-
“Mukumbuke Wale Wenye Wanaongoza Kati Yenu”Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
-
-
JUU YA NINI ‘TUKUMBUKE WALE WENYE WANAONGOZA’?
9 Kuko sababu mingi zenye zinafanya ‘tukumbuke wale wenye wanaongoza’ na kuonyesha kama tunawatumainia. Juu ya nini kufanya vile ni jambo ya lazima? Mutume Paulo alisema hivi: “Wanaendelea kuwalinda ninyi kama wale wenye watatoa hesabu, ili wafanye vile kwa furaha, hapana kwa kusumbuka, kwa maana jambo hilo lingewaumiza ninyi.” (Ebr. 13:17) Ni lazima tunyenyekee na kutii muongozo wa wale wenye kutuongoza juu wanaendelea kutulinda kiroho na kutusaidia tukuwe mu hali ya muzuri.
10 Mu 1 Wakorinto 16:14, Paulo alisema hivi: “Mambo yote yenye munafanya, yafanywe kwa upendo.” Maamuzi yote yenye inakamatwa kwa ajili ya watu wa Mungu inategemea ile sifa ya maana sana, ni kusema, upendo. Kuhusu upendo, 1 Wakorinto 13:4-8 inasema hivi: “Upendo ni wenye uvumilivu na wenye fazili. Upendo hauna wivu. Haujisifu, haujivune, haujiendeshe bila adabu, hautafute faida zake wenyewe, haukasirike haraka. Hauweke hesabu ya ubaya. Haufurahie ukosefu wa haki, lakini unafurahi pamoja na kweli. Unafunika mambo yote, unaamini mambo yote, unatumaini mambo yote, unavumilia mambo yote. Upendo haushindwe hata kidogo.” Wale wenye kuongoza wanakamataka maamuzi kwa upendo na kwa faida ya watumishi wa Yehova. Njo maana, namna wako natuongoza haipaswe kutuogopesha. Tena, tukumbuke kama ile ni njia yenye Yehova anatumia ili kuonyesha kama anatupenda.
Ni jambo ya maana tujinyenyekeze kwa wale wenye kuongoza, juu wanaendelea kutuhangaikia ili tukuwe na hali ya muzuri ya kiroho
11 Wakati ya mitume, Yehova alitumia watu wenye hawakamilike ili kuongoza watumishi wake. Na njo vile iko nafanya leo. Mu Biblia muko mifano yenye kuonyesha kama, zamani sana Yehova alikuwa natumia watu wenye hawakamilike ili kutimiza mapenzi yake. Kwa mufano, Noa alijenga safina na kuhubiria watu juu ya uharibifu wenye ulitokea mu ile wakati yake. (Mwa. 6:13, 14, 22; 2 Pe. 2:5) Musa alichaguliwa ili kutosha watu wa Yehova kule Misri. (Kut. 3:10) Roho ya Mungu iliongoza wanaume wenye hawakamilike ili waandike Biblia. (2 Ti. 3:16; 2 Pe. 1:21) Hata kama leo Yehova iko natumia wanaume wenye hawakamilike ili kuongoza kazi ya kuhubiri na ya kufanya wanafunzi, ile haipaswe kufanya tukose kutumainia tengenezo yake. Tofauti na ile, tunatiwa moyo juu tunajua kama hakuna kitu inaweza kufanyika mu tengenezo bila Yehova kusaidia. Mambo yenye mutumwa muaminifu anafanyaka wakati ya magumu na mu hali mbalimbali, inatuhakikishia kama ni roho ya Mungu njo iko namuongoza. Leo, sehemu yenye kuonekana ya tengenezo ya Yehova iko napata baraka mingi sana. Njo maana, tunapaswa kuiunga mukono na kuitumainia kwa moyo wote.
-
-
“Mukumbuke Wale Wenye Wanaongoza Kati Yenu”Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
-
-
14 Tena, tunaonyesha kama tunatumainia tengenezo ya Yehova kwa kuunga mukono maamuzi yote yenye ile tengenezo inakamata. Tunaweza kufanya vile kwa kufuata kwa unyenyekevu miongozo yenye waangalizi wa mizunguko na wazee wengine wa kutaniko wako natupatia. Wale ndugu wako kati ya “wale wenye wanaongoza.” Kwa hiyo, tunapaswa kuwatii kwa unyenyekevu. (Ebr. 13:7, 17) Hata kama hatuelewe muzuri juu ya nini walikamata maamuzi fulani, tunapaswa kuiunga mukono, juu tunajua kama itatuletea furaha ya wakati murefu. Na Yehova atatubariki kama tunatii Neno yake na tengenezo yake. Kwa kufanya vile, tunaonyesha kama tunatii kabisa Bwana wetu, Yesu Kristo.
-