Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 15/9 uku. 3-6
  • Faidika na Usemi wa Biblia Wenye Kutofautisha Mawazo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Faidika na Usemi wa Biblia Wenye Kutofautisha Mawazo
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • NAMNA YA KUFAIDIKA NA USEMI WA BIBLIA WENYE KUTOFAUTISHA MAWAZO
  • Yehova Anakusanya Tena Familia Yake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Epuka Giza, Bakia Katika Mwangaza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 15/9 uku. 3-6
[Picha katika ukurasa wa 3]

Faidika na Usemi wa Biblia Wenye Kutofautisha Mawazo

Bila shaka unakubali kwamba Yesu alikuwa Mwalimu mukubwa sana kuliko wote ambao wamekwisha kuishi duniani. Pengine umejaribu kuiga njia fulani alizotumia ili kufundisha, kama vile namna alivyotumia maulizo na mifano. Lakini, je, umejaribu kufikiria namna alivyotumia mara nyingi usemi wenye kutofautisha mawazo alipokuwa akifundisha?

Watu wengi wanazoea kutumia usemi wenye kutofautisha mawazo wanapozungumuza. Wewe pia unaweza kutumia usemi huo mara nyingi pasipo hata kujua. Kwa mufano, unaweza kusema hivi: “Walisema kwamba matunda yote yameivya, lakini, matunda haya yangali mabichi.” Ao, “Zamani mutoto huyu alikuwa mwenye haya, lakini sasa haogope tena watu.”

Katika mifano kama hiyo, kwanza unazungumuzia hali ao wazo fulani; kisha unatumia maneno kama vile lakini, hata hivyo, kuliko, ao kwa upande mwingine ili kuonyesha tofauti kati ya mawazo mawili. Ao unaweza kuongeza jambo fulani linalokazia wazo ulilozungumuzia mwanzoni. Kuzungumuza hivyo kutafanya maneno yako yawe wazi na kunaweza kuwasaidia wengine waelewe yale unayosema.

Hata ikiwa usemi wenye kutofautisha mawazo hautumiwe sana katika luga fulani, tunapaswa kujua kwamba usemi huo ni wa maana sana. Sababu gani? Kwa sababu mifano mbalimbali ya usemi huo inapatikana katika Neno la Mungu lililoongozwa na roho yake. Yesu alitumia mara nyingi usemi wenye kutofautisha mawazo. Fikiria mifano hii: ‘Watu wanawasha taa na kuiweka, si chini ya kikapu cha kupimia, bali juu ya kinara cha taa.’ “Sikuja kuharibu [Sheria], bali kutimiza.” “Ninyi mulisikia kwamba ilisemwa, ‘Usifanye uzinzi.’ Lakini mimi ninawaambia ninyi kwamba kila mutu ambaye anaendelea kumutazama mwanamuke . . . ” “Ilisemwa, ‘Jicho kwa jicho na jino kwa jino.’ Hata hivyo, mimi ninawaambia ninyi: Musimupinge yeye aliye mwovu; bali yeyote anayekupiga kofi kwenye shavu lako la kuume, mugeuzie lile lingine pia.”​—Mt. 5:15, 17, 27, 28, 38, 39.

Usemi wenye kutofautisha mawazo unapatikana katika vitabu vingine vya Biblia. Usemi huo unaweza kukusaidia kuelewa jambo fulani ao kuonyesha njia nzuri zaidi ya kufanya jambo fulani. Ikiwa wewe ni muzazi, fikiria usemi huu: ‘Nanyi, akina baba, musiwe mukiwakasirisha watoto wenu, bali endeleeni kuwalea katika nizamu na mwongozo wa akilini wa Yehova.’ (Efe. 6:4) Ikiwa mutume Paulo alimaanisha tu kwamba baba (ao mama) anapaswa kumufundisha mutoto kanuni za Yehova, hilo lingekuwa jambo la hekima na la kweli. Lakini wazo lake linaeleweka waziwazi zaidi anaposema ‘musiwe mukiwakasirisha bali endeleeni kuwalea katika nizamu na mwongozo wa akilini wa Yehova.’

Katika sura hiyo ya kitabu cha Waefeso, Paulo aliandika hivi: “Tuna kushindana mweleka, si juu ya damu na mwili, bali juu ya . . . majeshi ya roho waovu katika mahali pa kimbingu.” (Efe. 6:12) Usemi huo wenye kutofautisha mawazo unakusaidia kuelewa kwamba unapaswa kupigana vita kali sana. Haupigane na wanadamu wa hali ya chini, lakini, unapigana na majeshi ya roho waovu.

NAMNA YA KUFAIDIKA NA USEMI WA BIBLIA WENYE KUTOFAUTISHA MAWAZO

Katika kitabu hichohicho cha Waefeso, utaona maandiko mengi ambamo mutume Paulo alitumia usemi wenye kutofautisha mawazo. Kufikiri kuhusu usemi huo kunaweza kutusaidia kuelewa mambo aliyokuwa akizungumuzia na kunaweza kutusaidia kuelewa waziwazi zaidi jambo tunalopaswa kufanya.

Unaweza kufurahia na kuona kuwa jambo la maana kufikiria kisanduku kinachopatikana katika habari hii kinachoonyesha usemi mbalimbali wenye kutofautisha mawazo unaopatikana katika sura ya 4 na 5 ya kitabu cha Waefeso. Unaposoma kila usemi wenye kutofautisha mawazo, fikiri kuhusu maisha yako. Jiulize hivi: ‘Kwa kweli mimi ni mutu wa namna gani? Ninatenda namna gani katika hali hii ao katika hali inayofanana na hii? Wengine wanaweza kusema kwamba ni sehemu gani ya usemi huu inayofunua hali yangu?’ Ikiwa usemi huo unaonyesha waziwazi mambo unayopaswa kubadili, jikaze kufanya mabadiliko yanayohitajiwa. Faidika na usemi huo wenye kutofautisha mawazo.

Labda unaweza kutumia kisanduku kinachopatikana katika habari hii wakati wa ibada ya familia. Kwanza, kila mushiriki wa familia yako anaweza kusoma kila usemi wenye kutofautisha mawazo. Kisha mumoja kati yenu anaweza kutaja sehemu ya kwanza ya usemi huo na kuwaachia wengine wajaribu kukumbuka jambo linalokaziwa katika sehemu ya pili. Hilo linaweza kuwasaidia muwe na mazungumuzo yenye kufurahisha katika familia kuhusu namna munavyoweza kutumikisha vizuri zaidi sehemu hiyo ya pili katika maisha yenu. Bila shaka, kuchunguza usemi mbalimbali wenye kutofautisha mawazo kwa njia hiyo kunaweza kuwasaidia watoto na watu wazima kuwa na mwenendo muzuri katika familia na mahali pengine.

[Picha katika ukurasa wa 6]

Je, unaweza kukumbuka sehemu ya pili ya usemi huu wenye kutofautisha mawazo?

Utakapoelewa vizuri zaidi faida ya usemi huo, unaweza kuanza kuuvumbua kwa urahisi, na utaona kwamba unaweza kukusaidia sana katika kazi ya kuhubiri. Kwa mufano, unaweza kumwambia musikilizaji wako hivi: “Watu wengi wanasema kwamba kila mutu ana nafsi isiyokufa, lakini tuone yale ambayo Neno la Mungu linasema kuhusu jambo hilo.” Ao unapoongoza funzo la Biblia, unaweza kuuliza hivi: “Watu wengi hapa kwetu wanaamini kwamba Mungu na Yesu ni mutu mumoja; lakini, tumeona Biblia inafundisha nini? Na wewe unaamini nini?”

Kwa kweli, Biblia inatumia usemi mbalimbali wenye kutofautisha mawazo unaoweza kutusaidia tutembee katika njia ya Mungu. Na tunaweza kutumia usemi huo ili kusaidia watu wajue kweli ya Biblia.

Mifano Fulani ya Usemi Wenye Kutofautisha Mawazo Katika Waefeso Sura ya 4 na 5

Jaribu kutumia kisanduku hiki wakati wa ibada ya familia!

[Picha]

“Tusiwe tena watoto wachanga . . . tukirushwa huku na huku . . . kupitia udanganyifu wa watu, kwa njia ya ujanja katika kutunga kosa.”​—4:14.

“Lakini tukisema kweli, na tukue kwa upendo katika mambo yote ndani yake yeye aliye kichwa, Kristo.”​—4:15.

[Picha]

‘[Mataifa] yako katika giza kiakili, . . . kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao.’​—4:18, 19.

‘Bali hamukujifunza Kristo kuwa hivyo, muradi tu mulimusikia yeye na mulifundishwa kupitia yeye.’​—4:20, 21.

[Picha]

‘Munapaswa kuondolea mbali utu wa zamani unaolingana na mwenendo wenu wa kwanza.’​—4:22.

‘Lakini . . . munapaswa kufanywa upya katika nguvu zinazoendesha akili yenu, na munapaswa kuvaa utu mupya.’​—4:23, 24.

[Picha]

“Mwizi asiibe tena.”​—4:28.

“Bali afanye kazi ya bidii, akifanya kwa mikono yake kazi iliyo njema.”​—4:28.

[Picha]

“Neno lililooza na lisitoke kinywani mwenu.”​—4:29.

“Bali neno lolote ambalo ni jema kwa ajili ya kujenga.”​—4:29.

[Picha]

‘Uchungu wote wenye uovu na hasira na gazabu na kupiga kelele na matukano na viondolewe mbali kutoka kwenu pamoja na ubaya wote.’​—4:31.

‘Bali iweni wenye fazili ninyi kwa ninyi, wenye huruma nyororo, mukisameheana kwa hiari.’​—4:32.

[Picha]

‘Uasherati na ukosefu wa usafi wa kila namna ao pupa visitajwe hata kidogo katikati yenu.’​—5:3.

“Lakini badala ya hayo, utoaji wa shukrani.”​—5:4.

[Picha]

‘Wakati mumoja ninyi mulikuwa giza.’​—5:8.

“Bali sasa ninyi ni nuru kuhusiana na Bwana.”​—5:8.

[Picha]

‘Muache kushirikiana pamoja nao katika matendo yasiyozaa matunda, ambayo ni ya giza.’​—5:11.

‘Lakini badala yake muwe hata mukiyakaripia.’​—5:11.

[Picha]

‘Endeleeni kuangalia sana kwamba jinsi munavyotembea si kama watu wasio na hekima.’​—5:15.

“Bali kama watu wenye hekima, mukijinunulia wakati unaofaa.”​—5:15, 16.

[Picha]

‘Kwa hiyo muache kuwa wenye kukosa akili.’​—5:17.

“Bali endeleeni kufahamu yale yaliyo mapenzi ya Yehova.”​—5:17.

[Picha]

‘Musiwe mukilewa divai, ambayo ina upotovu ndani yake.’​—5:18.

“Bali endeleeni kujazwa na roho.”​—5:18.

[Picha]

‘Ili [Kristo] ajipe mwenyewe kwa kutaniko likiwa na fahari, likiwa bila doa ao kunyanzi lolote la mambo hayo.’​—5:27.

“Bali liwe takatifu na bila dosari.”​—5:27.

[Picha katika ukurasa wa 6]

‘Hakuna mutu anayeuchukia mwili wake.’​—5:29.

‘Bali anaulisha na kuutunza kwa upendo, kama vile Kristo pia anavyolitendea kutaniko.’​—5:29.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine