Sisi Ni Wenye Furaha Kujitoa Katika Utumishi wa Yehova!
1 Mtume Paulo alifurahi “kutumiwa kabisa” ili kutimiza utumishi wake wa Kikristo. (2 Kor. 12:15) Vivyo hivyo leo, Wakristo wengi wanajikaza kutumika kama mapainia. Wengine walio na madaraka mazito ya familia wanapanga wakati ili kuhubiri kila juma hata ikiwa wana mambo mengi ya kufanya. Wengine walio na matatizo mazito ya afya wanatumia nguvu walio nayo ili kuendeleza faida za Ufalme. Ni jambo lenye kutia moyo tunapoona watu wa Yehova wakijitoa katika utumishi wake ijapokuwa miaka yao na hali zao!
2 Upendo kwa Jirani: Kufanya yote tunayoweza ili kumtumikia Yehova, kuonyesha upendo kwa Mungu na kwa jirani, kunatufanya tuwe na zamiri safi. Kwa kuwa Paulo alitoa nafsi yake ili kutangaza habari njema, aliweza kusema kwa furaha kwamba: “Ninawaita ninyi kuona ushahidi leo hii kwamba mimi ni safi kutokana na damu ya watu wote.” (Mdo. 20:24, 26; 1 The. 2:8) Kujitoa katika kazi ya kuhubiri kadiri ambavyo hali zetu zinaturuhusu kufanya hivyo, kutatuepusha kuwa na deni la damu.—Eze. 3:18-21.
3 Kujitoa sana ili kusaidia wengine kunatuletea furaha. (Mdo. 20:35) Ndugu mmoja alisema hivi: “Inapokuwa magaribi, na ninaporudi nyumbani kisha kupitisha siku nzima katika utumishi wa Yehova, ni kweli kwamba ninajisikia kuchoka. Lakini mimi ni mwenye furaha, nami ninamshukuru Yehova kwa kuwa amenipatia furaha ambayo hakuna mtu anayeweza kuninyanganya.”
4 Upendo kwa Mungu: Sababu kubwa zaidi inayotuchochea kujitoa katika utumishi wa Yehova ni kwamba kufanya hivyo kunampendeza Baba yetu wa mbinguni. Upendo wetu kwa Mungu unatuchochea kutii amri zake, amri zinazotia ndani kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. (1 Yoh. 5:3) Hata wakati watu hawaonyeshi kupendezwa au wanatupinga, sisi tunaendelea kwa furaha kumtumikia Yehova kwa bidii.
5 Sasa si wakati wa kuacha kutenda. Tunaishi wakati wa mavuno. (Mt. 9:37) Kwa kawaida mlimaji anatumika saa nyingi wakati wa mavuno kwa kuwa ana wakati mchache wa kukusanya mazao ya mashamba kabla hayajaanza kuharibika. Wakati uliopangwa kwa ajili ya kazi ya mavuno ya kiroho pia ni mchache. Tukilinda akilini wakati tunamoishi, na tuendelee sisi wote kujikaza sana katika kazi ya kuhubiri.—Luka 13:24; 1 Kor. 7:29-31.