Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w12 1/12 uku. 5
  • Kuwa na Furaha ya Kutoa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kuwa na Furaha ya Kutoa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Shuguli za Watu Wakati wa Noeli
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 1/12 uku. 5

Kuwa na Furaha ya Kutoa

“Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”​—MATENDO 20:35.

Sababu inayowafanya watu wengine wafanye sikukuu ya Noeli.

Kama Yesu alivyosema, kutoa kunamuletea furaha mutu anayetoa na yule anayepokea. Ili kupata furaha hiyo, watu wengi wanaona kuwa kutoa zawadi wakati wa Noeli ni jambo la maana zaidi kuliko mambo mengine yote. Kwa mufano, hata wakati wa matatizo ya feza ya mwaka uliopita, uchunguzi fulani uliofanywa huko Irlande ulionyesha kama, kila familia ilitazamia kutumia dola karibu 660 ili kununua zawadi za kuwapatia wengine wakati wa Noeli.

Je, hiyo ni sababu yenye kufaa?

Watu wengi wanaona kama kutoa zawadi wakati wa Noeli hakuwaletee furaha nyingi lakini kunawaletea mahangaiko mengi. Namna gani? Watu wenye kununua vitu wanajisikia kuwa wanalazimishwa kununua zawadi ambazo hawana uwezo wa kununua. Na kwa sababu kila mutu anapenda kununua zawadi wakati wa Noeli, watu wengi wanajikuta kwenye mistari mirefu ya watu wanaonunua vitu na hivyo kununua vitu wakati huo linakuwa jambo lenye kuwachosha wengi.

Ni kanuni gani za Biblia zinazoweza kutusaidia?

Yesu alisema hivi: “Muwe na mazoea ya kuwapa watu.”a (Luka 6:38) Hakusema kama tunapaswa kungojea wakati fulani wa mwaka ambapo watu wanatazamia kupewa zawadi. Aliwatia wafuasi wake moyo wazoee kutoa zawadi wakati wowote.

‘Kila mumoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake, si kwa kutopenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu anamupenda mutoaji muchangamufu.’ (2 Wakorintho 9:7) Kulingana na kitabu fulani kinachoeleza Biblia, shauri hilo la Paulo linamaanisha kwamba ‘mutu yeyote asitoe kitu kwa sababu ya kulazimishwa.’ Ikiwa mutu ni ‘mutoaji muchangamufu,’ halazimike kungojea wakati fulani ili kumutolea mutu mwengine kitu fulani, kama vile watu wanazoea kufanya wakati wa Noeli.

‘Ikiwa utayari upo kwanza, hukubalika zaidi kulingana na kile ambacho mutu anacho, si kulingana na kile ambacho mutu hana.’ (2 Wakorintho 8:12) Mungu hawaombe Wakristo wajiingize katika madeni ili kuwapatia wengine zawadi za bei ya juu sana. Lakini, wakati mutu anatoa ‘kulingana na kile alicho nacho,’ zawadi zake hazifurahishe tu lakini pia ‘zinakubalika zaidi.’ Hilo ni tofauti kabisa na matangazo ya wakati wa Noeli yanayowatia watu moyo hivi: “Ununue sasa, utalipa baadaye!”

[Maelezo ya chini]

a Tafsiri fulani za Biblia zinatumia neno “toa.” Lakini, katika Kigiriki cha kwanza, neno toa linaonyesha tendo lenye kuendelea. Ili kueleza maana kamili ya neno ambalo Yesu alitumia hapo, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inatumia maneno “muwe na mazoea ya kuwapa watu.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine