-
Tia Nguvu Imani Yako Katika Mambo Yenye UnatumainiaMunara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo)—2016 | Mwezi wa 10
-
-
10. Ni nini ilisaidia watu wengi wakuwe na ujasiri na waendelee kuwa washikamanifu kwa Mungu?
10 Katika Waebrania sura ya 11, mutume Paulo anasema hivi: “Wanawake waliwapokea wafu wao kwa ufufuo; lakini watu wengine waliteswa kwa sababu hawakukubali kuachiliwa huru kupitia fidia [zabihu ya ukombozi] fulani, ili waupate ufufuo ulio bora.” (Waebrania 11:35) Wengi walivumilia majaribu na waliendelea kuwa washikamanifu kwa Mungu kwa sababu walikuwa na imani yenye nguvu katika tumaini la ufufuo lenye Mungu alikuwa ameahidi. Walijua kama wakati unaokuja, Yehova angewafufua na wangeishi tena milele hapa duniani. Fikiria mufano wa Nabothi na Zekaria. Walipigwa majiwe mupaka kufa kwa sababu walimutii Mungu. (1 Wafalme 21:3, 15; 2 Mambo ya Nyakati 24:20, 21) Danieli alitupwa katika shimo la simba wenye njaa, na marafiki wake walitupwa katika moto wenye kuwaka sana. Walikuwa tayari kufa kuliko kukosa ushikamanifu kwa Yehova. Wanaume hao walikuwa na imani yenye nguvu kuwa Yehova angewapatia roho yake takatifu na kuwasaidia waendelee kuvumilia mateso hayo.—Danieli 3:16-18, 20, 28; 6:13, 16, 21-23; Waebrania 11:33, 34.
-
-
Tia Nguvu Imani Yako Katika Mambo Yenye UnatumainiaMunara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo)—2016 | Mwezi wa 10
-
-
12. Mufano muzuri zaidi wenye tunaweza kuiga ni wa nani? Ni nini ilimusaidia avumilie majaribu
12 Yesu Kristo alivumilia jaribu kali zaidi na aliendelea kuwa mushikamanifu kwa Yehova. Ni nini ilimusaidia avumilie? Mutume Paulo alisema hivi: ‘Kwa ajili ya shangwe iliyowekwa mbele yake, yeye alivumilia muti wa mateso, akaizarau aibu [haya], naye ameketi kwenye mukono wa kuume wa kiti cha ufalme cha Mungu.’ (Waebrania 12:2) Kisha, Paulo alitia Wakristo moyo ‘wafikirie sana’ mufano wa Yesu. (Soma Waebrania 12:3.) Kama Yesu, Wakristo wengi wa wakati wa mitume walikufa kwa sababu walikuwa washikamanifu kwa Yehova. Mumoja wa Wakristo hao ni Antipa. (Ufunuo 2:13) Wakristo hao wamekwisha kupata zawadi yao. Lakini watumishi wengine wa Mungu wenye waliishi mbele yao walingojea kwa hamu kuishi duniani. (Waebrania 11:35) Wakati fulani kisha Yesu kuwa Mufalme katika mwaka wa 1914, Wakristo watiwa-mafuta wenye walikuwa wamekufa walifufuliwa na kupata uzima wenye hauwezi kufa mbinguni, na watatawala wanadamu pamoja naye.—Ufunuo 20:4.
-