-
Endelea Kuonyesha ‘Mutazamo wa Kungojea’Munara wa Mulinzi—2013 | Mwezi wa 11 15
-
-
9-11. Je, andiko la 1 Wathesalonike 5:3 limekwisha kutimia? Eleza.
9 Soma 1 Wathesalonike 5:1-3. Hivi karibuni, mataifa yatatangaza “Amani na usalama!” Ili tusidanganywe na tangazo hilo, lazima “tukae macho na kutunza akili zetu.” (1 Thes. 5:6) Ili tukae macho kiroho, acheni tuchunguze kwa kifupi matukio ambayo yametayarisha njia kwa ajili ya tangazo hilo la maana.
10 Mwishoni mwa vita ya kwanza na ya pili ya ulimwengu, mataifa yalitamani sana amani. Kisha vita ya kwanza ya ulimwengu, Ushirika wa Mataifa uliundwa ili kuleta amani. Baadaye, kisha vita ya pili ya ulimwengu, watu wengi walifikiri kwamba Umoja wa Mataifa ungeleta amani duniani. Viongozi wa serikali na wa dini walitumainia mashirika hayo ili kuletea wanadamu amani. Kwa mufano, katika 1986, Umoja wa Mataifa ulitangaza mwaka huo kuwa Mwaka wa amani wa Kimataifa. Katika mwaka huo, viongozi wa serikali na wa dini kutoka mataifa mengi waliungana na Papa wa Roma huko Assisi, Italia, ili kusali kwa ajili ya amani.
11 Hata hivyo, tangazo hilo la amani na usalama na matangazo mengine kama hayo, hayajatimiza unabii ulio katika 1 Wathesalonike 5:3. Sababu gani? Kwa sababu ‘uharibifu wa gafula’ haujatokea.
12. Tunajua nini kuhusu tangazo la “Amani na usalama”?
12 Ni nani watakaofanya tangazo hili la wakati ujao la “Amani na usalama”? Viongozi wa dini zinazojiita za Kikristo na dini nyingine watahusika namna gani? Viongozi wa serikali mbalimbali watahusika namna gani katika tangazo hilo? Maandiko hayaseme lolote. Jambo tunalojua ni kwamba hata tangazo hilo litolewe namna gani, hata liwe lenye kusadikisha namna gani, hakutakuwa “amani na usalama” wa kweli. Shetani ataendelea kuongoza ulimwengu huu. Ulimwengu huu umeoza kabisa na hautabadilika. Litakuwa jambo lenye kuhuzunisha kabisa ikiwa mumoja wetu ataamini uongo huo wa Shetani na kuunga mukono upande fulani wa kisiasa!
-
-
Endelea Kuonyesha ‘Mutazamo wa Kungojea’Munara wa Mulinzi—2013 | Mwezi wa 11 15
-
-
14. Ni nini inayoonyesha kwamba mwisho wa Babiloni Mukubwa uko karibu?
14 Babiloni Mukubwa, ni kusema, dini zote za uongo, atafikia mwisho wake ambao anastahili. ‘Watu na mataifa na luga’ hawataweza kumusaidia. Tayari tunaona alama zinazoonyesha kwamba mwisho wake uko karibu. (Ufu. 16:12; 17:15-18; 18:7, 8, 21) Leo, inaonekana wazi kwamba hana watu wa kumusaidia kwa sababu dini na viongozi wa dini wanashambuliwa sana katika vyombo vya habari. Hata hivyo, viongozi wa dini hizo za uongo wanafikiri kwamba hakuna shida yoyote. Wanajidanganya kabisa! Kisha tangazo la “Amani na usalama!,” serikali za ulimwengu huu wa Shetani zitageukia kwa gafula dini za uongo na kuziharibu kabisa. Babiloni Mukubwa atapotea milele! Bila shaka, ni lazima tujikaze kabisa kungojea kwa uvumilivu matukio hayo ya maana.—Ufu. 18:8, 10.
-