Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • “Ukombozi Wenu Unakaribia”!
    Munara wa Mulinzi—2015 | Mwezi wa 7 15
    • 14, 15. Ni kazi gani ya kukusanya itafanyika kisha shambulizi la Gogu wa Magogu kuanza, na litafanyika namna gani?

      14 Ni nini itatokea wakati Gogu wa Magogu ataanza kushambulia watumishi wa Mungu? Biblia inasema kwamba Mwana wa binadamu ‘atawatuma malaika zake pamoja na muvumo mukubwa wa tarumbeta, nao watawakusanya pamoja watu wake waliochaguliwa kutoka kwenye zile pepo ine, kutoka mwisho mumoja wa mbingu mupaka mwisho wake mwingine.’ (Marko 13:27; Mathayo 24:31) Kazi hiyo ya kukusanya haizungumuzie wakati Wakristo watiwa-mafuta wanachaguliwa kwa mara ya kwanza. Tena, haizungumuzie wakati Wakristo watiwa-mafuta wenye wangali duniani watatiwa muhuri kwa mara ya mwisho. (Mathayo 13:37, 38) Wakristo hao watatiwa muhuri kwa mara ya mwisho muda mufupi tu mbele ya ziki kubwa kuanza. (Ufunuo 7:1-4) Kwa hiyo, kazi hiyo ya kukusanya itafanywa wakati gani? Itafanywa wakati Wakristo watiwa-mafuta wenye wangali hapa duniani watapata zawadi yao ya kuenda mbinguni. (1 Wathesalonike 4:15-17; Ufunuo 14:1) Kazi hiyo ya kukusanya itafanywa wakati fulani kisha tu Gogu wa Magogu kuanza shambulizi lake. (Ezekieli 38:11) Kisha, kama vile Yesu alisema, ‘waadilifu wataangaa kwa uangavu kama jua katika Ufalme wa Baba yao.’—Mathayo 13:43.b (Ona maelezo ya chini.)

      15 Je, hilo linamaanisha kwamba Wakristo watiwa-mafuta “watanyakuliwa”? Watu wengi wenye kujiita kuwa Wakristo wanaamini kwamba Wakristo watachukuliwa kuenda mbinguni wakiwa na mwili wa wanadamu. Pia, wanafikiri kwamba wakati Yesu atarudia kutawala dunia, watamuona na macho ya kimwili. Lakini, Biblia inasema waziwazi kwamba wakati Yesu atarudia, watu hawatamuona na macho ya kimwili. Inasema hivi: ‘Ishara ya Mwana wa binadamu itaonekana mbinguni’ na, Yesu atakuja “juu ya mawingu ya mbinguni.” (Mathayo 24:30) Biblia inasema pia kwamba ‘nyama na damu haviwezi kuuriti Ufalme wa Mungu.’ Kwa hiyo, wale wenye wataenda mbinguni watakuwa kwanza na lazima ya ‘kubadilishwa, kwa muda mufupi, kufumba na kufumbua jicho, wakati wa tarumbeta ya mwisho.’c (Ona maelezo ya chini.) (Soma 1 Wakorintho 15:50-53.) Hatutumie neno “kunyakuliwa” ili kuzungumuzia tukio hilo kwa sababu neno hilo linapatana na mafundisho ya uongo ya dini zenye kujiita kuwa za Kikristo. Lakini, Wakristo watiwa-mafuta waaminifu wenye wangali duniani watakusanywa pamoja mara moja.

  • “Ukombozi Wenu Unakaribia”!
    Munara wa Mulinzi—2015 | Mwezi wa 7 15
    • c Wakristo watiwa-mafuta wenye watakuwa wangali duniani wakati huo hawataenda mbinguni na miili yao ya nyama na damu. (1 Wakorintho 15:48, 49) Inawezekana Mungu atafanya miili yao isionekane kama vile alifanya kuhusu mwili wa Yesu.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine