ya andiko ambayo tulizungumuzia hapo juu, mutume Paulo anavutia mara nyingi uangalifu wa ndugu zake kwa Yehova Mungu. Paulo anawakumbusha kuhusu “wonyesho wa shukrani kwa Mungu” na kuhusu “maonyesho mengi ya shukrani kwa Mungu.” (Mustari wa 11, na 12) Anaonyesha kwamba kazi hiyo ya kutoa misaada inachochea Wakristo ‘kumutukuza Mungu’ na kusifu ‘fazili nyingi zaidi zisizostahiliwa za Mungu.’ (Mustari wa 13, na 14) Mutume Paulo anamalizia mazungumuzo yake juu ya kazi ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu ao misiba kwa kusema hivi: “Mungu apewe shukrani.”—Mustari wa 15; 1 Pet. 4:11.

9. Kazi ya kutolea ndugu misaada inaweza namna gani kubadilisha mawazo mabaya ya watu? Toa mufano.

9 Kama mutume Paulo, leo watumishi wa Mungu wanaona kazi ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu kuwa nafasi nzuri ya kumuletea Yehova utukufu, na ya kupamba mafundisho yake. (1 Kor. 10:31; Tito 2:10) Kwa kweli, kazi hiyo ya kutolea ndugu misaada, mara nyingi inasaidia sana kuondoa mawazo mabaya ambayo watu fulani walikuwa nayo juu ya Yehova na juu ya Mashahidi wake. Tuchukue mufano huu: Mwanamuke fulani ambaye alikuwa anaishi katika eneo ambalo liliharibiwa na upepo mukali, alikuwa ameandika hivi kwenye mulango wake: “Mashahidi wa Yehova hawakaribishwe hapa.” Kisha siku fulani aliona ndugu upande mwingine wa barabara wanatengeneza nyumba fulani ambayo ilikuwa imeharibiwa. Kwa muda wa siku fulani, aliona namna wafanyakazi hao walikuwa wanatumika kwa urafiki sana, kisha akaamua kuenda kuwauliza wao ni nani. Wakati alijulishwa kwamba wao ni Mashahidi wa Yehova, alishangaa sana na kusema hivi: “Nilikuwa na maoni mabaya juu yenu.” Matokeo yalikuwa nini? Alifuta maandishi ambayo aliandika kwenye mulango wake.

10, 11. (a) Ni mifano gani inaonyesha kwamba tunafikia kusudi letu la pili la kazi yetu ya kutolea ndugu misaada? (b) Ni kichapo gani kinasaidia wafanyakazi ambao wanatolea ndugu misaada? (Soma kisanduku “Chombo Kingine kwa Ajili ya Wafanyakazi Ambao Wanatolea Ndugu Misaada.”)

10 Kusudi la Pili: Tunagawia ndugu zetu mahitaji yao kwa uwingi. (2 Kor. 9:12a) Tuko tayari kutimiza mahitaji ya ndugu na dada zetu ambao wanapatwa na magumu ili kuwatolea kitulizo. Sababu gani? Kwa sababu ndugu na dada katika kutaniko la Kikristo wanafanyiza ‘mwili mumoja,’ na “kiungo kimoja kikiumia [ao kuteswa], vile viungo vingine vyote vinaumia.” (1 Kor. 12:20, 26) Kwa hiyo, upendo wa kindugu na huruma vinawachochea ndugu na dada wengi leo kubadilisha programu zao bila kusita, kukusanya vyombo vyao vya kazi, na kuenda mahali ambapo kumefanyika musiba ili kutolea ndugu zao musaada. (Yak. 2:15, 16) Kwa mufano, katika mwaka wa 2011 kisha inchi ya Japani kupigwa na upepo mukali unaoitwa tsunami, Beteli ya Amerika ilituma barua kwa Halmashauri za Ujenzi wa Eneo za Amerika, ili kuomba ikiwa ndugu ambao wana ufundi wa kujenga wanaweza kuenda huko Japani kusaidia kujenga upya Majumba ya Ufalme. Matokeo yalikuwa namna gani? Kwa majuma kidogo tu, ndugu na dada karibu 600 wenye kujitolea walijaza fomu ili kuenda kusaidia. Walikubali pia kujilipia ndege wao wenyewe ili kuenda Japani! Beteli ya Amerika ilisema hivi: “Kujitoa kwao kulitutia moyo sana.” Wakati ndugu fulani wa Japani alimuuliza mumoja wa wafanyakazi hao wenye kujipendea sababu gani alikuja Japani kusaidia, alimujibu hivi: “Ndugu zetu katika Japani ni sehemu ya ‘mwili wetu.’ Taabu yao ni taabu yetu, mateso yao ni mateso yetu.” Wakati mwingine, upendo wa kujitoa kwa ajili ya wengine umefanya ndugu hao wenye kujitolea watie maisha yao katika hatari kwa ajili ya kusaidia ndugu zao.c​—1 Yoh. 3:16.

Dada, katika inchi ya Uswisi, anatayarishia ndugu wengine misaada katika mwaka wa 1946

Mwaka wa 1946, Uswisi

PROGRAMU YETU KUBWA ZAIDI YA KWANZA YA KUTOLEA NDUGU MISAADA KATIKA SIKU ZETU

KATIKA Mwezi wa 9, 1945, miezi kidogo kisha Vita ya Pili ya Ulimwengu katika Ulaya, Ndugu Knorr alitangaza mwanzo wa kampanye kubwa ya kutuma “musaada wa vitu vya kimwili kwa ndugu ambao walipatwa na magumu katika Ulaya ya kati.”

Kwa majuma kidogo, Mashahidi wa Kanada, Amerika, na sehemu zingine za dunia walianza kukusanya nguo na kuzifunga vizuri katika mifuko na pia walikusanya chakula. Kuanzia Mwezi wa 1, 1946 vitu hivyo vilitumwa kwa ndugu wa Autriche, Bulgaria, Chekoslovakia, Danemark, Finlande, Hollande, Hongrie, Italia, Norvège, Pologne, Rumania, Ubelgiji, Uchina, Ufaransa, Ufilipino, Ujerumani, Ugiriki, Uingereza.

Programu hiyo ya kutolea ndugu misaada haikuwa ya mwaka huo tu. Misaada iliendelea kutumwa kwa miaka miwili na nusu! Wakati huo ndugu na dada 85000 hivi, walitumia ndugu na dada zao ambao walikuwa katika inchi ambazo ziliharibiwa na vita, kilo zaidi ya 300000 ya chakula, kilo zaidi ya 450000 ya nguo, na zaidi ya viato 124000. Mwezi wa 8, 1948, programu hiyo kubwa zaidi ya kutolea ndugu misaada ilifikia mwisho. Gazeti Munara wa Mulinzi la 1949 lilisema hivi: “Programu hiyo ilikuwa alama ya upendo kabisa kati ya ndugu. Tunajua kwamba ndugu walifanya hayo yote kwa utukufu wa Bwana. Wanajua kwamba musaada huo wa vitu vya kimwili utawasaidia wengine waendeleze ibada ya kweli. Kwa hiyo, wanaona hilo kuwa pendeleo kubwa la kuweza kutumikia ndugu zao katika njia hiyo.” Programu hiyo ya kutolea ndugu misaada ilimuletea Yehova sifa, ilitolea ndugu kitulizo, na ilifanya umoja ambao uko kati ya ndugu duniani pote uwe wenye nguvu zaidi.

11 Watu ambao si Mashahidi wanaonyesha pia kwamba wanasamini kazi yetu ya kusaidia ndugu zetu wakati wa magumu. Kwa mufano, katika mwaka wa 2013, muji wa Arkansas, Amerika, ulipatwa na musiba. Kisha gazeti fulani liliandika namna Mashahidi wa Yehova wenye kujitolea walikuja haraka ili kusaidia. Liliandika hivi: “Mashahidi wa Yehova wanapanga mambo vizuri kuhusu wafanyakazi wenye kujitolea ili waweze kusaidia ndugu zao ambao walipatwa na musiba. Na jambo hilo linawasaidia wafanye kazi kwa ufundi sana na kwa matokeo mazuri.” Kwa kweli, kama vile mutume Paulo aliandika, tunagawia ndugu mahitaji yao kwa uwingi.

12-14. (a) Sababu gani kufikia kusudi letu la tatu la kutolea ndugu misaada ni jambo la maana sana? (b) Ndugu na dada walisema nini ili kuonyesha kwamba kuendelea na programu ya kiroho ni jambo la maana sana?

12 Kusudi la Tatu: Tunasaidia ndugu ambao walipatwa na magumu kurudilia programu yao ya kiroho. Sababu gani jambo hilo ni la maana? Mutume Paulo anasema kwamba wale ambao wanatolewa musaada watachochewa kumutolea Mungu “maonyesho mengi ya shukrani.” (2 Kor. 9:12b) Unafikiri kuna njia nzuri zaidi ambayo watu wenye kuteseka wanaweza kutumia ili kuonyesha shukrani zao kwa Yehova, isipokuwa kwa kurudilia haraka iwezekanavyo programu yao ya kawaida ya kiroho? (Flp. 1:10) Katika mwaka wa 1945, gazeti Munara wa Mulinzi lilisema hivi: “Mutume Paulo alikubali . . . kukusanywa kwa michango kwa sababu ilikuwa inasaidia . . . ndugu Wakristo kupata misaada fulani ya kimwili na hilo liliwasaidia kufanya kazi ya kutoa ushahidi juu ya Yehova bila magumu na kwa bidii kabisa.” Kusudi letu ni hilohilo pia leo. Wakati ndugu wanarudilia kazi ya kuhubiri, wanatia moyo jirani zao wenye kuteseka, lakini wao pia wanatiwa nguvu.​—Soma 2 Wakorintho 1:3, 4.

13 Acha tuchunguze maelezo fulani ya ndugu na dada ambao walipokea musaada wakati walikuwa katika uhitaji mukubwa. Walianza tena kuhubiri, na wakatiwa nguvu kwa kufanya hivyo. Ndugu mumoja alisema hivi: “Ilikuwa baraka kabisa kwa familia yetu kuanza tena kuhubiri. Mahubiri ilitusaidia sana, kwa kuwa wakati tuliwatia wengine moyo tulisahau magumu yetu kwa muda fulani.” Dada mwengine alisema hivi: “Kukazia sana kazi ya kiroho kulinisaidia nisifikirie sana vitu mbalimbali ambavyo viliharibika. Mahubiri ilinifanya nijisikie kuwa salama.” Dada mwengine alisema hivi: “Kulikuwa na mambo mengi ambayo hatukujua tufanye nini, lakini kazi ya kuhubiri ilitolea familia yangu muongozo. Kuzungumuza na wengine juu ya tumaini letu la ulimwengu mupya kulitia nguvu tumaini letu la kwamba vitu vyote vitakuwa vipya.”

14 Kuhuzuria mikutano ni utendaji ao kazi ingine ya kiroho ambayo ndugu ambao wanapatwa na musiba wanapaswa kurudilia haraka iwezekanavyo. Tuchukue mufano wa dada Kiyoko, ambaye anakaribia miaka 60. Upepo wa tsunami ulimufanya apoteze karibu kila kitu, alibaki tu na mavazi na pia viato ambavyo alikuwa anavaa wakati huo. Hakujua namna angeendelea kuishi. Kisha muzee wa kutaniko akamuambia kwamba wataanza kufanyia mikutano yao ya kawaida katika motokari yake. Dada Kiyoko alisema hivi: “Muzee huyo na bibi yake, dada mwengine na mimi tulikaa katika motokari ao motokaa. Mukutano ulikuwa mwepesi, lakini kama tu muujiza, mawazo ya tsunami yaliondoka katika akili yangu. Nilisikia ninakuwa na amani ya akili. Mukutano huo ulinisaidia kuona nguvu ya kuwa pamoja na Wakristo wengine.” Dada mwengine alizungumuzia mikutano ambayo alihuzuria kisha musiba kutokea. Alisema hivi: “Mikutano hiyo ilinisaidia kuvumilia!”​—Rom. 1:11, 12; 12:12.

Kazi ya Kutolea Ndugu Misaada Inaleta Faida Zenye Kudumu

15, 16. (a) Wakristo wa Korintho na wa mahali pengine wangepata faida gani kwa kuunga mukono kazi ya kutolea ndugu misaada? (b) Namna gani sisi pia leo tunapata faida ya kazi ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu?

15 Wakati mutume Paulo alikuwa anazungumuzia huduma ao kazi ya kutoa misaada, alifasiria pia Wakorintho faida ambazo wao na Wakristo wengine wangepata kwa kufanya kazi hiyo. Aliandika hivi: ‘Kupitia dua kwa ajili yenu wanatamani [Wakristo Wayahudi katika Yerusalemu ambao walipokea misaada] kuwaona ninyi kwa sababu ya fazili nyingi zaidi zisizostahiliwa za Mungu juu yenu.’ (2 Kor. 9:14) Ndio, ukarimu wa Wakorintho uliwasukuma Wakristo Wayahudi kusali kwa ajili ya ndugu zao katika Korintho, na Wakristo wa Mataifa pia, na hilo lingefanya wawe na upendo mwingi kuwaelekea.

16 Ili kuonyesha faida ambazo zinatokana na kazi ya kutolea ndugu misaada leo, gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 12, 1945, lilizungumuzia maneno ya mutume Paulo. Lilisema hivi: “Wakati kikundi fulani cha watu wa Mungu ambao wamejitoa kwake kinatoa michango ili kusaidia kikundi kingine ambacho kina magumu, bila shaka, hilo linatia nguvu umoja wao!” Ndugu ambao wanafanya kazi ya kutoa misaada wamejionea jambo hilo. Muzee fulani wa kutaniko ambaye alisaidia katika kazi ya kutolea ndugu misaada wakati maji yalijaa na kuharibu vitu vyao, alisema hivi: “Kufanya kazi ya kutolea ndugu misaada kulinifanya niwakaribie zaidi kuliko mbele.” Dada mumoja ambaye alishukuru sana wakati alipokea musaada alisema hivi: “Undugu wetu ndio jambo pekee ambalo tuko nalo wakati tunaendelea kungojea Paradiso hapa duniani.”​—Soma Methali 17:17.

17. (a) Namna gani maneno ya andiko la Isaya 41:13 yanapatana na kazi ya kutolea ndugu misaada? (b) Taja mifano tatu yenye kuonyesha namna kazi ya kutolea ndugu misaada inamuheshimisha Yehova na inafanya umoja wetu uwe na nguvu. (Soma pia kisanduku “Wafanyakazi Kutoka Katika Dunia Yote Wanajitolea ili Kutoa Misaada.”)

17 Wakati ndugu ambao wanafanya kazi ya kutoa misaada wanafika mahali ambapo kulitokea musiba, ndugu ambao wamepatwa na musiba wanajionea katika njia ya kipekee ukweli wa ahadi hii ya Mungu: ‘Mimi, Yehova Mungu wako, ninaushika mukono wako wa kuume, Mwenye kukuambia, Usiogope. Mimi mwenyewe nitakusaidia.’ (Isa. 41:13) Dada mumoja ambaye aliokoka musiba, alisema hivi: “Wakati niliona uharibifu ambao uliletwa na musiba, sikuwa tena na tumaini, lakini Yehova alinyoosha mukono wake. Musaada ambao ndugu walinitolea ulikuwa mukubwa sana.” Kisha musiba kuharibu eneo fulani, wazee wawili wa mahali hapo waliandika hivi kwa jina la makutaniko yao: “Tetemeko la udongo lilileta mateso makubwa, lakini tulijionea musaada wa Yehova kupitia ndugu zetu. Tulikuwa tumesoma juu ya kazi ya kutolea ndugu misaada, lakini sasa tumejionea na macho yetu namna kazi hiyo inafanywa.”

Peter Johnson anatumika kwa ajili ya matayarisho ya ujenzi wa majengo ya kiteokrasi

ILIMUSAIDIA KUTUMIA MAISHA YAKE VIZURI

KUFANYA kazi ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu kumekuwa na matokeo gani juu ya vijana? Acha tuzungumuzie kijana anayeitwa Peter Johnson, ambaye alifanya kazi hiyo kwa mara ya kwanza wakati alikuwa na miaka 18. Anasema hivi: “Kuona shukrani za ndugu na kujionea furaha ya kutoa, kulinigusa moyo sana. Kazi hiyo ilichochea sana tamaa yangu ya kutumia maisha yangu ili kumutumikia Yehova kadiri inawezekana.” Kisha, Peter alianza kazi ya upainia. Alitumikia pia kwenye Beteli na kisha alianza kutumika katika Halmashauri ya Ujenzi wa Eneo. Ndugu Peter anasema hivi leo: “Kazi ambayo nilifanya ya kutolea ndugu misaada katika mwaka wa 1974 ilinisaidia kutumia maisha yangu vizuri.” Wewe ni kijana? Unaweza kufuata mufano wa Peter? Nani anajua, pengine kazi ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu inaweza kukusaidia utumie maisha yako vizuri katika utumishi wa Yehova!

Unaweza pia Kusaidia?

18. Unapaswa kufanya nini ikiwa unapenda kuonja furaha ya kazi ya kutolea ndugu misaada? (Soma pia kisanduku “Ilimusaidia Kutumia Maisha Yake Vizuri.”)

18 Ungependa pia kuonja furaha ya kazi ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu? Ikiwa ndiyo, kumbuka kwamba wafanyakazi hao wanachaguliwa katikati ya ndugu na dada ambao wanajenga Majumba ya Ufalme. Kwa hiyo, uwaambie wazee wa kutaniko lako kwamba unapenda kujaza fomu. Muzee fulani mwenye uzoefu katika kazi ya kutolea ndugu misaada alitoa shauri hili: “Mbele ya kuenda katika eneo ili kusaidia, ngojea mupaka wakati utaitwa na Halmashauri ya Misaada ya Wakati wa Misiba.” Kwa kufanya hivyo, kazi yetu itafanywa kwa utaratibu.

19. Namna gani wafanyakazi wa kutolea ndugu misaada wanasaidia sana kuonyesha kwamba sisi ni wanafunzi wa kweli wa Kristo?

19 Kwa kweli, kufanya kazi ya kutolea ndugu misaada ni njia ya maana sana ambayo kupitia hiyo tunaonyesha kwamba tunatii amri ya Kristo ambayo inatuomba kuwa na “upendo kati [yetu] wenyewe.” Kwa kuwa na upendo kama huo, tunaonyesha kwamba sisi ni wanafunzi wa kweli wa Kristo. (Yoh. 13:34, 35) Sisi ni wenye kubarikiwa kabisa kwa sababu tuko na wafanyakazi wengi sana wenye kujipendea ambao wanamuletea Yehova utukufu wakati wanatoa musaada kwa wale ambao wanaunga Ufalme wa Mungu mukono kwa uaminifu!

a Sura hii inazungumuzia namna tunajikaza ili kutolea ndugu na dada misaada wakati wa magumu. Lakini, mara nyingi, tunatolea pia misaada watu wasio Mashahidi.​—Gal. 6:10.

b Mutume Paulo alitumia pia neno diaʹkonos (muhuduma) ili kuzungumuzia “watumishi wa huduma.”​—1 Tim.3:12.

c Soma habari “Kusaidia Familia Yetu ya Waamini Katika Bosnia,” katika gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 11, 1994, ukurasa 23-27.

Ufalme Ni Jambo la Kweli Kwako?

  • Namna gani tunajua kwamba kazi ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu ni sehemu ya utumishi wetu mutakatifu kwa Yehova?

  • Ni makusudi gani matatu ambayo yanatuchochea kufanya kazi ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu?

  • Kazi ya kutolea ndugu misaada inaleta faida gani zenye kudumu?

  • Namna gani kazi ya kutolea ndugu misaada wakati wa magumu inapatana na amri ya Yesu ambayo inapatikana katika andiko la Yohana 13:34?

WAFANYAKAZI KUTOKA KATIKA DUNIA YOTE WANAJITOLEA ILI KUTOA MISAADA

AFRIKA YA KATI NA YA MASHARIKI

Katika mwaka wa 1994, watu 800000 hivi ao zaidi waliuawa katika mauaji makubwa ya kikabila. Mauaji hayo makubwa yalileta misukosuko katika inchi zingine za Afrika ya Kati, na kufanya kuwe na makambi zenye kujaa wakimbizi katika inchi hizo. Ili kusaidia ndugu zao wenye kuteswa, Mashahidi wa Yehova katika Ubelgiji, Ufaransa, na Uswisi walituma kwa njia ya ndege toni 300 hivi za nguo, dawa, hema, chakula na mambo mengine. Kwa muda wa majuma kidogo, ndugu walipata vitu ambavyo viliwasaidia.

Pia katika Afrika, kikundi cha waganga na wasaidizi wao (infirmièrs) Mashahidi kutoka Ufaransa walitolea ndugu zetu misaada; ndugu zetu walikuwa wenye kuteseka sana, kwa sababu ya vita, njaa, na magonjwa. Kwa miaka mbili tu ambayo imepita ndugu hao walisaidia ao kutunza zaidi ya watu 10000. Yehova alisifiwa kupitia kazi yao na pia tengenezo lake. Dada mumoja kati ya wasaidizi hao alisema hivi: “Wakati tunafika katika eneo fulani ili kusaidia ndugu na dada, watu wanasema kwa heshima ‘Hawa ni Mashahidi wa Yehova. Wamekuja kusaidia ndugu zao.’” Kisha kupata musaada wa waganga, dada mumoja alisema kwa furaha: “Asante dada yangu. Asante Yehova!”

Wakati fulani, kazi ya kutolea ndugu misaada inaweza pia kuwa ya lazima wakati aksida zinatokea. Katika mwaka wa 2012, Mashahidi 13 walikufa katika aksida ya barabara huko Nigeria, wote walikuwa washiriki wa kutaniko fulani ndogo. Katika aksida hiyo wengine 54 waliumia vikali sana. Halmashauri ya kutoa misaada ilichukua mipango ya kutumika usiku na muchana ili kusaidia kila mutu aliyepatwa na aksida hiyo. Wakati mwanamuke mumoja mugonjwa kwenye hospitali aliona namna ndugu na dada ambao waliumia walisaidiwa, aliita pastere wake kwenye telefone, akamuambia: “Hakuna hata mutu mumoja wa kanisa letu ambaye amenitembelea. Kuja hapa kwenye hospitali uone upendo wa kweli kati ya Mashahidi wa Yehova!”

Hata ikiwa ndugu zetu wapendwa katika kutaniko hilo ndogo waliumizwa sana na jambo hilo la kufiwa, walifarijiwa na matendo ya upendo kutoka kwa ndugu zao. Zaidi ya hilo, wakati ndugu ambao walipatwa na musiba waliona namna ndugu zao wenye kutoa misaada waliwahangaikia kwa upendo mwingi, wengi katika kutaniko walichochewa kuongeza utendaji wao katika mahubiri. Mbele ya aksida kutaniko hilo lilikuwa na wahubiri 35. Kisha mwaka moja wahubiri waliongezeka na kufikia 60.

AUSTRALIA

Katika mwaka wa 2013, sehemu fulani za muji wa Queensland ulio pembeni ya bahari zilifunikwa na maji, na Mashahidi wa Yehova 70 walibaki bila makao. Ndugu Mark na bibi yake Rhonda na binti yao waliacha nyumba yao ambayo ilizama katika maji na wakaenda kubaki mahali fulani ambako watu walipelekwa. Mahali hapo palijaa watu sana. Dada Rhonda alisema hivi: “Watu walikuwa wengi sana na wenye kusimama, haikuwezekana kukaa.” Sauti kubwa za helikoptere ambazo zilikuwa zinatua na kuondoka zilifanya watu ambao walikuwa mahali hapo wawe katika wasiwasi zaidi. Kwa sababu ya woga dada alimuuliza bwana yake, “Tutafanya nini sasa?” Ndugu Mark alimuomba Yehova kwa bidii, awasaidie. Dada Rhonda alisema tena hivi: “Kisha dakika 30 hivi motokari ilifika mahali hapo na ndugu watatu walishuka kutoka ndani. Wakati tulionana, walituambia hivi: ‘Tumekuja kuwakamata. Mutaenda kukaa kwa ndugu fulani.’” Dada Rhonda anaendelea kusema: “Ni vigumu kufasiria namna tulijisikia wakati huo kwa kuona namna tengenezo la Yehova lilituhangaikia kwa upendo.”

Wafanyakazi wenye kujitolea zaidi ya 250 walienda haraka katika eneo hilo la musiba ili kusaidia ndugu zao. Muzee mumoja alisema hivi: “Kikundi fulani cha Mashahidi wa Yehova kilifika, sijue kilitokea wapi. Walitumika kwa bidii sana ili kuondoa uchafu ambao ulijaa katika nyumba yetu. Mimi na bibi yangu hatutasahau hata kidogo namna ndugu hao walitusaidia.”

BRAZILI

Katika mwaka wa 2008, mvua kubwa ilifanya udongo wa mulima uporomoke. Matope yalijaa eneo lote la Santa Catarina na kulazimisha watu 80000 hivi kuacha nyumba zao. Mukaaji mumoja alisema hivi: “Ilikuwa kama upepo mukali wa tsunami, ambao ulikuja na matope na miti.” Ndugu fulani walijipatia makao katika Jumba la Mikusanyiko. Ndugu Márcio ambaye anachunga jumba hilo, alisema hivi: “Ndugu walikimbia na nguo tu ambazo walikuwa wanavaa wakati huo, wote walikuwa wenye kujaa matope.” Dada mumoja alisema hivi: “Nyumba yetu ilibomoka. Iliumiza sana kuona namna ilipotea kwa dakika tu, lakini sitasahau hata kidogo namna ndugu na dada zetu walitufariji. Tulionyeshwa upendo kwa njia nyingi! Mambo ambayo yalitupata yalinifundisha kwamba ni jambo la hekima kabisa kushikilia sana mambo ya kiroho.”

Mashahidi wa Yehova wanatayarisha na kugawanya misaada iliyotolewa na ndugu kwa ajili ya ndugu wa Brazili

Mwaka wa 2009, katika Santa Catarina, Brazili, Jumba la Mikusanyiko linajaa vitu na limekuwa mahali pa kutolea ndugu misaada wakati wa musiba

Matope hayo yameharibu miji yote ambayo inapatikana kwenye miteremuko ya mulima karibu na muji wa Rio de Janeiro. Ili kupambana vizuri zaidi na musiba huo ambao unatokea kwa ukawaida, ndugu waliunda Halmashauri ya Misaada Wakati wa Musiba. Wakati maporomoko hayo ya matope yanatokea, ndugu wa eneo hilo wanajulisha mara moja halmashauri hiyo. Kwa haraka, wafanyakazi wa kujitolea wanafika katika motokari ambazo zinabandikwa alama yenye maandishi haya, “Mashahidi wa Yehova—Misaada kwa Ajili ya Watu Wenye Kuwa Katika Magumu.” Wafanyakazi hao wenye kujitolea walikuwa na vifaa vyote vya kazi, na kila mutu alijua mbele ya wakati kazi ambayo atafanya. Walivaa majaketi ambayo yaliwatambulisha kuwa Mashahidi wa Yehova. Wao pamoja na ndugu wa Halmashauri za Uhusiano na Hospitali, walisaidia ndugu na dada ambao waliumia. Wafanyakazi wenye kutolea ndugu misaada walileta chakula, maji, dawa, nguo, na dawa za kusafisha nyumba. Kuondoa matope katika nyumba za ndugu ni kazi kubwa sana. Hivi karibuni, wakati matope yalijaa, iliomba wafanyakazi 60 ili kuondoa camion 4 zenye kujaa matope katika nyumba moja tu!

KUJITAYARISHA KWA AJILI YA MISIBA

Baraza Lenye Kuongoza limetoa maagizo kwa tawi zote katika dunia kwamba wazee wa makutaniko na waangalizi wenye kusafiri wapewe miongozo kuhusu namna ya kujitayarisha na kutenda wakati misiba inatokea. Kwa mufano,hatambele ya musiba kutokea, wazee wanapaswa kuhakikisha kwambawana adresi za sasa ao namba za telefone za ndugu na dada katika kutaniko.

WAKATI MUSIBA UNATOKEA!

  1. Muzee wa kutaniko anataka kujua hali ya familia ya kutaniko lao

    Wazee wa kutaniko wanapaswa kujua hali ya wahubiri wote

  2. Wazee wanapaswa kumujulisha muratibu wa baraza la wazee hali ya wahubiri wote

  3. Kupashana habari kati ya waratibu wa makutaniko, waangalizi wenye kusafiri, na wandugu wengine wenye madaraka, na biro ya tawi

    Waratibu wanapaswa kuwajulisha waangalizi wenye kusafiri na ndugu wengine wenye madaraka ambao wataijulisha Beteli hali ya ndugu wenye kupatwa na musiba

  4. Chakula na maji ya kutolea ndugu na dada wenye walipatwa na musiba

    Chakula, maji, mahali pa kulala, madawa, na musaada wa kiroho na mashauri mengine yanapaswa kutolewa haraka iwezekanavyo

  5. Ripoti kuhusu misaada yenye kuhitajiwa inachunguzwa

    Beteli inatuma ripoti ambayo inaonyesha hali ya ndugu na mambo ambayo wanahitaji kwa Halmashauri ya Waratibu ya Baraza Linaloongoza

  6. Kugawanya misaada wakati wa musiba

    Halmashauri ya Misaada Wakati wa Misiba inapanga namna misaada itatolewa na inasaidia ndugu na dada kurudilia hali yao ya mbele

  7. Ndenge yenye kuwa na misaada inaruka

    Halmashauri ya Waratibu inaangalia uhitaji, na ikiwa ni lazima, inakubali wafanyakazi wenye kujipendea kutoka inchi zingine waende kusaidia ndugu wenye kuwa katika magumu

CHOMBO KINGINE KWA AJILI YA WAFANYAKAZI AMBAO WANATOLEA NDUGU MISAADA

Jalada ya broshua Jehovah’s Witnesses and Disaster Relief

MWEZI wa 6, 2013, broshua Jehovah’s Witnesses and ­Disaster Relief ilitolewa. Ilitayarishwa hasa zaidi kwa ajili ya wakubwa mbalimbali wa serikali katika Amerika ambao wanaangalia kazi mbalimbali za misaada wakati wa misiba. Broshua hiyo ilifasiria misaada mbalimbali ambayo tumetoa wakati wa misiba kuanzia katikati ya miaka ya 1940. Ilionyesha pia karte ambayo inaonyesha kazi ya kutoa misaada ambayo inafanywa duniani pote. Muzee ambaye anasaidia katika kupanga kazi hiyo alisema hivi: “Ndugu ambao wanatumika katika Halmashauri ya Misaada Wakati wa Misiba wanatumia broshua hii ili kuzungumuza, mbele ya wakati na wakubwa wa serikali mbele ya misiba kutokea katika maeneo ambamo misiba inatokea kila mara. Wakati wakubwa hao wanajua vizuri namna tunatumika ili kutoa misaada, inakuwa rahisi kupata ruhusa ya kuingia mahali ambapo musiba ulitokea.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine