Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Wazazi—Musaidie Watoto Wenu Wakuwe na “Hekima kwa Ajili ya Wokovu”
    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo)—2017 | Mwezi wa 12
    • 3. (a) Namna gani Timotheo alifikia kuwa Mukristo, na namna gani alitumikisha mambo yenye alijifunza? (b) Paulo aliandikia Timotheo juu ya mambo gani tatu kuhusu kujifunza?

      3 Mutume Paulo alitembelea Listra kwa mara ya kwanza katika mwaka wa 47 kisha kuzaliwa kwa Yesu. Inawezekana ni wakati huo ndio Timotheo alijua mafundisho juu ya Ukristo. Hata kama wakati huo inawezekana Timotheo alikuwa angali kijana sana, alikuwa anatumikisha mambo yenye alijifunza. Kisha miaka mbili, akaanza kusafiri pamoja na Paulo. Kisha kupita miaka 16 hivi, Paulo aliandikia Timotheo hivi: ‘Endelea katika mambo uliyojifunza na uliyoshawishiwa kuamini, ukijua ni kutoka kwa watu gani ulijifunza haya na kwamba tangu utoto muchanga umeyajua maandishi matakatifu [Maandiko ya Kiebrania], ambayo yanaweza kukufanya ukuwe mwenye hekima kwa ajili ya wokovu kupitia imani kuhusiana na Kristo Yesu.’ (2 Tim. 3:14, 15) Ona kwamba Paulo anataja (1) kujua maandishi matakatifu, (2) kushawishiwa kuamini mambo yenye mutu amejifunza na (3) kuwa na hekima kwa ajili ya wokovu kupitia imani katika Kristo Yesu.

  • Wazazi—Musaidie Watoto Wenu Wakuwe na “Hekima kwa Ajili ya Wokovu”
    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo)—2017 | Mwezi wa 12
    • ‘KUSHAWISHIWA KUAMINI’

      5. (a) ‘Kushawishiwa kuamini,’ maana yake nini? (b) Tunajua namna gani kuwa Timotheo alishawishiwa kuamini habari njema juu ya Yesu?

      5 Ni jambo la lazima kujua maandishi matakatifu. Lakini, haitoshe tu kufundisha watoto juu ya watu na matukio yenye kuzungumuziwa katika Biblia. Timotheo ‘alishawishiwa kuamini’ pia. Katika Kigiriki, maneno hayo yanamaanisha “kuwa hakika juu ya” ao “kusadikishwa na kukubali kuwa jambo fulani ni kweli.” Timotheo alijua Maandiko ya Kiebrania tangu wakati alikuwa mutoto. Lakini, kisha wakati fulani alisadikishwa na ushuhuda wenye kuonyesha wazi kuwa Yesu alikuwa Masiya. Ao tunaweza kusema kuwa ujuzi wake ulitia nguvu imani yake. Kwa kweli, imani ya Timotheo juu ya habari njema ilikuwa yenye nguvu sana mupaka akafikia kuwa mwanafunzi mwenye kubatizwa na akaanza kutumika pamoja na Paulo katika kazi ya umisionere.

      6. Namna gani unaweza kusaidia watoto wako washawishiwe kuamini mambo yenye wanajifunza katika Neno la Mungu?

      6 Namna gani unaweza kusaidia watoto wako watie nguvu imani yao ili washawishiwe kuamini kama Timotheo? Kwanza, ukuwe muvumilivu. Inaomba wakati ili mutu akuwe na imani yenye nguvu; na kwa sababu wewe unaamini jambo fulani haimaanishe kuwa mutoto wako pia ataamini jambo hilo. Kila mutoto anapaswa kutumia ‘nguvu zake za kufikiri’ ili kutia nguvu imani yake juu ya kweli ya Biblia. (Soma Waroma 12:1.) Wewe muzazi uko na daraka la maana sana la kumusaidia kufanya hivyo, zaidi sana wakati mutoto wako anauliza maulizo. Tuzungumuzie mufano mumoja.

      7, 8. (a) Namna gani baba mumoja Mukristo anaonyesha uvumilivu wakati anafundisha mutoto wake? (b) Namna gani umetambua kuwa ni jambo la maana kuonyesha uvumilivu kama huo?

      7 Thomas, baba ya mutoto mwanamuke wa miaka 11 anaeleza hivi: “Wakati fulani mutoto wangu ananiuliza, ‛Inawezekana kuwa Yehova alitumia mageuzi ili kutokeza uzima katika dunia?’ ao, ‛Sababu gani hatujiunge na wengine, kwa mufano, kwa kufanya uchaguzi ili kujaribu kufanya mambo yakuwe muzuri zaidi?’ Wakati fulani ninapaswa kuzuia ulimi wangu ili nisitoe jibu la moja kwa moja. Jambo lenye kusadikisha mutu haiko kweli ya moja kwa moja yenye unamuelezea. Lakini, ni mambo madogo-madogo yenye kusadikisha.”

      8 Thomas anajua pia kwamba inaomba kuwa muvumilivu wakati unafundisha. Kwa kweli, uvumilivu ni sifa ya maana kwa Wakristo wote. (Kol. 3:12) Thomas anajua kama inaomba wakati na inaomba kuzungumuza na mutoto wake mara kwa mara. Anapaswa kufikiri naye kupitia maandiko ili aamini kabisa mambo yenye anajifunza. Thomas anasema hivi: “Zaidi sana kuhusu mambo ya maana, mimi na bibi yangu tunapenda kujua ikiwa mutoto wetu anaamini kabisa mambo yenye anajifunza na ikiwa anayaona kuwa yenye kupatana na akili. Ni muzuri ikiwa anauliza maulizo. Kusema kweli, ninaweza kuwa na wasiwasi ikiwa anakubali jambo fulani bila kuuliza maulizo.”

      9. Namna gani unaweza kusaidia mutoto wako aamini Neno la Mungu?

      9 Ikiwa wazazi wanafundisha watoto wao kwa uvumilivu, pole kwa pole watoto wataanza kuelewa “upana na urefu na kimo na kina” cha imani. (Efe. 3:18) Tunaweza kuwafundisha mambo yenye kupatana na miaka yao na uwezo wao. Kadiri wanaendelea kuwa na imani yenye nguvu juu ya mambo yenye wanajifunza, itakuwa vyepesi zaidi kwao kutetea imani yao mbele ya wengine, kutia ndani wanafunzi wenzao. (1 Pet. 3:15) Kwa mufano, watoto wako wanaweza kufasiria mambo yenye Biblia inasema juu ya hali ya watu wenye kufa? Wanakubali kabisa mafasirio ya Biblia juu ya jambo hilo?a Kwa kweli, unapaswa kuwa muvumilivu ili kusaidia mutoto wako aamini Neno la Mungu, lakini utapata matokeo ya muzuri.​—Kum. 6:6, 7.

      10. Kufundisha kunatia ndani jambo gani la maana?

      10 Bila shaka mufano wako ni wa maana pia ili kusaidia watoto wako wakuwe na imani yenye nguvu. Stephanie, mama mwenye kuwa na watoto watatu wanawake, anasema hivi: “Tangu wakati watoto wangu walikuwa wadogo, ninajiuliza hivi, ‘Ninaelezea watoto wangu sababu gani niko hakika kuwa Yehova iko, niko hakika juu ya upendo wake, na kuwa kanuni zake ni zenye kuwa sawa? Watoto wangu wanaweza kuona waziwazi kuwa ninamupenda Yehova kabisa?’ Siwezi kutazamia watoto wangu washawishiwe kuamini ikiwa mimi siamini.”

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine