Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 9/15 uku. 3-6
  • Namna ya Kuwa na Mawazo ya Muzuri Juu ya Feza

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kuwa na Mawazo ya Muzuri Juu ya Feza
  • Amuka!—2015
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • FEZA NA UBAGUZI
  • MAMBO BIBLIA INASEMA
  • UKO NA MAWAZO GANI JUU YA FEZA?
  • Makuta Njo Chanzo ya Mambo Yote ya Mubaya?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Feza
    Amuka!—2014
  • Namna ya Kutumia Feza Vizuri
    Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
Amuka!—2015
g 9/15 uku. 3-6
Mwanaume mumoja anaangalia marundo marefu sana ya feza za vichele

HABARI KUBWA

Namna ya Kuwa na Mawazo ya Muzuri Juu ya Feza

WATU wanazoea kusema hivi: “Feza njo mambo yote.” Maneno hayo ni ya kweli katika njia fulani. Kwa kweli, inaomba kuwa na feza ili kuuza chakula, nguo, na kulipia ao kuuza nyumba. Muandikaji mumoja wa mambo ya feza aliandika hivi: “Feza ziko na kazi ya maana sana katika maisha ya watu. Ikiwa tungeacha kutumia feza ili kuuza ao kuuzisha, kisha mwezi moja tu, tunaweza kuingia katika hali ya woga na vita.”

Lakini, feza ziko na mipaka. Arne Garborg, muandikaji mumoja wa Norwe (Norvège) alisema kama kupitia feza “unaweza kununua chakula, lakini hapana hamu ya kula; matunzo, lakini hapana afya; vitanda vya muzuri, lakini hapana usingizi; ujuzi, lakini hapana hekima; vitu vyenye kuvutia, lakini hapana uzuri; utukufu, lakini hapana upendo; mambo ya kujifurahisha, lakini hapana furaha; watu wenye unajuana nao, lakini hapana marafiki wa kweli; watumishi, lakini hapana uaminifu.”

Wakati mutu anaendelea kuwa na mawazo ya muzuri juu ya feza, ni kusema, kuziona kuwa njia ya kutimiza mambo fulani kuliko kuziona kuwa kusudi la kwanza katika maisha, anaweza kuwa na furaha kwa kiasi fulani. Biblia inatoa angalisho kwamba “kupenda pesa [feza] ni chanzo cha mambo mabaya ya namna zote, na kwa kujitahidi [kujikaza] kufikia upendo huo wengine . . . wamejichoma wenyewe kila mahali kwa maumivu mengi.”—1 Timotheo 6:10.

Ujue kama ni upendo wa feza ndio unaleta mambo mabaya, lakini haiko feza zenyewe. Ndiyo, kupenda feza sana kunaweza kuleta mugawanyiko kati ya marafiki na kati ya watu wa familia. Ona mifano fulani.

Feza zinaangukia kwenye rundo la feza

Daniel:a “Sikuzote, nilimuwazia rafiki yangu Thomas kuwa mutu muzuri na mwenye kutumainika. Nilikuwa sijapata magumu naye hata siku moja mupaka wakati aliuza motokari yangu yenye nilikuwa nilisha kutumikisha. Sikujua kama motokari yangu ilikuwa na tatizo fulani. Hata hivyo, aliitika kuandika makubaliano ili kuuza motokari hiyo katika hali ilikuwa. Miezi tatu kisha hapo, motokari hiyo iliharibika. Thomas aliona kuwa nilimudanganya na kwa hasira alikazia nimurudishie feza zake. Nilishangaa sana! Wakati nilipima kuzungumuza naye juu ya jambo hilo, akakuwa mukali na mwenye hasira sana. Hakukuwa tena Thomas mwenye nilijua, kwa sababu tu ya mambo ya feza, alibadilika.”

Esin: “Katika familia yetu, tulizaliwa tu mimi na Nesrim. Tulikuwa tunapatana muzuri, na hata siku moja sikuwaza kama urafiki wetu unaweza kuharibika kwa sababu tu ya mambo ya feza. Lakini ni vile ilitokea kabisa. Wakati wazazi wetu walikufa, walituachia uriti kidogo na wakasema kama tugawanye feza sawasawa. Dada yangu hakuheshimu mambo wazazi wetu walisema na akaomba zaidi ya ile alipaswa kupewa. Lakini, kwa sababu niliamua kuheshimia maagizo ya wazazi wetu, alikasirika sana na kusema maneno yenye kuniogopesha. Mupaka leo, anaendelea kunikasirikia sana.”

FEZA NA UBAGUZI

Kuwa na mawazo mabaya juu ya feza kunaweza kufanya mutu akuwe na tabia ya kuhukumu wengine. Kwa mufano, tajiri anaweza kuona kama masikini wako wavivu sana, hawafanye kitu ili maisha yao yakuwe ya muzuri. Ao masikini anaweza kuona kama matajiri wanapenda sana vitu vya kimwili na wako na tamaa. Leanne, kijana mwenye kuwa katika familia tajiri, alipambana na ubaguzi kama huo. Anasema hivi:

Mashauri ya Biblia juu ya feza yangali ya maana leo kama vile yalikuwa wakati yaliandikwa

“Nilijulikana kuwa kijana mwanamuke mwenye baba iko na feza nyingi sana. Kwa hiyo, mara nyingi marafiki wangu waliniambia maneno kama haya: ‘Kama unapenda kupata kitu fulani, umuombe tu Baba yako’ ao ‘Sisi wote hatuko matajiri na hatuna uwezo wa kupata motokari nyingi za muzuri kama vile familia yenu.’ Mwishowe, niliomba marafiki wangu waache kusema maneno kama hayo, na niliwafasiria sababu gani maneno yao yaliniumiza. Sikupenda kujulikana kuwa mutu mwenye feza, lakini nilipenda kujulikana kuwa mutu mwenye kutendea wengine mambo ya muzuri.”

MAMBO BIBLIA INASEMA

Biblia haiseme kama feza ni mubaya na haiseme mubaya juu ya watu wenye kuwa na feza, hata wale wenye kuwa na feza nyingi. Shida haiko wingi wa feza zenye mutu iko nazo lakini ni mawazo yake juu ya feza zenye iko nazo ao zile anataka kupata. Mashauri ya Biblia juu ya feza ni yenye usawaziko, na yangali ya maana leo kama vile yalikuwa wakati yaliandikwa. Ona mifano yenye kufuata.

BIBLIA INASEMA HIVI: “Usijitaabishe kutafuta utajiri.”—Methali 23:4.

Kitabu kimoja kinasema kama watu wenye kutafuta sana utajiri wanaweza kwa vyepesi “kupatwa na matatizo ya akili, tena wako na matatizo ya kimwili, kama vile maumivu ya koo, ya mugongo, na ya kichwa na walikuwa wanakunywa pombe sana na kutumia dawa za kulewesha. Inaonekana kama kutafuta sana kuwa na feza nyingi kunafanya watu wakuwe wenye huzuni sana katika maisha.” (The Narcissism Epidemic)

BIBLIA INASEMA HIVI: ‘Namna yenu ya maisha ikuwe bila upendo wa pesa, huku mukirizika na vitu vya sasa.’—Waebrania 13:5.

Mutu mwenye kurizika ao mwenye kufurahia yenye iko nayo anaweza pia kuwa na mahangaiko ya feza, lakini anajua namna ya kuzuia mahangaiko hayo. Kwa mufano, mutu mwenye kurizika hahangaike kupita mipaka wakati anapata matatizo ya feza. Lakini, anajikaza kuwa na mawazo kama ya mutume Paulo, mwenye aliandika hivi: ‘Kwa kweli ninajua jinsi ya kupungukiwa na vyakula, kwa kweli ninajua jinsi ya kuwa na wingi. Katika mambo yote na katika hali zote nimejifunza siri ya jinsi ya kushiba na pia jinsi ya kuwa na njaa, jinsi ya kuwa na wingi na pia jinsi ya kupatwa na uhitaji.’—Wafilipi 4:12.

BIBLIA INASEMA HIVI: “Anayetegemea [anayetumainia] utajiri wake—yeye mwenyewe ataanguka.”—Methali 11:28.

Wachunguzi wanasema kama ndoa nyingi zinavunjika kwa sababu ya matatizo ya feza. Matatizo ya feza yamefanya pia watu wajiue. Watu fulani wanaona feza kuwa za maana zaidi kupita kiapo chao cha ndoa ao hata kupita maisha yao! Lakini, watu wenye kuwa na mawazo ya muzuri juu ya feza hawatumainie feza. Wanatambua kuwa maneno haya ya Yesu ni ya hekima: ‘Hata wakati mutu ana vitu vingi uzima wake hautokane na vitu alivyo navyo.’—Luka 12:15.

UKO NA MAWAZO GANI JUU YA FEZA?

Mwanaume mwenye kuwa na marundo ya feza pembeni yake, anajichunguza katika kioo

Kama unajichunguza, unaweza kuona ikiwa uko na lazima ya kuwa na mawazo ya muzuri juu ya feza. Kwa mufano, ujiulize maulizo yenye kufuata.

  • Ninavutiwa na mipango ya kuwa tajiri haraka?

  • Ni vigumu kwangu kutolea wengine feza zangu?

  • Ninafanya urafiki na watu wenye wanazoea kuzungumuza juu ya feza na vitu vyenye wako navyo?

  • Ninatumia uongo ao tabia zingine mbaya ili kupata feza?

  • Feza zinanifanya nijione kuwa mutu wa maana?

  • Ninawaza sikuzote juu ya feza?

  • Mawazo yangu juu ya feza yanaleta matokeo mabaya juu ya afya na familia yangu?

    Ukuwe mutoaji kwa wengine

Ukijibu ndiyo kwa ulizo fulani kati ya maulizo hayo, ufanye nguvu ili kupinga mawazo na vishawishi vyenye kufanya upende vitu vya kimwili. Uepuke kufanya urafiki na watu wenye kuona feza na vitu vya kimwili kuwa vya maana sana. Lakini, ufanye urafiki na watu wenye kuona kanuni za mwenendo muzuri kuwa za maana sana kuliko vitu vya kimwili.

Usiruhusu hata kidogo upendo wa feza ukomae katika moyo wako. Lakini, utie feza pa nafasi yake, ni kusema, utie pa nafasi ya kwanza marafiki wako, familia yako, afya yako ya kimwili na ya moyoni, na feza pa nafasi ya pili. Kwa kufanya hivyo, utaonyesha kama uko na mawazo ya muzuri juu ya feza.

a Majina yamebadilishwa katika habari hii.

Wanawake wawili wanaangaliana kwa hasira

FAMILIA NI YA MAANA SANA KUPITA FEZA

“Hivi karibuni baba yangu alifanya uamuzi juu ya uriti; uamuzi huo ulipunguza sana sehemu ya uriti wenye ningepata, na kuongeza sehemu ya uriti wenye ndugu zangu wangepata. Lakini tulizungumuzia jambo hilo. Ninaelewa muzuri mawazo yake, na ninakubali uamuzi wake. Sitaruhusu hata siku moja kitu chochote cha bure kama vile feza kilete migawanyiko katika familia yetu.”—Josué, mwenye miaka 55.

FEZA NA UPENDELEO

‘Masikini ni chukizo hata kwa mwenzake, lakini tajiri ana rafiki wengi.’—Methali 14:20.

Kama vile andiko hilo la Biblia linaonyesha, mawazo yetu juu ya feza yanaweza kuwa na matokeo juu ya namna tunatendea watu. Kwa mufano, tunaweza kuwa na mwelekeo wa kuzarau masikini wenye hawawezi kutufanyia kitu chochote. Kwa upande mwengine, tunaweza kuwa na mwelekeo wa kuwasifu-sifu matajiri, kujipendekeza kwao ili kutafuta watupende, pengine ili watupatie feza.

Biblia haikubali watu wenye kuonyesha upendeleo, kwa kuzarau wenye kuwa masikini ao kwa ‘kuwasifu kwa kustaajabia watu mashuhuri kwa ajili ya faida yao.’ (Yuda 16; Isaya 10:1, 2) Ujiwekee mupango wa kuwaona watu wote kuwa sawa na kuwatendea sawasawa.

Hekima Ya Biblia

Biblia inakubali kuwa . . .

  • “Pesa [feza] ni ulinzi.” —MHUBIRI 7:12.

Lakini Biblia inatoa angalisho kuwa . . .

  • “Yeye anayefanya haraka kupata utajiri hatabaki pasipo hatia.”—METHALI 28:20

  • ‘Wale ambao wameazimia kuwa matajiri wanaanguka katika jaribu na mutego na tamaa nyingi za kijinga na zenye kuzuru.’—1 TIMOTHEO 6:9.

Kwa hiyo, Biblia inashauria kuwa . . .

  • ‘Namna yenu ya maisha ikuwe bila upendo wa pesa.’ —WAEBRANIA 13:5.

  • ‘Mujilinde na kila namna ya tamaa, kwa sababu hata wakati mutu ana vitu vingi uzima wake hautokani na vitu alivyo navyo.’ —LUKA 12:15.

  • ‘Musisahau kutenda mema na kushiriki vitu pamoja na wengine.’—WAEBRANIA 13:16.

Utapata faida gani kwa kufuata mashauri hayo?

  • “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”— MATENDO 20:35.

  • “Nafsi yenye ukarimu hiyo yenyewe itanoneshwa, naye anayenywesha wengine kwa ukarimu yeye mwenyewe pia atanyweshwa kwa ukarimu.” —METHALI 11:25.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine