Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 6/00 uku. 1
  • ‘Iweni wakarimu, tayari kushiriki’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • ‘Iweni wakarimu, tayari kushiriki’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Iweni Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Fanya Mema na Ushiriki Pamoja na Wengine
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Kupanda kwa Wingi Kunaleta
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Chukua kwa Uzito Kazi Yako ya Kuhubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 6/00 uku. 1

‘Iweni wakarimu, tayari kushiriki’

1 Karne nyingi zilizopita, mtume Paulo aliagiza Timotheo atie waamini wenzake moyo “kufanya mema, kuwa matajiri katika kazi zilizo bora, kuwa wakarimu, tayari kushiriki.” (1 Tim. 6:18) Paulo alikumbusha pia Wakristo Waebrania wasisahau “kule kutenda mema na kule kushiriki vitu pamoja na wengine.” (Ebr. 13:16) Kwa nini aliandika maagizo hayo? Kwa kuwa alijua kwamba kungekuwa “utukufu na heshima na amani kwa kila mtu afanyaye lililo jema.”—Rom. 2:10.

2 Kwa sababu ya kuwa kwake Muumbaji, Yehova Mungu ndiye Mwenye vitu vyote. (Ufu. 4:11) Tunathamini bila shaka yale ambayo yeye anafanya na mali zake kwa ajili yetu. Ingawa ukosefu wa shukrani wa wanadamu walio wengi, Aliye Juu Zaidi anaendelea kuruhusu wote wafaidike na maandalizi yake yenye ukarimu kwa ajili ya kutegemeza uhai. (Mt. 5:45) Alitoa hata Mwana wake mpendwa zaidi kuwa dhabihu ili tuwe na uhai wa milele. Je, upendo ambao tumeonyeshwa haupaswi kutulazimisha kujionyesha wenye shukrani kwa kuwa wakarimu kuelekea wanadamu wenzetu?—2 Kor. 5:14, 15.

3 Ni nini tunaloweza kushiriki? Ni jambo lenye kufaa kwamba tutumie mali zozote tulizo nazo kwa njia yenye kupendeza machoni pa Mungu. Hakika tunataka kutegemeza kimwili na kiroho kazi ya ulimwenguni pote ya Ufalme. Bila shaka, habari njema ndiyo hazina ya thamani zaidi ambayo mtu anaweza kuwa nayo, kwa kuwa hiyo ni “nguvu ya Mungu kwa ajili ya wokovu.” (Rom. 1:16) Kwa kutumia kwa ukarimu wakati na mali zetu kila mwezi ili kushiriki katika kazi ya kuhubiri na kufundisha, huenda tukawa na uwezo wa kushiriki hazina hiyo ya kiroho pamoja na wengine, tukiwaongoza wapate uhai wa milele.

4 Yehova ni mwenye furaha sana wakati tunaposaidia wale wasio na mapato mengi. Yeye anaahidi kutubariki, na anatukumbusha pia: “Mali hazina faida kwa siku ya gazabu: lakini haki inaokoa na mauti.” (Mez. 11:4; 19:17) Kutegemeza kimwili kazi ya Ufalme na kuwa na ushiriki kamili katika kuhubiri habari njema ni njia nzuri ajabu ambazo katika hizo tunaweza kuonyesha kwamba sisi ni wakarimu kwelikweli, tayari kushiriki.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine