Tumepewa Hazina
1 Mtume Paulo aliona kazi ya kuhubiri aliyopewa na Mungu kuwa ya maana sana na kwa hiyo aliilinganisha na “hazina.” (2 Kor. 4:7) Alivumilia magumu na mateso alipotimiza kazi hiyo. Alihubiri kila mtu aliyekutana naye bila kuchoka. Alifanya safari nyingi zenye matatizo mengi na hatari nyingi barabarani na baharini. Namna gani tunaweza kufuata mfano wa Paulo na kuonyesha kwamba tunapendezwa sana na kazi yetu ya kuhubiri? (Rom. 11:13) Ni nini kinachofanya kazi yetu ya kuhubiri iwe ya maana sana na isiyolinganishwa na kazi nyingine?
2 Hazina ya Hali ya Juu: Mara nyingi hazina za kimwili zinatokeza maumivu mengi na kuleta faida ndogo tu au faida zisizokawia. Lakini, kazi yetu ya kuhubiri inatuletea sisi na wengine pia faida zenye kudumu. (1 Tim. 4:16) Inasaidia watu wanyoofu wamjue Yehova, wafanye mabadiliko ya maana katika maisha zao, na wapate tumaini la kweli la uzima wa milele. (Rom. 10:13-15) Kwa kuona kazi yetu ya kuhubiri kuwa ya maana sana, tunakuwa na kusudi lenye kutufanya tutosheke maishani, tunajisikia kwamba tunatimiza jambo fulani, na tunakuwa na tumaini la wakati ujao lenye kufurahisha sana.—1 Kor. 15:58.
3 Onyesha Kwamba Unapendezwa Sana na Hazina Yako: Tunaonyesha kwamba tunapendezwa sana na jambo fulani kwa kujitolea kwa ajili ya jambo hilo. Ni pendeleo kabisa kutumia wakati wetu na nguvu yetu katika kumsifu Yehova. (Efe. 5:16, 17) Namna tunavyotumia wakati wetu inapaswa kuonyesha kwamba tunapendezwa sana na mambo ya kiroho kuliko ufuatiaji wa vitu vya kimwili. Kwa kuwa tuna jambo fulani la maana sana la kutolea wengine, je, tutapenda kuhubiri kwa uchangamfu na kuwa waangalifu katika kutumia kila nafasi inayojitokeza ili kuhubiri habari njema.
4 Kwa kawaida, hazina ya bei sana haifichwi lakini inaonyeshwa wazi ili wengine waifurahie. Ikiwa tunaona kazi yetu ya kuhubiri kama hazina au kuwa ya maana sana, hivyo jambo hilo litakuwa ndilo jambo la maana sana katika maisha yetu. (Mt. 5:14-16) Tukiwa na mioyo yenye kujaa shukrani, na tufuate sikuzote mfano wa mtume Paulo na kutumia kwa faida kila nafasi inayojitokeza ili kuonyesha kwamba tunapendezwa kwelikweli na kazi yetu ya kuhubiri, na kwamba tunaiona kuwa hazina.